Jumanne, 30 Aprili 2019

DK.MABODI-ASEMA MUUNGANO NI CHIMBUKO LA MAENDELEO YA ZANZIBAR NA TANZANIA BARA.

 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Mabodi (wa kwanza kulia), Mkurugenzi Mtendaji wa Bomba FM Radio Munir Zakaria (wa pili kulia) na Mhariri Mkuu wa Bomba FM Radio Mwinyi Saadalla (wa kwanza kushoto) wakiwa katika Mahojiano Maalum ya Miaka 55 ya Muungano wa Zanzibar na Tanganyika pamoja na Utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2015/2020 kwa upande wa Zanzibar.


NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla ‘Mabodi’  amesema CCM inaamini kuwa Muungano wa Serikali mbili ya Zanzibar na Tanganyika ndio chimbuko la Maendeleo endelevu yaliyofikiwa katika Nyanja za Kiuchumi, Kijamii na Kisiasa.

Amesema Siri ya kudumu kwa Muungano huo  hadi kufikia miaka 55 ni kutokana na kujikita katika Undugu wa Damu badala ya Maslahi binafsi ya kila Nchi, hali iliyopelekea kuwepo kwa kuaminiana, kushauriana na kuheshimiana katika kutatua changamoto za Muungano huo.

Ufafanuzi huo ameutoa leo katika Mahojiano Maalum  ya Miaka 55 ya Muungano  na Utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2015/2020 yaliyorushwa Mubashara (Live) kupitia Kituo cha Redio ya Bomba FM iliyopo Uwanja wa Ndege Zanzibar.

Dk.Mabodi ameeleza kuwa huwezi kuutaja Muungano huo bila kueleza Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964 pamoja na Uhuru wa Tanganyika wa mwaka 1961, ambavyo ndio chachu ya Ukombozi,Utu na Ustawi wa kijamii kwa Wananchi wa pande zote za Muungano.

Amesema Waasisi wa Muungano huo ambao ni Marehemu Mzee Abeid Aman Karume na Hayati Mwl.Julius Kambarage Nyerere waliamua kuunda Mfumo huo kwa kutafakari kwa kina maendeleo na fursa za Kijamii za Wananchi waliowaongoza kwa wakati huo.

Amesema haikuwa kazi rahisi Nchi ndogo ya Zanzibar kukubali iungane na Nchi kubwa ya Tanganyika lakini kupitia mashauriano ya Vikao vya Wazee na ridhaa ya Wananchi wenyewe yalizaa matunda ya kufikia mwafaka wa kuingia katika Mfumo huo ili kushirikiana katika masuala ya Kiuchumi,Kisiasa, kimaendeleo na kijamii.

Naibu Katibu Mkuu huyo wa Zanzibar Dk.Mabodi alisema Muungano huo ulikuwa na changamoto zaidi ya 15 zilizotatuliwa hatua kwa hatua ambapo hivi sasa zimebaki nne na 11 tayari zimetafutiwa ufumbuzi wa kudumu.

Amewapongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein pamoja na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli kwa kusimamia ipasavyo utatuazi wa changamoto hizo za Muungano hatua iliyoendelea kuleta ufanisi katika masuala ya Kiuchumi.

Amesema changamoto nne zilizobaki nazo zikitafutiwa ufumbuzi zitaibuka zingine kutokana na asili ya maisha ya binadamu kwani kila siku Watu wanazaliwa na mahitaji yanaongezeka kutokana na mahitaji ya wakati husika.

“Katika Utawala wa Serikali ya Awamu ya Saba ya Dk.Shein  na Awamu ya Tano ya Dkt.Magufuli changamoto hizi zimetatuliwa kwa kasi kubwa sana na zilizobaki zitatuliwa wakati wowote kwa njia ya Vikao vya pande zote mbili.

Wananchi waendelee kuamini kwamba Serikali zao zipo makini sana katika kusimamia maslahi yao na masuala mbali mbali ya Kitaifa,Kikanda na Kimataifa chini ya Muungano wetu huu wa Serikali mbili”,alisema Dk.Mabodi.

Amesema kuna baadhi ya Watendaji wasiokuwa waaminifu wanaohudumu katika Sekta za Umma wamekuwa wakichafua hadhi ya Muungano kutokana na vitendo vyao vya Rushwa na Urasimu usiokuwa na sababu za msingi katika utoaji wa Huduma.

Aliziutaja sababu za kuwepo kwa Muungano huo kuwa ni Ulinzi na Usalama wa Nchi zote mbili pamoja na kutoa Uhuru kwa Wananchi wa pande zote mbili kuishi sehemu yoyote ya Muungano bila kusumbuliwa.

Ameeleza kuwa kwamba msimamo wa Serikali zote mbili ni kulinda kwa gharama yoyote Tunu hiyo ya Muungano dhidi ya maadui wanaopambana uvunjwe ili wao wapate njia ya kupenya katikati na kurudisha utawala Kikoloni na Kisultani.

Akizungumzia Utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa Zanzibar Dk.Mabodi amesema ahadi walizoahidiwa Wananchi kupitia Uchaguzi Mkuu uliopita zimetatuliwa kwa zaidi ya asilimia 97 za kabla ya 2020 zitakuwa zimetatuliwa kwa kiwango kikubwa.

Amesema Serikali ya awamu ya Saba chini ya Uongozi wa Rais wa Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein zimeimarishwa kwa kiwango kikubwa Sekta za Afya, Elimu,Maji Safi na Salama, Uvuvu,Kilimo pamoja na Miundombinu ya Babaraba Anga na Nchi Kavu.

Alieleza kwamba katika awamu hiyo Dk.Shein ameasisi Sera ya Elimu bure na Afya bure kwa lengo la kuwapunguzia mzigo Wananchi wa Visiwa vya Zanzibar katika kulipia matibabu na Elimu ili Sekta hizo zipate kuimarika.

Aidha  katika maelezo yake Dk.Mabodi amemtaja  Dk.Shein kuwa ni Shujaa wa maendeleo kwani kwani ameandika Historia mpya katika Nchi za Afrika Mashariki ya kuwalipa Pencheni ya Shilingi 20,000 kila mwezi Wazee wote  wenye umri wa kuanzia miaka 70 bila ya kujali tofauti zao za Kisiasa.

Pamoja na hayo amewaomba Wananchi kupima na kutathimini shughuli zinazofanywa na Vyama vya Siasa vinavyopewa Ruzuku na Serikali vinashughulikia kwa kiasi gani Changamoto za Wananchi na hatimaye wafanye maamuzi sahihi ya kutoa ridhaa kwa CCM ili iendelede kuongoza Dola kupitia Uchaguzi wa mwaka 2020.

Ijumaa, 26 Aprili 2019

RC AYOUB- ATAKA MUUNGANO ULINDWE NA KUTHAMINIWA.



 MKUU wa Mkoa wa Mjini na Magharib Mhe.Ayoub Mohamed Mahmoud akiwahutubia Vijana wa UVCCM Idara ya Vyuo na Vyuo Vikuu katika Bonanza la kuadhimisha miaka 55 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar lililofanyika Maisara Zanzibar.

 NAIBU Katibu Mkuu wa UVCCM Zanzibar Ndugu Mussa Haji Mussa akitoa maelezo juu ya Bonanza hilo.

 MATEMBEZI ya UVCCM kupitia Idara ya Vyuo na Vyuo Vikuu wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharib Mhe.Ayoub Mohamed.

 WASHIRIKI wa matembezi hayo ambao ni Vijana wa UVCCM kupitia Idara ya Vyuo na Vyuo Vikuu wakifanya mazoezi ya kunyoosha viungo mara baada ya Matembezi katika Viwanja vya Maisara.

 WASHIRIKI wa matembezi hayo ambao ni Vijana wa UVCCM kupitia Idara ya Vyuo na Vyuo Vikuu wakicheza Mpira wa Nage.







VIJANA nchini wametakiwa kujitathimini na kujipima kifikra juu ya mwenendo wao wa uzalendo kama unaenda sambamba na dhamira ya Waasisi wa Muungano wa Serikali mbili ya Zanzibar na Tanganyika.

Rai hiyo imetolewa leo na Mkuu wa Mkoa wa Mjini na Magharib Mhe.Ayoub Mohamed Mahmoud wakati akiwahutubia Vijana zaidi ya 700 katika Bonanza la UVCCM kupitia Idara ya Vyuo na Vyuo Vikuu katika maadhimisho ya Kilele cha miaka 55 ya Muungano wa Tanzania, huko katika Viwanja vya Maisara Mjini Zanzibar.

Amesema ni muda wa Vijana wa sasa kujipanga vizuri kwa kuendeleza mema yaliyoasisi na Waasisiwa wa Muungano huo ambao ndio chimbuko la maendeleo endelevu ya Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.

Ameongeza kuwa lengo la Muungano huo ni kuhakikisha Ulinzi na Usalama wa Nchi zote mbili unaimarika sambamba na kukua kwa Uchumi.

Ameeleza kwamba dhamira ya Wazee walioasisi Muungano huo waliamini kwamba maendeleo ya Nchi yoyote Duniani yanapatikana baada ya kuwepo kwa Amani na Utulivu ya kudumu.

Katika maelezo yake Mhe.Ayoub,amesema ni wajibu wa kila kijana kulinda Muungano huo, uliobeba mafanikio na matumaini ya Mamilioni ya Watanzania.

Amesema wapo baadhi ya Watu wanaopotosha juu ya Muungano kwa kudai hauna maslahi hali ya kuwa wao wananufaika na fursa mbali mbali zinazopatika katika Muungano huo.  

"Vijana nakuombeni tuendelee kuwa Wamoja katika kulinda Muungano huu ili Nchi zetu ziendelee kustawi Kiuchumi,Kisiasa na Kijamii", amesema RC Ayoub.

Akizungumza Naibu Katibu Mkuu wa UVCCM Zanzibar Ndugu Mussa Haji Mussa amesema lengo la Matembezi hayo ni kuunga mkono juhudi za Waasisi waliobuni jambo la kimaendeleo la kuanzisha Muungano, kama Chombo rasmi cha kulinda maslahi ya Wananchi wa Zanzibar na Tanzania Bara.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini 'B' Mhe.Rajab Ali Rajab, amewataka Vijana Wasomi kuwa Mabalozi wazuri wa kuelimisha Jamii juu ya faida zilizopatikana katika kipindi cha miaka 55 ya Muungano huo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Idara ya Vyuo na Vyuo Vikuu ya UVCCM Zanzibar Ndugu Masoud Shibli Makame amesema katika Sekta ya Elimu Vijana wa Zanzibar wananufaika na fursa ya Mikopo miwili ya Elimu ya Juu hatua inayochochea upatikanaji wa Wasomi wengi Nchini. 

Bonanza hilo limetanguliwa na Matembezi ya Vijana zaidi ya 700 kutoka Taasisi za Elimu ya Juu pamoja na UVCCM wa Mikoa mbali mbali ya Zanzibar sambamba kuchezwa Michezo mbali mbali ikiwemo Mpira wa Nage,Mpira wa Miguu na kuvuta kamba.

DK.MABODI ATANGAZA NEEMA KIJIJI CHA KIKOBWENI, MHE.NADIR AELEZA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM 2016-2017.


 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi akizungumza katika Mkutano wa Jimbo wa Jimbo la Chaani wa  kuelezea Utekelezaji wa Ilani ya CCM.
 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi(kulia) akimsikiliza Mkaazi wa Kijiji cha Kikobweni Ndugu Hassan Nganja(kushoto) aliyetoa maoni yake juu ya kuwepo na upungufu wa huduma za Maji Safi katika Kijiji hicho.

 MWAKILISHI wa Jimbo la Chaani Unguja Mhe.Nadir Abdul-Tif Yussuf akizungumza na Wananchi katika Mkutano wa Jimbo hilo katika uwanja wa Mpira wa Kijiji cha Kikobweni Wilaya ya Kaskazini 'A' Unguja.

 BAADHI ya Wananchi wa Jimbo la Chaani wakisikiliza kwa makini taarifa mbali mbali za Utekelezaji wa Ilani katika Jimbo hilo.


NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar Dk.Abudlla Juma Saadalla Mabodi amesema CCM itachimba Kisima cha Maji Safi na Salama kwa muda wa wiki mbili ili kuondosha changamoto ya ukosefu wa nishaji hiyo kwa Wananchi wa Kijiji cha Kikobweni Jimbo la Chaani Wilaya ya Kaskazini  'A' Unguja.

Ahadi hiyo ameitoa katika Mkutano wa Jimbo la Chaani wa kueleza utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa Chama na Serikali,ambapo baadhi ya Wananchi wa kijiji hicho wamedai kuwa na upungufu wa huduma za maji ambapo kwa sasa wanatumia maji kisima cha zamani ambacho hakikidhi mahitaji ya huduma hiyo kwa wananchi hao.

Dk.Mabodi amesema kwa hatua ya awali anatoa kiasi cha shilingi milioni 1.5 kwa ajili ya maandalizi ya uchimbaji wa kisima hicho ili wananchi wa kijiji hicho na vijiji jirani wapate huduma hiyo kwa wakati hasa katika mwezi Mtukufu wa Ramadhani unaotarajiwa kuanzi hivi karibuni.

Amesema  wananchi wana haki ya kueleza changamoto zinazowakabili kwa viongozi wao waliowapa ridhaa ya kuwaongoza katika ngazi mbali mbali za kiuongozi katika Chama na Serikali.

Amesema  CCM ni Taasisi ya Kisiasa inayoahidi na ikatekeleza kwa vitendo na kwa wakati mwafaka na haitoi ahadi za kuwalaghai Wananchi kama vinavyofanya baadhi ya vyama vya upinzani kuwa wataijenga Zanzibar kwa Siku 100 iwe kama Nchi ya Singapore.

Amesema  Maendeleo hayana itikadi wala misimamo ya kisiasa kwani inapotekelezwa Ilani ya CCM kwa kuwafikishia wananchi huduma za maji,Umeme,Bababara na Vituo vya Afya fursa hizo hazitumiwi na Wanachama wa CCM pekee yao bali wananufaika wananchi wote.

Ameeleza  kwamba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa sasa inatekeleza Ilani ya CCM kwa kujenga Barabara yenye kiwango cha Lami katika Mkoa wa Kaskazini Unguja ili kurahisisha huduma za Usafiri kwa Wananchi wa Mkoa huo.

Katika maelezo yake Dk.Mabodi amewambia Wananchi wa Jimbo la Chaani kwamba Serikali ipo katika hatua za kutekeleza Mradi mkubwa wa Maji Safi na Salama ambapo ukikamilika utamaliza changamoto ya upungufu wa huduma za maji Mkoani humo.

Kupitia Mkutano huo Dk.Mabodi ameeleza kuridhishwa kwake na Utekelezaji  wa Ilani ya CCM katika Jimbo hilo, licha ya kuwepo kwa changamoto ndogo ndogo zinazotafutiwa ufumbuzi wa kudumu na viongozi wa jimbo hilo.

Amewataka Mbunge na Mwakilishi wa Jimbo hilo watatue changamoto zilizopo katika maeneo mbali mbali ya jimbo hilo ili Chama kishinde bila vikwazo katika  Uchaguzi Mkuu ujao.

Amesema  CCM inapozungumzia ushindi wake wa Kihistoria katika Uchaguzi Mkuu ujao wa mwaka 2020, ni kutokana na utekelezaji mzuri wa ahadi zilizotolewa kupitia Uchaguzi Mkuu uliopita.

Pamoja na hayo amewasihi wananchi wa Jimbo hilo kuthamini miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwani kuna baadhi yao wamekuwa wakihujumu miradi hiyo kwa makusudi hali inayokwamisha baadhi ya fursa za kimaendeleo.

" Nimeshuhudia katika Mkoa huu inahujumiwa miondombinu ya Maji Safi na Salama kwa kuiba vifaa vya umeme,kuharibiwa kwa Gari ya wagonjwa na matukio mengine ya kukatisha tamaa na yote hayo yanatekelezwa na watu wachache wapinga maendeleo.",ameeleza Dk.Mabodi.

Amewaonya  baadhi ya Watendaji na Viongozi wa Ngazi za Majimbo katika Wilaya ya Kaskazini 'A' Unguja, wanaojihusisha na mipango ya kuwaandaa  Wagombea wa ngazi mbali mbali za Uongozi kabla ya muda wa kufanya hivyo kufika kwani kufanya hivyo ni kukiuka Katiba ya CCM ya mwaka 1977 na miongozo yake.

Pamoja na hayo amesema  CCM itaendelea kulinda Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwa gharama yeyote na atakayejaribu kubeza atakuwa ni msaliti na adui wa Taifa.

Akitoa Taarifa ya Utekelezaji wa Ilani ya CCM Mwakilishi wa Jimbo hilo Mhe.Nadir Abdul-Tif Yussuf amesema kwa kipindi cha mwaka 2016-2017 alitekeleza masuala mbali mbali yakiwemo kuvipatia fedha za mitaji vikundi vya ujasiriamali,alinunua Gari maalum la Wagonjwa,kuweka Taa za umeme za kuwasha usiku Viwanja Vitatu,kujenga visima vya Maji Safi na Salama pamoja na kununua mashine za Kilimo za Power Tiller kwa ajili ya shughuli za Kilimo.

Miradi mingine iliyotekelezwa ni pamoja na matengenezo ya Ofisi mbali mbali za CCM,ununuzi wa Dawa za Binadamu katika Vituo vya Afya mbali mbali mbali pamoja na ununuzi wa Vyarahani 10 kwa ajili ya vikundi vya Jimbo.

Mhe.Nadir  ametoa  tahadhari kwa baadhi ya Watu wanaotengeneza makundi ya kuwagawa na kuwafitinisha viongozi wa Jimbo hilo uku wakipanga wagombea kinyume na utaratibu na kuongeza kwamba watu hao hawakitakii mema Chama Cha Mapinduzi.

Wakizungumza kwa wakati tofauti Wananchi wa Jimbo hilo mara baada ya Mkutano huo,wameeleza kwamba wamenufaika sana na miradi inayotekelezwa na fedha za Mfuko wa Jimbo wa Mwakilishi.

Jumatano, 24 Aprili 2019

CCM MKOA WA MAGHARIB YAENDELEA NA ZIARA YAKE JIMBO LA KIEMBE SAMAKI UNGUJA.

 DIWANI wa Wadi ya Mbweni Unguja Ndugu Maabadi Ali Maulid akitoa maelezo juu ya usambazaji wa mipira ya maji Safi na Salama katika maeneo mbali mbali ya Wadi hiyo.

 KAMATI ya Siasa ya CCM Mkoa wa Magharib wakikagua Mradi wa Maji Safi na Salama uliotekelezwa chini Mfuko wa Jimbo la Kiembe Samaki katika ziara yao ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM.

  Afisa Mipango Manispaa ya Magharib 'B' Ndugu Saumu Daniel Yussuf(hayupo pichani) akitoa ufafanuzi wa miradi iliyotekelezwa na Manispaa hiyo katika Kituo cha Afya cha Kiembe Samaki chini ya Mfumo wa Ugatuzi mbele ya Kamati ya Siasa ya CCM ya Mkoa wa Magharib.


KAMATI ya Siasa ya CCM Mkoa wa Magharib wakikagua Vyarahani vilivyotolewa na Mwakilishi wa Jimbo hilo Mahmoud Thabit Kombo kwa Kikundi cha Ujasiriamali cha UWT cha Jimbo hilo huko tawi la CCM Mbweni Matrekta Unguja.


CHAMA Cha Mapinduzi(CCM) Mkoa wa Magharibi Unguja kimewataka Viongozi wa Jimbo la Kiembe Samaki kuongeza kasi ya utekelezaji wa Ilani ya CCM ili kutatua kwa wakati mwafaka changamoto zinazowakabili Wananchi.

Rai hiyo imetolewa leo na Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa huo Ndugu Mohamed Rajab Soud katika mwendelezo wa ziara ya Kamati ya Siasa ya Mkoa ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM katika Jimbo la Kiembe Samaki.

Amesema pamoja na kutekelezwa kwa miradi mbali mbali ya maendeleo kupitia fedha za mifuko ya maendeleo ya Jimbo hilo bado kupanahitajika juhudi za ziara za kutatua kero za wananchi katika sekta za Afya,Maji Safi na Salama pamoja na miondombinu ya barabara za ndani.

Amesema lengo la ziara hiyo ni kukagua miradi inayotekelezwa na viongozi hao kama thamani ya fedha zinazotumika zinaendana na miradi inayotekelezwa. 

Amewambia viongozi hao kuwa wahakikishe miradi wanayoitekeleza inasaidie jamii husika badala ya watu wachache.

Aidha amewasihi Wananchi wa Jimbo hilo kuithamini na kuitunza miradi mbali inayotekelezwa kupitia Ilani ya CCM ili iwanufaishe vizazi vya sasa na vijavyo.

"Utekelezaji wa Ilani ya CCM ndani ya Jimbo la Kiembe Samaki unafanuyika lakini bado sijaridhika kwa baadhi ya maeneo hivyo wahusika wanatakiwa kuongeza kasi kubwa katika kutatua kero za wananchi.",amesema Mwenyekiti huyo Mohamed.

Naye Diwani wa Wadi ya Mbweni Ndugu Maabadi Ali Maulid amesema katika kutatua kero za wananchi wamejipanga kutekeleza miradi mitatu ikiwemo kujenga minara mitatu mirefu katika visima vya maji safi na salama,kumalizia kuezeka bweni Wanafunzi wa Skuli ya Sekondari ya Kiembesamaki pamoja na  matengenezo ya Barabara za ndani kwa kushirikiana na Serikali Kuu.

Naye Afisa Mipango Manispaa ya Magharib 'B' Ndugu Saumu Daniel Yussuf akizungumza katika Kituo cha Afya cha Kiembe Samaki amesema wanaendelea kuimarisha huduma za Afya katika Vituo mbali mbali licha ya kukabiliwa na changamoto za uchakavu wa majengo waliokabidhiwa katika mfumo wa ugatuzi.











Jumatatu, 22 Aprili 2019

DK.MABODI-ASEMA CCM IMEJIZATITI KUTATUA CHANGAMOTO ZA WANANCHI NA KUSIMAMIA DEMOKRASIA.

 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi akiwahutubia Wanachama wa CCM na Wananchi  katika ziara yake ya kukagua Utekelezaji wa Ilani katika Maskani ya CCM ya Kisonge, iliyopo Shehia ya Mzuri Jimbo la Makunduchi Wilaya ya Kusini Unguja.



NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk.Abdulla Juma Saadalla ‘Mabodi’ amesema Chama hicho kimejizatiti kutatua changamoto za Wananchi pamoja na kusimamia Demokrasia kwa kukemea vitendo viovu vinavyohatarisha Amani na Utulivu wa Nchi.

Kauli hiyo ameitoa katika ziara yake ya kukagua Uhai wa Chama na Utekelezaji wa Ilani ya CCM katika Jimbo la Makunduchi Wilaya ya Kusini Unguja, amesema vipaumbele vya CCM ni kutekeleza kwa kasi ahadi zilizotolewa na Taasisi hiyo kwa wananchi kupitia Uchaguzi Mkuu uliopita.

Amesema Chama Cha Mapinduzi kinaendelea kuaminiwa,kupendwa na kuthaminiwa na Mamilioni ya Watanzania kutokana na usimamizi mzuri wa utekelezaji wa Sera zake, kwa kutatua changamoto za kijamii kwa wakati mwafaka.

Aidha amesema katika kusimamia dhana ya Demokrasia CCM haitosita kukemea vitendo viovu vinavyoashiria kuvunja Sheria za Nchi, hasa vinavyotekelezwa na baadhi ya Vyama vya upinzani.

“Tumekubali kuingia katika mfumo wa Vyama vingi ili tushindane kwa Sera na sio kushindana kwa vituko na vurugu ni muhimu kila mwanasiasa kujitathimini juu ya mwenendo wake kwa jamii anayoiongoza.”, ameeleza Dk.Mabodi.

Amesema katika zama za CCM mpya imekuwa imekuwa ni kimbilio la wananchi wanaoamini katika siasa za maendeleo ambao wametelekezwa na Vyama vyao na kupokelewa  vizuri ndani ya CCM ili wanufaike na Demokrasia iliyotukuka.

Amewataka Viongozi na Watendaji wa CCM kutowawekea vikwazo Wananchi wanaotaka  kujiunga na Chama na badala yake wapewe fursa hiyo bila masharti magumu sambamba na kuwasomesha miongozo na itikadi za kitaasisi.

Amewaagiza Wabunge,Wawakilishi na Madiwani kufanya mikutano katika maeneo yao ya kuwaeleza Wananchi mafanikio yaliyofikiwa katika utekelezaji wa Ilani ili wananchi hao wawe Mabalozi wa kufikisha taarifa hizo kwa jamii.

Amewambia wananchi kuwa CCM imesimamia kwa ufanisi miradi ya maendeleo ukiwemo wa TASAF ambao upo katika Ilani ya CCM ya mwaka 2015/2020, ambao umewaondosha wananchi katika wimbi la umasikini na kuwa na kipato cha kati.  

Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa mbali mbali vikiwemo Runinga (Television) pamoja na Fedha kwa vikundi 11 vya Saccos ya Shehia ya Mzuri katika Maskani ya CCM ya Kisonge Makunduchi Dk.Mabodi amesisitiza kuwa uhai wa Taasisi hiyo ya kisiasa unaanza kuimarishwa kuanzia ngazi ya mashina.

Naye Mwakilishi wa Jimbo la Makunduchi Mhe.Haroun Ali Suleiman amesema tayari Ilani ya CCM ndani ya Jimbo hilo imetekelezwa kwa asilimia 90, na kwa sasa wanaendelea kutatua baadhi ya changamoto ili kuzimaliza kabla ya 2020.

Mhe.Haroun amesema kwa kushirikiana na Kamati ya Siasa ya Jimbo hilo wamefanya ziara katika Shehia 13 za Jimbo kwa kuratibu changamoto zinazowakabili wananchi na nyingi zimetatuliwa sambamba na kueleza fursa na miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na Serikali.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo hilo Mhe. Ameir Haji Timbe ameeleza kuwa maendeleo yaliyopatikana katika Jimbo hilo yametokana na ushirikiano mkubwa uliopo baina ya viongozi na wananchi.

Akizungumza Mwenyekiti wa Maskani ya CCM ya Kisonge iliyopo Makunduchi Abdallah Hassan Haji amesema wanaendelea kuvuna wanachama wapya kutoka vyama vya upinzani huku wakijipanga kufuta masalia ya upinzania ndani ya Jimbo hilo.

Naye Mwenyekiti wa Maskani ya CCM ya Hapa Kazi Tu Yussuf Abeid Haji, akizungumza katika uzinduzi wa Maskani hiyo amefafanua kuwa eneo la maskani yao litatumika kuwa chachu ya kujenga umoja,mshikamano pamoja na kuwa kituo mbadala cha kubuni miradi mbali mbali ya maendeleo kwa maslahi ya Wana CCM.

MATUKIO KATIKA PICHA ZIARA YA NAIBU KATIBU MKUU WA CCM ZNZ DK.ABDULLA JUMA MABODI KATIKA JIMBO LA MAKUNDUCHI UNGUJA.

 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi akizungumza na Wananchi wa Kijiji cha Kibuteni alipoenda kwa ajili ya kukagua Utekelezaji wa Ilani ya CCM katika Jimbo la Makunduchi Wilaya ya Kusini Unguja.

 MWENYEKITI wa CCM Wilaya ya Kusini Unguja Abdulaziz Haji akizungumza katika ziara hiyo ya Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar  Dk.Abdulla Juma Mabodi katika Jimbo la Makunduchi.

 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi akikabidhiwa zawadi ya Madafu na Wananchi wa Kijiji cha Kibuteni Makunduchi. 

 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi  amebeba mtoto mara baada ya kuzungumza na Wananchi wa Kijiji cha Kibuteni alipoenda kukagua Uwanja wa Mpira wa miguu wa  kisasa unaojengwa katika Kijiji hicho.

 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi akiwa akiimba na kucheza jimbo mbali mbali za CCM pamoja na Vijana wa UVCCM wa kikundi maalum cha Hamasa katika ziara yake ya kukagua Utekelezaji wa Ilani ya CCM Jimbo la Makunduchi.
  
 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi akikagua ukarabati wa ujenzi katika Ofisi ya CCM Jimbo la Makunduchi.  

 

 WAJUMBE wa Kamati ya Siasa ya Jimbo la Makunduchi wakizungumzia mafanikio mbali mbali yaliyofikiwa katika masuala mbali mbali ya utekelezaji wa Ilani ya CCM Jimboni humo.

 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi akimkabidhi fedha kiongozi wa Kikundi cha Saccos ya Shehia ya Mzuri iliyopo Makunduchi Wilaya ya Kusini Unguja.
  
 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi akikabidhi Runinga(Television) kwa Uongozi wa Maskani ya CCM ya Kisonge iliyopo katika Jimbo la Makunduchi.  
 MWAKILISHI wa Jimbo la Makunduchi Mhe.Haroun Ali Suleiman akielezea Utekelezaji wa Ilani ya CCM ndani ya Jimbo hilo.


 MBUNGE wa Jimbo la Makunduchi Mhe. Ameir Haji Timbe akizungumza na Wananchi wa Jiimbo la Makunduchi katika ziara ya Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Mabodi.
 
 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi akiwa amebeba ndoo yenye udongo katika ujenzi wa Tawi la CCM Miwaleni Jimbo la Makunduchi Wilaya ya Kusini Unguja.

 MWAKILISHI wa Jimbo la Makunduchi Mhe.Haroun Ali Suleiman akisomba udongo wa kifusi wa kuweka katika Tawi la CCM la Miwaleni katika ziara ya kukukagua uhai wa Chama na Utekelezaji wa Ilani ya CCM katika Jimbo hilo Wilaya ya Kusini Unguja.

 MKUU wa Wilaya ya Kusini Unguja Idrisa Mustafa Kitwana (aliyebeba kifaa cha kubebea udongo wa kifusi wa pili kushoto) akishiriki ujenzi wa Taifa katika Tawi la CCM Miwaleni Makunduchi.  
 
 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi akizindua Maskani ya CCM ya Hapa Kazi Tu iliyopo Mtende Mndo Makunduchi.
 
 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi akikagua ujenzi wa Tawi la CCM Mtende Mndo Makunduchi Wilaya ya Kusini Unguja.  

 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi akikabidhi Runinga kwa Uongozi wa Maskani ya CCM ya Mtende Mndo Makunduchi.
 

Jumamosi, 20 Aprili 2019

MATUKIO KATIKA PICHA HAFLA YA JUMUIYA YA MAENDELEO YA VIJANA YA CCM KUTOA VIFAA VYA UJENZI NA SARE ZA WANAFUNZI SKULI YA KIDAGONI KASKAZINI 'A'


 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi akipokelewa na Wanafunzi wa Shule ya maandalizi,msingi na Kati ya Kidagoni Wilaya ya Kaskazini 'A' Unguja. 

 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi akipewa maelezo na Sheha wa Shehia ya Kidoti Makame Suweid Haji  juu ya ujenzi wa Kituo cha Afya kinachojengwa kwa nguvu za wananchi katika kijiji cha Kidagoni.

NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi akikagua Kituo hicho. 

 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi akizungumza na Uongozi wa Kamati ya Maendeleo ya Skuli ya Kidagoni. 

VIJANA mbali mbali wa UVCCM wakishusha mabembea mbali mbali yaliyotelewa na Jumuiya ya Vijana wapenda maendeleo kwa ajili ya wanafunzi wa maandalizi wa Skuli hiyo.


 WAJUMBE mbali mbali wa Jumuiya ya Vijana wapenda maendeleo wakiimba wimbo wa mashujaa  mara baada ya kuwasili skulini hapo.

 WANAFUNZI wa Skuli ya Kidagoni wakisoma utenzi 

 VIJANA wa kundi Maalum la Hamasa kutoka CCM Afisi Kuu wakiwa katika hafla hiyo.

 Mwalimu wa Skuli ya Kidagoni Neema Othman Khamis akisoma risala ya Skuli hiyo.

 VIJANA wa kikundi cha sarakasi cha UVCCM Wilaya ya Kaskazini 'A' wakionyesha uwezo wao katika hafla hiyo.


VIJANA wa kundi Maalum la Hamasa kutoka CCM Afisi Kuu wakiwa katika hafla hiyo.
 MJUMBE wa Jumuiya ya Vijana wapenda Maendeleo akisoma risala ya Jumuiya hiyo.

 MWENYEKITI wa  Jumuiya ya Vijana wapenda Maendeleo Mwinyi Ahmed Mwinyi akizungumzia lengo la kutoa vifaa vya ujenzi pamoja na sale,viatu,mikoba na mabembea kwa wanafunzi wa Jumuiya hiyo.

 MWENYEKITI wa CCM Wilaya ya Kaskazini 'A' akitoa salamu za CCM katika Wilaya hiyo.

 KATIBU wa CCM Mkoa wa Kaskazini Unguja Mulla Othman Zubeir akitoa salamu za CCM kwa niaba ya Mkoa.

 MWAKILISHI  wa Jimbo  la Nungwi Mhe. Ame Haji Ali akizungumzia utekelezaji wa Ilani katika Jimbo hilo mbele ya mgeni rasmi katika hafla hiyo.

  MWENYEKITI wa  Jumuiya ya Vijana wapenda Maendeleo Mwinyi Ahmed Mwinyi akikabidhi Sale za wanafunzi ambavyo ni moja vitu mbali mbali vilivyotolewa na Jumuiya yake kwa Skuli ya Kidagoni.

 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi akiwahutubia wananchi wa Kidagoni katika hafla hiyo.



 PICHA ya pamoja ya viongozi wa Jumuiya, Viongozi wa Skuli ya Kidagoni pamoja na mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Mabodi.
 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi akiwa na Ujumbe wa Viongozi mbali mbali wa CCM na Jumuiya zake kutoka Kibiti na Rufiji.(PICHA NA IS-HAKA OMAR-AFISI KUU YA CCM ZNZ).