Ijumaa, 15 Desemba 2017

KINANA-AWATAKA WANA CCM SINGIDA KASKAZINI KUWAKATAA WANASIASA UCHWALA NA MADALALI WA KISIASA



  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mjumbe wa kamati kuu ya siasa ya Mkoa,Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt Rehema Nchimbi mara baada ya kuwasili katika Kata ya Ilongero,Singida vijijini katika jimbo la Singida la Kaskazini. 
 Mjumbe wa kamati kuu ya siasa ya Mkoa,Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt Rehema Nchimbi akizungumza mapema jana kwenye mkutano wa Halmashauri kuu ya Wilaya uliokuwa ukifanyika jana katika kata ya Ilongero, Singida vijijini katika jimbo la Singida la Kaskazini,ambapo Chama cha Mapinduzi


Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Singida Juma Kilimba akimkaribisha Mgeni rasmi,Katiibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana aliyepita kuwasalimia na kuona wamejiandaaje na uchaguzi wao wa kura za maoni kwa ajili ya kumchagu Mtu atakaewawakilisha katika uchaguzi Mdogo wa Ubunge unaotarajiwa kufanyika hivi karibuni.
Katibu MKuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza mapema kwenye mkutano wa Halmashauri kuu ya Wilaya uliokuwa ukifanyika jana katika kata ya Ilongero, Singida vijijini katika jimbo la Singida Kaskazini.


 Baadhi ya Wananchi waliovutiwa na hotuba ya Katibu Mkuu Ndg.Kinana,ilibidi wasogee zaidi na kuendelea kusikiliza.



TAARIFA NA  IS-HAKA OMAR..

KATIBU Mkuu wa Chama cha Mapinduzi(CCM) Taifa, Abdulrahman Omar Kinana amewataka  wanachama wa Chama hicho kutofanya makosa ya kuchagua kiongozi asiyekuwa na msimamo wala uzalendo wa kweli  kwa jamii anayoitumikia.

Maelekezo hayo ameyatoa jana wakati akizungumza na wanachama wa CCM kabla hawajapiga kura ya maoni za kumchagua  mwana CCM atakayepeperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi mdogo utakaofanyika hivi karibuni kumtafuta Mbunge wa jimbo la Singida Kaskazini.

Katibu Kinana, amewambia wanachama hao kwamba CCM kwa sasa haina muda wa marumbano wala kujadili wanasiasa na vyama vilivyopoteza muelekeo kisiasa, bali chama kina muda wa kutatua kero za wananchi.

Amesema kwa sasa wananchi wanatakiwa kuendelea kumuunga mkono  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa juhudi zake za kupambana na vitendo vya rushwa na ufisadi.

“Sote ni mashahidi jinsi serikali ya awamu ya tano inavyopigania haki na maisha ya wananchi wote bila ubaguzi wa dini, kabila na rangi wote mnapata haki sawa.

Pia ni wakati wenu wa kuwakataa wanasiasa uchwala na madalali wa kisiasa wenye nia ya kujineemesha wao huku wananchi mkibaki na dhiki, chama pekee chenye sera zinazojali na kuthamini maisha ya watu ni CCM wala hakuna kingine”.amewambia wanachama hao Kinana.

Uchaguzi huo utafanyika kufuatia aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo, Lazaro Nyarandu kwa tiketi ya CCM Kujivua uachama wa Chama cha Mapinduzi na kujiuzulu nyadhifa zake zote.






Hakuna maoni:

Chapisha Maoni