Alhamisi, 14 Desemba 2017

UVCCM YAIPUKUTISHA ACT-WAZALENDO, CUF NA CHADEMA.

 BAADHI ya Viongozi na wanachama wa ngazi za juu kutoka vyama vya upinzani waliojiunga na CCM baada ya kuvutiwa na Sera za Chama cha Mapinduzi.

NA IS-HAKA OMAR, DODOMA.

WANACHAMA 200 wakiwemo viongozi waandamizi wa kitaifa wa vyama vya upinzani wengi wakiwa ni kutoka ACT Wazalendo, CHADEMA na CUF  wamejiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Viongozi hao wamepokewa na Mwenyekiti mpya wa UVCCM Taifa Kheir James kwenye hafla fupi ya makaribisho iliyoandaliwa na umoja huo mkoa wa Dodoma na kufanyika Makao Makuu ya CCM (White House) mjini hapa.

Wakizungumza  kwa nyakati tofauti kwenye hafla hiyo baada ya kukabidhiwa kadi mpya aliyekuwa Ofisa wa Sheria Makao Makuu ya ACT Wazalendo, Mwantumu Mgonja, amesema ameamua kujiondoa katika chama hicho kwa kukosekana uwazi, demokarsia na mipango thabiti kama chama cha siasa.

Mwantumu alisema ndani ya chama hicho licha ya kukosekana uwazi, uwajibikaji na ukosefu wa majadiliano kwa msingi wa kujenga na kuendelea mbele, hakina malengo ya kuleta mabadiliko aliyoyatarajia.
"Nimeona ni heri nijiondoe kwenye chama ambacho hakina dira, mipango na sera lakini pia nimevutiwa na utendaji wa serikali ya awamu ya tano katika kukuza dhana ya uzalendo na kupigania matumizi ya rasimali za nchi kwa maslahi ya wananchi,"alieleza Mwantumu.
Naye Julius Kamabrage aliyekuwa Mwenyekiti wa ACT Wazalebdo jimbo la Butima mkoani Mara na kuwa mgombea wa ubunge katioka jimbo hilo, alisema upinzani umepoteza maana na matarajio na sasa hauna ajaenda.
Kambarage alisema ana idadi kubwa ya wenyeviti na wajumbe wa serikali za vijiji na vitongoji kwenye wilaya na mkoa wa mara ambao wote watarejea CCM na kujiondoa kwenye vyama vya upinzani.

"Upinzani umekabidhiwa majimbo mawili mkoa wa Mara pamoja na kuongoza halmashauri mbili za wilaya, lakini hakuna lolote wanalolifanya huku wananchi wakikosa uwakilishi sahihi na kuweza kutatua shida na matatizo yao,"Alieleza Kambarage.

Kwa upande wake mwenyekiti mpya wa UVCCM Taifa, Kheir James, aliwakaribisha vijana hao katika kikosi cha ushindi na kuwataka kuongeza nguvu ya ushindi na kujenga Chama imara kinachotumainiwa na wananchi wote.
Kheir alisema vijana wote hawana mahali pa kwenda na sehemu sahihi kwao ni CCM, hivyo kurudi kwao ndani CCM kutafungua milango zaidi ya kuitumikia nchi, kuwa watii, wazalendo na wenye wajibu wa kujituma na kuzalisha mali.

Kati ya wanachama 200 waliojiunga na CCM 15 kati yao ndiyo waliokabidhiwa kadi mpya za Chama akiwemo Mwantumu, Mwenyekiyti wa Vijana Mkoa wa Mwanza kupitia ACT Wazalendo, Ramadhani Itenya, Katibu wa chama hicho Mkoa wa singida, Loth Thomas, Aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Kata ya Mabibo, Dar es Salaam, Jackob Mosha  na aliyekuwa Ofisa Utawala ACT Wazalendo, Emmanuel Kitundu.
Wengine ni Mwenyekiti wa Vijana ACT Wazalendo Wilaya ya Ilala, Rose Peter, Mwenyekiti wa chama hicho Jimbo la Singida Mjini, Nkamia John, Katibu wa ACT Wazalendo Mkoa wa Mwwanza, Robert Gwanchele, aliyekuwa msanii wa CHADEMA, Andrew Mgalama, Pascal Waruba kutoka ACT Wazalendo Wilayaya Tarime, Katibu Mipango na Uchaguzi ACT Wazalendo Tarime, Anthon Mrigini Katibu wa Vijana Wilaya ya Tarime, Yaassin Daud na Julius Sinda Katibu wa CUF Wilaya ya Tarime.
Hafla hiyo alihudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara) Rodrick Mpogolo, Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Zanbzibar) Dk. Abdalla Juma Mabodi, Katibu wa Halmashauri Kuu ya (NEC) ya CCM, Idara ya Itikadi na Uenezi, Hamprey Polepole na Katibu wa NEC, Oganaizesheni na Siasa, Pereira Ame Silima.


Wengine ni Makamu Mwenyekliti wa UVCCM Taifa, Tabia Mwita, Kaimu Katibu Mkuu wa UVCC, Shaka Hamadu Shaka na Katibu wa UVCCM Mkoa wa Dodoma, Asia Halamga na Mwenyekiti wa umoja huo mkoani humo, Bill Chidabwa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni