Jumatano, 27 Desemba 2017

MAKAMU MWENYEKITI UVCCM TAIFA TABIA MWITA - ASEMA UCHAGUZI UMEKWISHA KILICHOBAKI NI KUFANYA KAZI KWA BIDII

MAKAMU Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Tabia Maulid Mwita akizungumza katika hafla ya  mapokezi hayo kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti.
NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR.

MAKAMU Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM)Taifa,  Tabia Maulid Mwita amewataka vijana kuvunja makundi yote yaliyoundwa wakati wa kampeni za uchaguzi na badala yake libaki kundi moja la UVCCM litakalotetea na kusimamia maslahi ya vijana wote wa Tanzania.

Rai hiyo ameitoa leo katika hafla ya mapokezi ya viongozi wa jumuiya hiyo ngazi ya Taifa waliofika Zanzibar kwa mara ya kwanza tokaka wachaguliwe kupitia Mkutano Mkuu wa Tisa wa UVCCM uliofanyika wiki kadhaa zilizopita Mjini Dodoma.

Amesema uchaguzi umekwisha na tayari viongozi wa ngazi mbali mbali wamechaguliwa hivyo kilichobaki kwa viongozi hao ni kuwatumikia vijana wa Umoja kwa ufanisi.

Amesema changamoto zinazoikabili UVCCM zitatafutiwa ufumbuzi wa kudumu endapo vijana mbali mbali wa umoja huo watakuwa tayari kushirikiana na viongozi wao katika kutathimini na kubuni mikakati mipya ya kuleta maendfeleo ndani ya umoja huo.

“ Ndugu zangu wapendwa na vijana wenzangu wa UVCCM nakupendeni sana lakini ushauri wangu kwenu ni kwamba tufanye kazi kwa bidii ili umoja wetu uendelee kuwa na heshima ya ndani na nje ya Chama cha Mapinduzi.

Pia uchaguzi umekwisha lakini pia makundi ya kuharisha uhai wa jumuiya yetu, rushwa na ufisadi tuyapige vita kwani hayatatusaidia bali yatatutafuna na kudhohofisha taasisi yetu.”, amesema Makamu Mwenyekiti huo.

Hata hivyo amewashukru vijana mbali mbali wa umoja huo wanaoendelea kuonyesha upendo na mshikamano kwa uongozi mpya wa ngazi ya taifa uliochaguliwa kuongoza kwa miaka mitano ijayo.


Amewambia mamia ya vijana waliojitokeza katika mapokezi hayo kwamba Umoja huo umejipanga kufanya mageuzi makubwa katika masuala ya  uongozi na kiuchumi kwa lengo la kufanya taasisi hiyo kuwa kimbilio la kudumu kwa vijana.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni