Alhamisi, 7 Mei 2015

VUAI AKABIDHI MSAADA KWA WAATHIRIKA WA MAFURIKO ZANZIBAR.


                  
CHAMA Cha Mapinduzi Zanzibar leo kimemkabidhi Mwenyekiti wa Kamati ya Maafa Zanzibar Mhe. Mohamed Aboud Mohamed, msaada wa bidhaa za vyakula vya aina mbali mbali vyenye thamani ya Tssh. milioni ishirini na laki nne, kwa ajili ya wananchi walikumbwa na mafuriko katika maeneo mbali mbali ya Mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja.

Akikabidhi msaada huo, katika hafla fupi iliyofanyika Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Ndugu Vuai Ali Vuai, alisema Chama hicho kimelazimika kuungana na taasisi nyengine na watu binafsi walioguswa kutokana na janga hilo lililowapata wananchi wa maeneo kadhaa ya Wilaya za Mjini na Magharibi ya Mkoa huo.

Msaada uliotolewa ni pamoja na mchele polo (paketi) mia mbili (200), sukari, unga wa ngano, sabuni za kufulia (unga), mafuta ya kupikia yaina ya korie, pamoja na fedha taslim shilingi milioni tano (5,000,000/-).

Maeneo yaliyoathiriwa na mafuriko hayo mkoani humo ni pamoja na Mpendae kwa Binti Amrani na Mpendae ya Migombani, Mwanakwerekwe, Sebleni na Jang’ombe (Mjini), Kianga, Tomondo, Ziwamaboga na Mtopepo (Magharibi) ambapo nyumba kadhaa zilibomoka kufuatia kujaa maji na kuleta hasara kubwa.

“Chama Cha Mapinduzi ni chama kinachowajali na kuwakumbatia wananchi, ndio maana tulilazimika kusitisha kikao cha sekretarieti ya Kamati Maalum ya NEC Zanzibar,na kwenda kuwakagua na kuwafariji wananchi wote siku iliyotokea mafuriko hayo”. Alisema Naibu Katibu Mkuu huyo wa CCM Zanzibar na kuongeza kusema kuwa “CCM itafanya kila linalowekana kuhakikisha wananchi wanapatiwa kila aina ya misaada, ili waishi kama watu wengine”. Alidai Vuai.

Akitoa neon la shukrani, Mwenyekiti wa Kamati ya Maafa ya Taifa (Zanzibar), ambaye pia ni Waziri Nchi (OMPR) Mhe. Mohame Aboud Mohamed, ameelezea kufarajika kwake kutokana na msaada huo, ambapo alisema umekuja katika wakati muafaka.

Amesema masaada huo kwa kiasi kikubwa utatumika kama ulivyokusudiwa na kukidhi haja ya wananchi  102 waliopo katika kambini ya Mwanakwerekwe, Wilaya ya Magharibi na kuongeza kusema kwamba idadi hiyo huenda ikaongezeka katika siku zijazo.

Akizungumza na Watendaji wa Wizara ya Majenzi pamoja na Manispaa, baada ya kutembelea maeneo yaliyokumbwa na mafuriko hapo mei 5, mwaka huu, aliwataka kutekeleza  wajibu wao ikiwemo kusimamia na kuifanyia marekebisho mitaro ya maji taka, ili iweze kupitisha maji kwa urahisi. 

ufuatia hali hiyo, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein, amewaagiza Mwisho.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni