MAKAMU
Mwenyekiti wa CCM, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.
Dkt. Ali Mohamed Shein, leo (mei 10, 2015) amewaongoza mamia ya Wana CCM
waliohudhuria maziko ya Makada wawili kati ya watu wa Chama Cha Mapinduzi waliofariki
dunia kutokana na ajili ya gari.
Makada hao
waliozikwa katika makaburi ya
Mwanakwerekwe ni pamoja na Mwanaidi
Zamir Haji (28), mkazi wa Magogoni na Mwanahawa Haji Machano (50), mkazi
wa Mkele, Wilaya ya Mjini.
Aidha, Mjumbe
wa Kamati Kuu na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Balozi Seif Ali Iddi, aliwaongoza
wananchi wa Jimbo la Mkwajuni waliohudhuria maziko ya kada mwengine wa CCM Munira
Abdullah (16), aliyezikwa Kijijini kwao Mkwajuni, Wilaya ya Kaskazini “A”.
Wana CCM hao watatu
walifikwa na umati na wengine saba
kujeruhiwa kufuatia gari (basi) walilokuwa wakisafiria kutoka Nungwi kuja Mjini
kupasuka mpira wa mbele na kupinduka baada ya kugonga gari la ng’ombe, katika maeneo
ya Mto wa Pwani, Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Makada
waliolazwa katika Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja, ni pamoja na Maua Haji Khamis
(54), Salhiya Sheha Khamis (26) na Sawadi Haji Khamis (38), wote wakazi wa
Kwamtipura, Mjini Unguja.
Chama Cha
Mapinduzi kimepokea kwa mshituko, kuhuzuni na masikitiko makubwa taarifa za
vifo vya makada wake hao, kwani walikuwa mstari wa mbele katika kikilinda,
kikihifadhi, kukipigania na kukitetea kwa nguvu zao zote Chama hicho. Aidha, wanamuomba Mwenyezi Mungu, Muumba Mbingu na Ardhi, awape nafuu majeruhi wote waliolazwa
hospitali, ili wapone haraka na kuungana na wananchi wengine katika ujenzi wa taifa.
“Kwa niaba ya
Viongozi na Wanachama wa CCM, na kwa niaba yangu binafsi, nachukua nafasi hii
kuwapa mkono wa pole wana familia, ndugu na jamaa wote wa marehemu hao,
kufuati vifo hivyo”. Alisema Naibu
Katibu Mkuu huyo wa CCM Zanzibar Ndugu Vuai Ali Vuai, alipokuwa akiwafariji
moja ya wanafamilia ya maiti hao.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni