Alhamisi, 30 Agosti 2018

MATUKIO KATIKA PICHA ZIARA YA DK.SHEIN KATIKA TAASISI ZA UTAFITI Z'BAR.



















DK.SHEIN AMEFANYA ZIARA KATIKA TAASISI ZA UTAFITI ZANZIBAR.


  RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi akizungumza na Wananchi wa Mkoa wa Kusini Wilaya ya Kati baada ya kumaliza ziara ya kukagua Majengo ya Taasisi ya Utafti wa masuala ya Afya katika maeneo ya Binguni Unguja.
 BAADHI ya viongozi na wanachama wa CCM walioudhuria katika ziara hiyo ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein.
 WANANCHI walioudhuria katika ziara hiyo ya Dk.Ali Mohamed Shein.



NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein amesema serikali itaimarisha taasisi zote za utafiti nchini ziweze kufanya utafti wenye hadhi ya kimataifa. 

Kauli hiyo ameitoa leo wakati akifanya ziara katika taasisi mbali za utafiti ambazo ni taasisi ya Utafti wa Mifugo Langoni Kizimbani Wilaya ya Magharibi "A" pamoja na Taasisi ya Utafti wa masuala ya Afya iliyopo Wilaya  ya Kati Zanzibar. 

Amesema Taasisi hizo ni nyenzo za kuharakisha maendeleo ya Zanzibar kwani katika ulimwengu wa sasa kila jambo lenye kuleta maendeleo ama madhara katika jamii lazima lifanyiwe Utafti wa kitaalamu. 

Dk.Shein Akizungumza mara baada ya kukagua eneo litakalojengwa Hospitali kuu ya kisasa Zanzibar, ambayo itakuwa na taasisi ya utafti ya Afya itakayotoa mafunzo kwa wataalamu wa afya ili waweze kuwa na ujuzi mkubwa wa kutoa huduma za afya kitaalamu. 

Amesema ujenzi wa hospitali hiyo utakapokamilika itawasaidia wananchi wa maeneo mbali mbali ya Zanzibar na kupunguza  msongamano wa wananchi kwenda kufuata huduma za Afya katika hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja.

Dk.Shein ameongoza kuwa hatua hizo ni miongoni mwa utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015/2020 kwa lengo la kutatua changamoto za wananchi na kuwaletea maendeleo.

Ameeleza kwamba  CCM inaendeleza utamaduni wake wa asili wa kutekeleza kwa vitendo miradi mbali mbali ya maendeleo kwa manufaa ya wananchi wote. 

"Hospitali hii itakapokamilika itakuwa na uwezo mkubwa wa vifaa tiba, wataalamu na miundombinu ya kisasa ya masuala ya Afya hivyo wananchi mnaoishi karibu na eneo hili muunge mkono juhudi za serikali.

Pia vijana wetu wenye utaalamu wa masuala ya Afya watakuja hapa kupata mafunzo na kufanya utafti wa tiba za maradhi mbali mbali na kuwatibu wananchi.",amesema Dk.Shein.

Akikagua maendeleo ya ujenzi wa majengo ya Taasisi ya utafti wa Mifugo huko Langoni Unguja,  Dk.Shein amesema taasisi hiyo itasaidia kufanya utafti wa  Mifugo hapa nchini na kupunguza gharama za kwenda Tanzania bara na maeneo mengine kufanya utafti huo.

Mapema Akizungumza Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafti wa Mifugo Zanzibar,Dk.Kassim Gharib Juma amesema taasisi hiyo tayari imefanya utafti mbali mbali wa mifugo ikiwemo Ng'ombe,Mbuzi na kuku ulioweza kuleta tija kwa kubaini maradhi na njia za kitaalamu za kukabiliana na changamoto hizo pamoja na ufugaji bora wa Mifugo hiyo. 

Pia alieleza kwamba wamefanya utafti wa kutengeneza chakula cha wanayama kupitia zao la mwani, ambao utasaidia kuzalisha chakula bora cha mifugo hapa nchini.

Naye Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Zanzibar, Halma Maulid Salum amesema  ujenzi wa majengo mbali mbali ya Taasisi ya utafti wa afya pamoja na Hospitali katika eneo la Binguni Wilaya ya Kati Unguja hadi kukamilika kwake utagharimu kiasi cha shilingi bilioni nne.

Ameeleza kuwa  Wizara ya Afya itasimamia kikamilifu ujenzi wa majengo hayo ili taasisi hiyo itowe huduma bora za Afya kwa jamii.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa CCM zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla (Mabodi), amempongeza Dk.Shein kwa mfumo mzuri wa uongozi shirikishi baina ya Chama Cha Mapinduzi na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 

Amesema mambo mema yanayotekelezwa na serikali ya awamu ya Saba Zanzibar chini ya uongozi wa Dk.Shein inafuata nyayo za utawala wa Rais wa Kwanza wa Zanzibar hayati Abeid Aman Karume kwa kutekeleza miradi ya maendeleo inayodumu kwa muda mrefu kwa maslahi ya jamii. 

Amesema kazi kubwa inayofanywa na serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar  kwa kuimarisha huduma muhimu za kijamii ni miongoni mwa kibali halali cha kisiasa cha  kuiletea ushindi CCM katika Uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.






Jumamosi, 25 Agosti 2018

KHEIR JAMES: ATAKA ELIMU ZA VIJANA ZISAIDIE JAMII ILIYOWAZUNGUKA.


 MWENYEKITI wa UVCCM Taifa Kheir James akiwahubia wanafunzi wa kidato cha sita Zanzibar wa mwaka 2018 waliofaulu kwa kiwango daraja la kwanza, pili na tatu katika hafla ya kuwapongeza iliyoandaliwa na CCM Zanzibar ambayo imefanyika hoteli ya Z-ocean iliyopo Bububu Mkoa wa Mjini  Magharibi Unguja.

 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar ambaye pia ni mlezi wa UVCCM Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi akizungumza katika hafla hiyo ya kuwapongeza wanafunzi wa kidatu cha sita mwaka 2018 Zanzibar.

 MAKAMU Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Tabia Maulid Mwita akizungumza na wanafunzi hao kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi ambaye ni Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Kheir James katika hafla ya kuwapongeza wanafunzi wa kidato cha sita waliofaulu.

 NAIBU Katibu Mkuu wa UVCCM Zanzibar Shaka Hamdu Shaka akizungumza katika hafla ya kuwapongeza wanafunzi wa kidato cha sita Zanzibar waliofaulu masomo yao kwa kliwango cha daraja la kwanza, pili na tatu mwaka 2018, iliandaliwa na CCM.

 
BAADHI ya wanafunzi wa kidato cha sita mwaka 2018 waliofaulu wakifuatilia na kusikiliza nasaha mbali mbali kutoka kwa viongozi wa Chama Cha Mapinduzi na Serikali walioudhuria katika hafla hiyo.


NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR.

MWENYEKITI wa Umoja wa vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa Kheir James amewataka vijana wasomi nchini kuhakikisha tija ya elimu waliyonayo inanufaisha jamii iliyowazunguka kwa maslahi ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Rai hiyo ameitoa leo katika hafla ya kuwapongeza wanafunzi waliofaulu mtihani wa kidatu cha Sita Zanzibar mwaka 2018 kwa kiwango cha daraja la kwanza, la pili na tatu  (Division I,II na III) hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Z-Ocean iliyopo Bububu Wilaya ya Magharibi ‘’A’’  Zanzibar.

Ameeleza kuwa endapo vijana hao watashindwa kuzitumia vizuri elimu zao kwa kuzinufaisha jamii zilizowazunguka basi elimu hizo zitakuwa hazina maana kwao wao na taifa kwa ujumla.

Amesema serikali zote mbili ambazo ni Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar pamoja na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zinaendelea kuthamini vijana kwa kuwawezesha kupitia nyanja mbali mbali hasa za kitaaluma.

Amewataka vijana hao ambao watajiunga na elimu ya juu katika vyuo mbali mbali nchini kuwa wanatakiwa kusoma masomo ambayo wana uwezo nayo ili waweze kufaulu vizuri katika masomo ya elimu ya juu na wawe wataalamu wenye uwezo wa kuleta mabadiliko chanya katika jamii.

Mwenyekiti huyo Kheir amefafanua kwamba CCM na serikali zake mbili inawaamini vijana kwa kuwapatia nafasi mbali mbali za uongozi sio kwa sababu za kujuana bali ni kutokana na sifa walizokuwa nazo kitaaluma.

“ CCM haina vijana wa ovyo ovyo kama zilivyo taasisi zingine za kisiasa bali ina vijana madhubuti, wazalendo,weledi na wenye sifa na kila vigezo vinavyokubalika katika nyanja mbali mbali za uongozi na utendaji katika taasisi za serikali na binafsi.”amefafanua  Mwenyekiti huyo.

Alisema taasisi yoyote isiyokuwa na utaratibu wa kurithisha uongozi kutoka kizazi kimoja kwenda kingine basi taasisi hiyo itakuwa ni sawa na mfu na ndio maana CCM inaendeleza utaratibu wa kuwarithisha na kuwaanda vijana wake kiungozi ili waweze kuwa viongozi bora ndani na nje ya Serikali zao.

Ameeleza kuwa suala la vijana kupendana ni lazima na sio hiari kwani endapo kundi hilo litaendekeza tabia ya kufanyiana fitna, majungu na kuchafuana hawatokuwa na uwezo wa kulinda rasilimali za taifa kwani nguvu nyingi watakuwa wanazitumia kuchafuana badala ya kufanya mambo ya maendeleo.

Pia amewataka viongozi wa serikali kuendeleza utamaduni wa kusema na kutangaza mambo mema yanayofanywa na serikali kwa wananchi pamoja na kutoa ufafanuzi wa masuala mbali mbali yanayopotoshwa na baadhi ya watu wasioitakia mema CCM na serikali zake.

Pamoja na hayo aliwambia viongozi vijana walioaminiwa na kupewa nafasi za uongozi ndani ya Chama na Serikali wafanye kazi zao kwa uadilifu ili vijana na wananchi kwa ujumla waendelee kuwaamini na kujifunza mambo mema kutoka kwao.

Mwenyekiti huyo amekemea vikali tabia za baadhi ya vijana wanaopenda kulalamika bila ya kujituma kufanya kazi kwa kubuni mambo mbali mbali ya kuwaingizia kipato pamoja na kulitumikia taifa kwa maendeleo endelevu.

Kupitia hafla hiyo ameipongeza CCM Zanzibar kwa juhudi zake  za kuendeleza utamaduni wa kuwaamini vijana wasomi kwa kuwapatia fursa mbali mbali zinazowasaidia kupata elimu ya juu na mafunzo ya ujasiriamali bila ya usumbufu.


Aidha Kheir amempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein kwa kuipa kipaumbele sekta ya elimu pamoja na kuimarisha Amani na Utulivu wa Zanzibar hatua ambayo imechangia kuharakisha maendeleo ya nchi.

Naye Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla (Mabodi) amesema Chama Cha Mapinduzi kinaendelea kulea kitaaluma vijana wa makundi yote ili waweze kunufaika na rasilimali za nchi.

Amesema CCM Zanzibar inatekeleza mipango mbali mbali ya kuwawezesha vijana kwa kuwajengea mazingira bora yatakayowawezesha kujiajiri wenyewe na kuwasaidia vijana wenzao ambao bado hawajafika ngazi ya elimu ya juu.

 Pia ameeleza kwamba taasisi hiyo pia inaendelea na mikakati ya kuanzisha miradi mikubwa ya ujasiriamali itakayowezesha vijana ambao hawakufika elimu ya juu kuweza kujiajiri wenyewe.

“Chama chetu kinajali vijana wa makundi yote na sio wasomi pekee na ndio maana mipango yetu ya kuwajengea uwezo ipo kwa vijana wa makundi yetu na ndio maana hata nchi yetu imekombolewa na vijana waliokuwa wakwezi na wakulima.”, amesema Dk.Mabodi.

Mapema Makamu Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Tabia Maulid Mwita amesema vijana hao wapo tayari kutumia uwezo wao wote kulinda na kuthamini mambo mema yanayotekelezwa na Serikali zote mbili chini ya usimamizi wa Chama Cha Mapinduzi.

Hafla  hiyo imeandaliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar  kwa kushirikiana na UVCCM  kwa lengo la kuwapongeza vijana 470 wa kidato cha sita Zanzibar waliofaulu kwa kiwango cha daraja la kwanza, pili na tatu (Division I,I na III) mwaka 2018.

Jumatatu, 20 Agosti 2018

DK.BASHIRU AITAJA MIKAKATI YA KUKUZA UCHUMI WA CCM

 VINGOZI mbalimbali wa CCM na UVCCM wakiwa katika uwanja wa ndege wa Pemba kwa ajili ya kumuaga Katibu Mkuu wa CCM Tanzania Dk.Bashiru Ally ambaye amehitimisha ziara yake  kisiwani Pemba.

 MAKATIBU wa Idara za CCM Zanzibar  Katibu wa Kamati maalum ya NEC, Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa ambaye pia ni Mjumbe wa kamati kuu ya CCM Taifa Mwl.Kombo Hassan Juma (kushoto wa kwanza), Katibu wa kamati maalum ya NEC, Idara ya Uchumi na Fedha CCM Zanzibar ambaye  Mjumbe wa kamati kuu ya CCM Taifa Afadhali Taib Afadhali (wa pili kushoto), Katibu wa Kamati maalum ya NEC, Idara ya Organazesheni CCM Zanzibar Ndugu Bakar  Hamad Khamis (kulia) wakiwa uwanja wa ndege wa Pemba kwa ajili ya kumuaga Katibu Mkuu wa CCM Tanzania Dk.Bashiru Ally.

NAIBU Katibu Mkuu wa UVCCM Zanzibar Ndugu Shaka Hamdu Shaka(kulia) akiagana na Katibu mkuu wa CCM  Tanzania Dk.Bashiru aliyekuwa kisiwani Pemba kwa ajili ya ziara.


Katibu mkuu wa CCM  Tanzania Dk.Bashiru Ally akisalimiana na Makamu Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Tabia Maulid Mwita katika uwanja wa ndege wa Pemba. 






 Katibu wa kamati maalum ya NEC, Idara ya Uchumi na Fedha CCM Zanzibar ambaye  Mjumbe wa kamati kuu ya CCM Taifa Afadhali Taib Afadhali (kushoto) akiagana na Katibu Mkuu wa CCM Tanzania Dk.Bashiru Ally.


Katibu Mkuu wa CCM Tanzania Dk.Bashiru Ally akiwapungia mkono viongozi mbali mbali wa CCM waliokuwa uwanja wa ndege kwa ajili ya kumuaga na kumsindikiza baada ya kumaliza ziara yake na kuelekea Dar es saalam kwa ajili ya majukumu yake.



NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR.

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Dk.Bashiru Ally amesema Chama hicho kinadhibiti ubadhilifu wa mali na matumizi mabaya ya rasilimali fedha ili kijitegemee kiuchumi.

 Amesema endapo rasilimali hizo zitatumika vizuri na kuanzishwa kwa miradi mingine mikubwa ya uzalishaji wa kipato katika ngazi mbali mbali za chama na jumuiya ili ziwanufaishe wanachama wote badala ya watu wachache.

Kauli hiyo katika ziara yake kisiwani Pemba wakati akizungumza na viongozi na wanachama wa Chama cha Mapinduzi wa Mikoa Miwili katika ukumbi wa Fidel Castro uliopo, Mkoa wa Kusini Pemba.

Dk.Bashiru ameeleza kuwa lengo la kusimamia dhana ya ukuaji wa uchumi ndani ya chama kupitia vyanzo vyake vya mali na fedha ni kukiondosha chama katika mazoea ya kutegemea ufadhili wa watu wenye fedha wanaokuwa na malengo ya kujinufaisha wenyewe kisiasa.

Pia ameyataja malengo mengine kuwa ni uimarishaji wa maslahi ya watumishi wa CCM na jumuiya zake kwani bado maslahi yao ni ya kiwango cha chini ambayo hayaendani na hadhi ya taasisi yenyewe.

Ameeleza kuwa malengo hayo yakifanikiwa utakuwa ni ushindi mkubwa kwa wanachama wa CCM wote kwani tabia za rushwa na makundi ya kusaka nafasi za uongozi kwa kutumia fedha yatakuwa yamedhibitiwa.

Amewasisitiza viongozi wote wa taasisi hiyo kuunga mkono malengo hayo kwa kuhakikisha wanapunguza matumizi holela ya fedha na badala yake waanzishe miradi itakayowasaidia kujiendesha ili kulinda heshima na hadhi ya CCM mbele ya jamii.

Pamoja na hayo amezitaka taka jumuiya zote hasa ya umoja wa vijana (UVCCM) kuhakikisha wanakuwa wabunifu kwa kutumia rasilimia walizonazo kwa kuanzisha miradi mikubwa ya kilimo, uvuvi na viwanda vidogo vidogo ili vijana wajiajiri wenyewe.

Katibu Mkuu huyo Dk.Bashiru amewaka  wazi msimamo wa Chama Cha Mapinduzi kuwa wale wote waliohusika na kutapeli na kujimilikisha mali za taasisi hiyo kinyume na utaratibu wote watachukuliwa hatua za kisheria.

Naye Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Mabodi alisema wanachama wote wana haki ya kuunga mkono mambo mema yanayotekelezwa na taasisi hiyo kwa nia ya kuongeza ufanisi.

Amesema wakati wa vyama vya ukombozi vya ASP na TANU viongozi wa wakati huo walifanikiwa kupanga mambo ya maendeleo yaliyodumu kwa muda mrefu kutokana na umoja na mshikamano waliokuwa nao hasa katika masuala ya kuvijenga kimaendeleo vyama vyao.

Dk. Mabodi ameeleza  kuwa suala la uzalendo katika kusimamia maslahi ya kitaifa ni jambo muhimu hasa kwa viongozi wanaoaminiwa na kupewa dhamana za kuongoza jamii.

Akizungumzia ushindi wa CCM visiwani Zanzibar mwaka 2020 alisema mpaka sasa Zanzibar hakuna upinzani bali kuna vikundi vidogo vidogo vya watu wanaojivisha joho la upinzani wakati wao ni madalali wa kisiasa waliofilisika kifikra.

Naibu Katibu Mkuu huyo amesema  CCM itashinda kisayansi kutokana na serikali zake kutekeleza mahitaji ya wananchi wa mijini na vijijini kupitia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2015/2020.

.


Jumapili, 19 Agosti 2018

DK.BASHIRU ASEMA CCM INAZIDI KUIMARIKA

 


NA IS-HAKA, ZANZIBAR.

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Dk.Bashiru Ally amesema CCM inaendelea kuimarika na hakuna Chama chochote cha kisiasa nchini kinachoweza kushindana na taasisi hiyo katika uringo wa siasa za ushindani wa sera za maendeleo kwa wananchi.

Kauli hiyo aliitoa mara baada ya kuwasili kisiwani Pemba katika mwendelezo wa ziara yake ya kujitambulisha ambapo amezungumza na wanachama mbalimbali katika ukumbi wa Skuli ya Sekondari ya Fidel Castro Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Amesema kutokana na uimara huo hakuna chama kingine mbadala wa Chama Cha Mapinduzi kinachoweza kushuka kwa wananchi nyumba kwa nyumba na kutatua changamoto za wananchi.  

Dk.Bashiru amewahakikishia wanachama na viuongozi hao kuwa CCM bado ipo imara na itapata ushindi wa kihistoria mwaka 2020 kwa nchini nzima kuliko ushindi unaopatikana kwa sasa katika uchaguzi mdogo unaoendelea katika maeneo mbalimbali nchini.

Ameongeza kwamba sababu za Chama Cha Mapinduzi kushinda kwa kishindo kwa kila uchaguzi huku vyama vya upinzani vikisambaratika na kukosa muelekeo wa uhalali wa kuitumikia jamii.

Kupitia mkutano huo aliwambia wanachama wa vyama vya upinzania kisiwani Pemba kwamba huu ndio wakati wao wa kujitawala kifikra kwa kujiunga na CCM kwani Chama Cha CUF hakina tena mvuto kwa jamii kutokana na tabia ya unafiki na uongo unaofanywa na viongozi wakuu wa CUF.

 Dk.Bashiru kupitia mkutano huo alitangaza rasmi kuwa Chama Cha Mapinduzi kitaendelea kuvunja ngome zote za upinzani kabla ya mwaka 2020, ambapo mamlaka hayo yanatokana na usimamizi mzuri wa utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi wa CCM ya mwaka 2015/2020.

Kupitia mkutano huo pia Dk.Bashiru aliwapokea wanachama wapya 62 waliotoka chama cha CUF na kujiunga na CCM kisiwani Pemba.

Aliwapongeza wanachama wajumbe wote wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kwa kumuamini kasha kupendekeza ateuliwe kushika nafasi ya Katibu Mkuu wa CCM Tanzania, na akaahidi kuwa atatumia nafasi yake kuleta mageuzi makubwa ya kiutendaji ndani na nje ya Chama Cha Mapinduzi.

Akizungumza Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla (Mabodi), amesema kazi kubwa ya Chama cha mapinduzi kwa zama za sasa ni kutekeleza kwa vitendo dhana ya CCM mpya na Tanzania mpya kwa maendeleo ya jamii.

Amefafanua kuwa miradi mbali mbali ya maendeleo iliyotekelezwa kwa ufanisi kisiwani Pemba ikiwemo mfuko wa maendeleo wa TASAF na kuongeza bei ya zao la karafuu ni kutokana na utekelezaji mzuri wa sera za CCM.

Naye Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kusini Pemba Ndugu Yussuf Ali Juma amesema ndani ya Mkoa huo wanaendelea na mikakati ya kuhakikisha CCM inashinda kwa ngazi zote katika uchaguzi Mkuu ujao.

Katika ziara hiyo Dk. Bashiru alifuatana na viongozi mbali wa Chama na Jumuiya wakiwemo wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, wajumbe wa halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Makamu Wenyeviti wa Jumuiya pamoja na viongozi mbali mbali wa Chama na Serikali Zanzibar.

MATUKIO KATIKA PICHA ZIARA YA DK.BASHIRU PEMBA.

 KATIBU Mkuu wa CCM Tanzania Dk.Bashiru Ally akivishwa sikafu mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Pemba akitoka Unguja. 
KATIBU Mkuu wa CCM Tanzania Dk.Bashiru Ally akisalimiana na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Mwl.Kombo Hassan Juma mara baada ya kuwasili Pemba kwa ajili ya kuendelea na ziara yake kisiwani humo.

 KATIBU Mkuu wa CCM Tanzania Dk.Bashiru Ally akisalimiana na mwakilishi wa Jimbo la Chake Chake Suleiman Sarahan mara baada ya kuwasili uwanja wa ndege wa Pemba kwa ajili ya ziara ya kujitambulisha. 

 KATIBU Mkuu wa CCM Tanzania Dk.Bashiru Ally akisalimiana na Makamu Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Ndugu Tabia Maulid Mwita mara baada ya kuwasili uwanja wa ndege wa Pemba.

 KATIBU Mkuu wa CCM Dk,Bashiru akiangalia  ngoma ya kirumbizi kutoka Mkoa wa kusini Pemba ambayo ni miongoni mwa mapokezi ya kiongozi huyo.

 KATIBU Mkuu wa CCM Tanzania Dk.Bashiru akipokelewa na vijana wa UVCCM kwa wimbo wa mashujaa katika Uwanja wa Ndege wa Pemba.

 KATIBU Mkuu wa CCM Tanzania Dk.Bashiru Ally na msafara wake wakitembea  kwa maandamano ya mapokezi kuelekea ofisi ndogo ya CCM Chake chake mjini Pemba.


Mwenyekiti wa  Baraza la Wazee wa Chama Cha Mapinduzi Pemba  Ali Hamad Khatib  akimpokea na kumpa nasaha Katibu Mkuu wa CCM Dk.Bashiru baada ya kufika katika Ofisi Ndogo ya CCM Pemba.


 KATIBU Mkuu wa CCM Tanzania  Dk.Bashiru akizungumza na Watumishi wa CCM wa Ofisi ndogo ya Chama Cha Mapinduzi Zanzibar.

 MWANACHAMA mpya kutoka CUF Amina Juma Kassim  ambaye ni miongoni mwa wanachama waliohama katika chama hicho na kujiunga na CCM, akisalimiana na Katibu Mkuu wa CCM Tanzania Dk.Bashiru Ally.


 
 BAADHI ya Wana-CCM wakifuatilia kwa karibu matukio yanayoendelea katika Mkutano wa Katibu Mkuu wa CCM Dk.Bashiru uliofanyika leo katika Ukumbi wa skuli ya Fidel Castro.

 KATIBU Mkuu wa CCM Tanzania Dk.Bashiru Ally akiwahutubia wanachama na viongozi wa CCM katika ukumbi wa skuli ya Fidel Castro Mkoa wa Kusini Pemba.

 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Mabodi akizungumza na viongozi na wanachama wa CCM kabla ya kumkaribisha Katibu Mkuu wa CCM Dk. Bashiru katika ukumbi wa Skuli ya Fidel Castro.

 MWENYEKITI wa CCM Mkoa  wa Kaskazini Pemba  Ndugu Mbwerwa Hamadi Mberwa akimkabidhi zawadi ya ndizi ya mkono wa Tembo Katibu Mkuu wa CCM Tanzania Dk.Bashiru  Ally katika ziara ya kujitambulisha kwa wanachama wa CCM Pemba.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kaskazini Pemba Ndugu Mbwerwa Hamad Mberwa  ya ngao ya mwenge wa uhuru Katibu Mkuu wa CCM Tanzania Dk.Bashiru kutoka Mikoa miwili ya Pemba.


 MWENYEKITI wa CCM Mkoa wa Kusini Pemba Yussuf Ali Juma akiwakaribisha viongozi mbalimbali katika Mkoa wa Kusini Kichama.