Jumamosi, 16 Mei 2015

Chama cha mapinduzi (CCM) Zanzibar kimesema kwamba kitapambana kisiasa

CHAMA cha mapinduzi (CCM) Zanzibar kimesema kwamba kitapambana kisiasa kuhakikisha kinadhibiti mbinu, njama na mipango ya wapinzani kuvuruga uchaguzi mkuu ujao haifanikiwi.

 Hayo yameelezwa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai, alipokuwa akiwahutubia wana CCM na wananchi wa Mkoa wa Mjini Magharibi, katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Kwa Mabata, Magogoni Unguja. 

Vuai amesema viongozi wa vyama vya upinzani wamekuwa mstari wa mbele katika kupanga njama chafu na kuanzisha vurugu kila kukikaribia uchaguzi mkuu ili waonekane mbele ya taasisi za kimataifa kuwa wanaonewa na CCM, jambo ambalo watafeli katika uchaguzi wa mwaka huu, kwani serikali imejipanga ipasavyo kudhibiti hali hiyo. 

Alifafanua kwamba licha ya Viongozi na wafuasi wa kambi ya upinzani kutoa vitisho na propaganda za upotoshaji dhidi ya CCM na Serikali zake, chama hicho hakitoyumbishwa na mwenendo huo, bali kitajipanga vizuri na kuhakikisha kinashinda kwa kishindo chini ya demokrasia ya vyama vingi nchini. “

Tunaviambia vyama siasa nchini CCM itaendeleza wimbi la ushindi na kukamata hatamu ya dola Tanzania Bara na Zanzibar kufuatia ushindi mkubwa na wa kihistoria na tunawambia kuwa wapinzani hawawezi tena bora wajitoe mapema, vyenginevyo wataaibika mbele ya watu wao wanaowadanganya na kuwapotosha." Alidai Vuai. 

 Naibu Katibu Mkuu huyo wa CCM Zanzibar alisisitiza haja kwa Wazanzibari kufahamu kwamba Zanzibar inahitaji kiongozi (Rais) mwadilifu na mwenye busara za hali ya juu ya kuwaongoza wananchi kwa misingi ya amani na utulivu na kamwe siyo kiongozi mwenye uchu wa madaraka na kutawaliwa na ndoto za kuingia Ikulu kwa ajili ya kulipiza visasi.

 Alizungumzia kuhusu serikali ya awamu ya saba inayoongozwa na CCM imepiga hatua kubwa za kimaendeleo ikiwemo upatikanaji wa huduma bora za kijamii pamoja na kupanuka kwa miuondombinu mijini na vijijini, Unguja na Pemba. 

Alisema katika bajeti ya mapato na matumizi ya serikali kwa mwaka 2015/2016, imetoa kipaumbe kwa huduma za msingi za kijamii ikiwemo afya, elimu na sekta zingine zinazogusa maisha ya wananchi wa hasa wa kipato cha chini. 

 Alisema katika bajeti hiyo, kwa mara ya kwanza wazee wote waliostaafu serikali na wale ambao hawakufanya kazi za utumishi serikali kuanzia umri wa miaka 70 wataanza kulipwa pensheni ya shilingi 20 kwa kila mwezi kwa lengo la kuwapunguzia ukali wa maisha. 

 Aidha alifafanua kwamba kuanzia mwaka 2011 serikali ya mapinduzi ya Zanzibar imekuwa ikitoa mikopo ya fedha kwa wanafunzi wa elimu ya juu zaidi ya shilingi bilioni 26, kwa lengo la kuzalisha wataalamu wa fani mbali mbali wenye uwezo na weledi wa kufanya kazi katika sekta mbali mbali nchini.

 Kuhusu serikali ya umoja wa kitaifa Zanzibar (SUK) Vuai aliwambia viongozi na wafuasi wa vyama vya upinzani hasa CUF kwamba wao ndio wanaoanzisha choko choko za kuvuruga dhamira na malengo ya kuanzishwa kwa serikali hiyo. “CCM tulitaka kuanzisha SUK mapema kutokana na CUF kukataa katika vikao vilivyofanyika Butiama mwaka 2008, baada ya mazungumzo baina ya CCM na Chama hicho yaliyochukua miezi 14 bila ya mafanikio. Lakini wenzetu baadae wakarudi wenyewe kutaka tuanzishe serikali yenye mfumo huo (SUK) lakini kwa vile sisi CCM ni waungwana tukakubali lakini tulijuwa kuwa wenzetu wana nia na malengo ya kuingia Ikulu na siyo kujenga umoja na mshikamano wa Wazanzibari.” 

Alisisitiza Naibu Vuai. Naye Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM ya Taifa, Pandu Ameir Kificho, aliwasihi wananchi wa Wazanzibari kuweka kando ushabiki wa kisiasa na kufanya maamuzi yanayofaa kwa kuunga mkono katiba inayopendekezwa, ili kuipitisha kuwa katiba kamili kwani imebeba mambo ya msingi kwa maslahi ya jamii ya pande zote mbili za muungano. 

Alisema kuwa baadhi ya viongozi wa kisiasa Zanzibar wamekuwa na utamaduni usiofaa wa kuwahamasisha wananchi kushiriki katika vitendo vya uvunjaji wa Amani na utulivu nchini. “Lazima wananchi tujiepushe na utumwa wa kupandikizwa mbegu za chuki na kutugawa hasa katika kipindi hichi cha maandalizi ya kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka huu, kwani watu wote duniani wameelekeza masikio ya Zanzibar, kufahamu nini tutafanya.”Alishauri Kificho.

Naye Mwenyekiti wa Mkoa Magharibi Kichama, Yussuf Mohamed Yussuf aliwataka wafuasi wa chama hicho na wananchi kwa ujumla kuendelea kujipanga kisaikolojia kwa kupima uwezo na sera za kila chama kiutendaji na hatimaye watajua wapi waunge mkono katika uchaguzi mkuu huo.

Yussuf alisema kuwa CCM ipo imara na ina uwezo wa kupambana na vikwazo vyote vilivyowekwa na CUF vikiwemo kupandikiza mbegu za chuki kwa wananchi kwa kubeza na kudharau kila jambo jema linalofanywa na serikali ya CCM, suala ambalo wananchi waliokuwa wengi wameshutuka na kuona wananyang’anywa ambao kwa sasa wanarudi katika chama cha mapinduzi chenye sera makini na zinazotekelezeka.

Katika hali isiyotarajiwa wakati mgeni rasmi kwenye mkutano huo akijiandaa kushuka kwenye jukwaa ghafla watu wanaosadikiwa kuwa wafuasi wa chama cha CUF walianza kurusha mawe katika ya mkutano huo, lakini hali hiyo ilidhibitiwa mapema na askari wa jeshi la polisi na haikuleta madhara kwa wananchi waliokuwa katika mkutano huo.

Jumapili, 10 Mei 2015

DKT. SHEIN AWAONGOZA WANA CCM MAZIKO YA MAKADA WA CHAMA HICHO




MAKAMU Mwenyekiti wa CCM, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein, leo (mei 10, 2015) amewaongoza mamia ya Wana CCM waliohudhuria maziko ya Makada wawili kati ya watu wa Chama Cha Mapinduzi waliofariki dunia kutokana na ajili ya gari.

Makada hao waliozikwa katika makaburi  ya Mwanakwerekwe ni pamoja na Mwanaidi  Zamir Haji (28), mkazi wa Magogoni na Mwanahawa Haji Machano (50), mkazi wa Mkele, Wilaya ya Mjini. 

Aidha, Mjumbe wa Kamati Kuu na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Balozi Seif Ali Iddi, aliwaongoza wananchi wa Jimbo la Mkwajuni waliohudhuria maziko ya kada mwengine wa CCM Munira Abdullah (16), aliyezikwa Kijijini kwao Mkwajuni, Wilaya ya Kaskazini “A”.

Wana CCM hao watatu walifikwa  na umati na wengine saba kujeruhiwa kufuatia gari (basi) walilokuwa wakisafiria kutoka Nungwi kuja Mjini kupasuka mpira wa mbele na kupinduka baada ya kugonga gari la ng’ombe, katika maeneo ya Mto wa Pwani, Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Makada waliolazwa katika Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja, ni pamoja na Maua Haji Khamis (54), Salhiya Sheha Khamis (26) na Sawadi Haji Khamis (38), wote wakazi wa Kwamtipura, Mjini Unguja. 

Chama Cha Mapinduzi kimepokea kwa mshituko, kuhuzuni na masikitiko makubwa taarifa za vifo vya makada wake hao, kwani walikuwa mstari wa mbele katika kikilinda, kikihifadhi, kukipigania na kukitetea kwa nguvu zao zote Chama hicho. Aidha, wanamuomba  Mwenyezi Mungu, Muumba Mbingu na  Ardhi, awape nafuu majeruhi wote waliolazwa hospitali, ili wapone haraka na kuungana na wananchi wengine  katika ujenzi wa taifa.

“Kwa niaba ya Viongozi na Wanachama wa CCM, na kwa niaba yangu binafsi, nachukua nafasi hii kuwapa mkono wa pole wana familia, ndugu na jamaa wote wa marehemu hao, kufuati  vifo hivyo”. Alisema Naibu Katibu Mkuu huyo wa CCM Zanzibar Ndugu Vuai Ali Vuai, alipokuwa akiwafariji moja ya wanafamilia ya maiti hao.

Chama Cha Mapinduzi kimesema kinatambua machungu waliyonayo wanafamilia, ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu hao, lakini kinawaomba kuwa na moyo wa subra na kinaungana nao, katika kipindi hiki kigumu cha maombolezi ya wapendwa wao hao.

CCM ina uhodari mkubwa wa kukabili...



Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesema kuwa kina uhodari mkubwa wa kukabili changamoto na kuheshimu mageuezi ya kifikra, kidemokrasia, kiuchumi  na kisiasa.

Tamko hilo limetamkwa na Mwakilishi wa Jimbo la Mwembemakumbi Machano Othman Said, wakati akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Tawi la Kinyasini, Wilaya ya Kaskazini ‘A’, Unguja.

Mwakilishi huyo, ambaye ni Waziri Asiyekuwa na Wizara Maalum wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) amesema historia ya CCM kabla ya mwaka 1977 imeonyesha jinsi chama hicho kilivyopita na kufuzu katika vipindi vingi vya mpito bila ya kuyumba, kubabaika wala kutetereka.

Amesema mwaka 1977 vyama vya ASP na TANU vilifanya mageuzi makubwa ya kisasa kwa kuunganisha nguvu za kisiasa, mwaka 1992 nchi ikatoka katika mfumo wa chama kimoja hadi vyama vingi na sera za CCM kiuchumi zikabadilika toka uchumi hodhi hadi soko huria.

Akizungumnzia  hali ya kisiasa Zanzibar na mivutano  yake mara baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 1995,2000 na 2005, amesema CCM iliona umuhimu wa kuwauliza wananchi ili kuridhia au kutoridhia  kuendelea na mfumo wa anayeshinda kuchukua vyote au kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK).
Kuhusu Katiba Inayopendekezwa, Mhe. Machano amesisitiza haja kwa wana CCM na wananchi wapenda amani na utulivu wa Wilaya hiyo (Kaskazini ‘A’) kutofanya makosa na badala yake waipigie kura ya ndio Katiba hiyo wakati utakapofika.

Ametoa wito kwa wana CCM kutobabaishwa na kauli za wapinzani  bali waelekeze nguvu zaidi katika kuisoma na kuifahamu vyema Katiba Pendekezwa, kabla ya kuchukua maamuzi sahihi kwa maslahi yao, vizazi vya leo na vya baadae.   

Alitumia kikao hicho kukabidhi Seti ya TV pamoja na king’amuzi kwa uongozi wa Maskani ya Chama Cha Mapinduzi ‘Bado Tungalipo’ ya Tawi hilo la Kinyasini Wilayani humo.

Akitoa neno la shukrani, Diwani wa Wadi ya Kinyasini Khamis Amour  Ame, amefarajika na msaada huo, ambao ulikuwa ukitakiwa sana na vijana hao wa Maskani  na kuahidi kuahidi kuitumia kama ilivyokusudiwa.

" Acheni makundi " Waride

Viongozi katika majimbo ya uchaguzi wametakiwa kujenga mshikamano na kuachana na makundi ambayo yamekuwa yakidhoofisha umoja wa wanachama katika utekelezaji wa ilani ya chama cha mapinduzi. Hayo yalisemwa na katibu wa kamati maalumu ya halmashauri kuu ya CCM Zanzibar ya itikadi na uenezi Waride Bakari Jabu wakati alipozungumza na viongozi wa jimbo la Bububu mjini hapa. Alisema mshikamano wa viongozi ikiwemo wawakilishi wabunge na madiwani unahitajika kwa kiwango kikubwa ili kufanikisha utekelezaji wa ilani ya CCM na kuondoa kero za wananchi katika majimbo. 'Chama cha mapinduzi kinakerwa na makundi ambayo yanadhoofisha maendeleo ya chama na kupiga hatua kubwa ya maendeleo'alisema. Katika mkutano huo mwakilishi wa jimbo hilo Hussein Ibrahim Makungu maarufu Bhaa na mwakilishi wa mbnge wa jimbo hilo Sururu walitangaza rasmin kuzika tofauti zao na hitilafu zilizokuwepo awali huku wakielekeza nguvu kuhakikisha chama cha mapinduzi kinaendelea kushikilia jimbo hilo.

Alhamisi, 7 Mei 2015

VUAI AKABIDHI MSAADA KWA WAATHIRIKA WA MAFURIKO ZANZIBAR.


                  
CHAMA Cha Mapinduzi Zanzibar leo kimemkabidhi Mwenyekiti wa Kamati ya Maafa Zanzibar Mhe. Mohamed Aboud Mohamed, msaada wa bidhaa za vyakula vya aina mbali mbali vyenye thamani ya Tssh. milioni ishirini na laki nne, kwa ajili ya wananchi walikumbwa na mafuriko katika maeneo mbali mbali ya Mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja.

Akikabidhi msaada huo, katika hafla fupi iliyofanyika Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Ndugu Vuai Ali Vuai, alisema Chama hicho kimelazimika kuungana na taasisi nyengine na watu binafsi walioguswa kutokana na janga hilo lililowapata wananchi wa maeneo kadhaa ya Wilaya za Mjini na Magharibi ya Mkoa huo.

Msaada uliotolewa ni pamoja na mchele polo (paketi) mia mbili (200), sukari, unga wa ngano, sabuni za kufulia (unga), mafuta ya kupikia yaina ya korie, pamoja na fedha taslim shilingi milioni tano (5,000,000/-).

Maeneo yaliyoathiriwa na mafuriko hayo mkoani humo ni pamoja na Mpendae kwa Binti Amrani na Mpendae ya Migombani, Mwanakwerekwe, Sebleni na Jang’ombe (Mjini), Kianga, Tomondo, Ziwamaboga na Mtopepo (Magharibi) ambapo nyumba kadhaa zilibomoka kufuatia kujaa maji na kuleta hasara kubwa.

“Chama Cha Mapinduzi ni chama kinachowajali na kuwakumbatia wananchi, ndio maana tulilazimika kusitisha kikao cha sekretarieti ya Kamati Maalum ya NEC Zanzibar,na kwenda kuwakagua na kuwafariji wananchi wote siku iliyotokea mafuriko hayo”. Alisema Naibu Katibu Mkuu huyo wa CCM Zanzibar na kuongeza kusema kuwa “CCM itafanya kila linalowekana kuhakikisha wananchi wanapatiwa kila aina ya misaada, ili waishi kama watu wengine”. Alidai Vuai.

Akitoa neon la shukrani, Mwenyekiti wa Kamati ya Maafa ya Taifa (Zanzibar), ambaye pia ni Waziri Nchi (OMPR) Mhe. Mohame Aboud Mohamed, ameelezea kufarajika kwake kutokana na msaada huo, ambapo alisema umekuja katika wakati muafaka.

Amesema masaada huo kwa kiasi kikubwa utatumika kama ulivyokusudiwa na kukidhi haja ya wananchi  102 waliopo katika kambini ya Mwanakwerekwe, Wilaya ya Magharibi na kuongeza kusema kwamba idadi hiyo huenda ikaongezeka katika siku zijazo.

Akizungumza na Watendaji wa Wizara ya Majenzi pamoja na Manispaa, baada ya kutembelea maeneo yaliyokumbwa na mafuriko hapo mei 5, mwaka huu, aliwataka kutekeleza  wajibu wao ikiwemo kusimamia na kuifanyia marekebisho mitaro ya maji taka, ili iweze kupitisha maji kwa urahisi. 

ufuatia hali hiyo, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein, amewaagiza Mwisho.


Jumatatu, 4 Mei 2015

Wajumbe wa Sekreatrieti ya Kamati Maalum ya NEC, Zanzibar wawafariji waloiathirika na mvua

WAJUMBE wa Sekreatrieti ya Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya (NEC) ya CCM, jana walitembelea maeneno yaliyofikwa na mafuriko ya Mkoa wa Mjini Magharibi kwa lengo la kuangalia na kuwafariji wananchi walioathirika na mkasa huo.

Wakiongozwa na Mwenyekiti wao, ambaye ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Vuai Ali Vuai, wajumbe hao wa Sekreatrieti walitembelea maeneo mbali mbali mkoani humo ikiwemo Mpendae kwa Binti Amrani, Tomondo na Mwanakwerekwe, ambayo yalikumbwa na kadhia hiyo.

Walitumia nafasi hiyo kuwafariji baadhi ya wananchi waliathirika na mafuriko hayo, ambapo baadhi nyumba zimejaa maji na nyengine kuanguka kuta zake, na kusabababisha hasara kubwa.

Wajumbe hao wamewataka wale wote waliokumbwa na janga hilo, kuwa na moyo wa subra na kuiachia Serikali kupitia kitengo cha maafa kutafakari na kuona nini la kufanya. Aidha, wametoa wito na haja kwa jamii nzima ya Wazanzibari kuchukua tahadhari hasa wakati huu wa mvua za masika zinazoendelea kunyesha.

Mvua hiyo kubwa iliyonyesha kwa muda wa masaa matatu mfululizo, kuanzia saa 3:30, iliwafanya wananchi wa Manispaa ya Zanzibar na vVitongoji vyake kushindwa kutekeleza shughuli zao za kimaendeleo.