Jumapili, 12 Agosti 2018

DK.MABODI AZIFARIJI FAMILIA ZA WATU WALIOFARIKI KWA AJALI

 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi (aliyevaa kanzu na koti nyeusi) akiwa katika ziara ya kuzifariji familia za ndugu wa watu watatu waliofariki dunia kwa ajali katika Kijiji cha Ndagaa Wilaya ya kati Mkoa wa Kusini Unguja. 

 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi (aliyevaa kanzu na koti nyeusi) akiwapa pole ndugu wa familia ya Ndugu Francis Haroun aliyefariki katika ajali ya gari mkaazi wa kijiji cha Ndagaa Wilaya ya Kati Unguja.

 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi (aliyevaa kanzu na koti nyeusi) akimkabidhi  fedha ya ubani ndugu wa marehemu Francis Haroun, ndugu Said Sadi (alivaa tisheti ya rangi nyekundu).

NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi (aliyevaa kanzu na koti nyeusi) akiwa pole familia ya ndugu Yoana Antony alifariki katika ajali hiyo.

 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi (aliyevaa kanzu na koti nyeusi) akiwapa pole vijana wawili waliojeruhiwa katika ajali hiyo ambao ni Said Masoud na Mudrik Salum Dude.


 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi (aliyevaa kanzu na koti nyeusi) akizungumza Ndugu Suleiman Ali Makisa ambaye ni babu wa ndugu Suleiman Abdullah Miraj aliyefariki Dunia katika ajali hiyo.

 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi (aliyevaa kanzu na koti nyeusi) akizungumza Ndugu Jabir Ali Mtonga ambaye ni miongoni mwa majeruhi walionusurika katika ajali hiyo.  
 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi (aliyevaa kanzu na koti nyeusi) akimfariji ndugu Elisha Simon ambaye ni mume wa bi.Agata Francis Pius aliyeuawa na watu wasijulikana kwa mapanga siku za hivi karibuni katika kijiji cha Ndagaa.

 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi (aliyevaa kanzu na koti nyeusi) akimfariji ndugu Ali Omar Risasi ambaye ni miongoni mwa majeruhi wa ajali hiyo.




NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR.

NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Zanzibar Dk. Abdulla Juma Saadalla Mabodi amezitembelea na kuzifariji familia za ndugu wa watu watatu waliofariki kwa ajali ya gari aina ya noah na wengine wanne  kujeruhiwa vibaya.

Waliofariki katika ajali hiyo ni Francis Haroun (28), Yoana Antony (20) na Suleiman Abdalla Miraj (18) ambapo majeruhi ni Jabir Ali Mtonga (29), Ali Omar Risasi (17), Said Masoud (14) na Mudrick Salum Dude.

Akizungumza na familia hizo Naibu Katibu Mkuu huyo Dk.Mabodi huko katika kijiji cha Ndagaa Wilaya ya kati Mkoa wa Kusini Unguja alisema CCM imepokea kwa mshutuko,majonzi na uzuni  mkubwa taarifa za ajali hiyo iliyopoteza maisha ya watu muhimu katika ujenzi wa maendeleo ya kitaifa.

Dk. Mabodi alisema Makamu Mwenyekiti wa CCM Taifa ambaye pia ni Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein amesikitishwa na msiba huo mzito na kuzipa pole familia zote ambazo ndugu zao wamepata ajali hiyo.

Aliziomba familia zote ambazo ndugu zao wamefariki kutokana na matukio mbali mbali ya ajili zilizosababisha vifo hivyo kuwa na subra na uvumilivu kwa kipindi hiki kigumu na kuwaombea dua na ibada marehemu hao ili mwenyezi mungu awasamehe madhambi yao na kuwalaza mahali pema peponi amin.

Naibu katibu Mkuu huyo aliwasihi madaktari na wauguzi wanaowatibu majeruhi walionusurika kifo kupitia ajali hiyo kuhakikisha wanawafanyia vipimo vya mara kwa mara sambamba na kutibu majeraha waliyoyapata kwa umakini ili watu hao wapone haraka na kuendelea na shughuli zao za ujenzi wa taifa.

Pia Naibu Katibu Mkuu huyo ameitembelea familia ya marehemu bi.Agata Francis Pius (48) aliyeuawa kwa kukatwa na mapanga na watu wasiojulikana siku za hivi karibuni.

Akizungumza na ndugu wa marehemu huyo, Dk.Mabodi amelitaka jeshi la Polisi nchini kukamilisha kwa wakati upelelezi wa mauaji hayo na kuwakama watu wote waliosababisha kifo hicho ili wafikishwe katika vyombo vya kisheria.

“ Wananchi wote wa kijiji cha Ndagaa na vijiji jirani nakupeni pole sana na mendelee kuamini kwamba CCM ipo pamoja nanyi kwani hiki ni Chama cha kisiasa kilichotokana na wakwezi na wakulima, na ndio maana tupo karibu na wananchi wa makundi yote bila kujali tofauti za kisiasa na kidini.”, alisema Dk.Mabodi akiwa katika hali ya uzuni mkubwa juu ya misiba hiyo.

Mara baada ya kumaliza ziara maalum ya kuzifariji familia hizo, Dk.Mabodi alizungumza na Kamati ya siasa ya Tawi la CCM Ndagaa na kuwaagiza viongozi wake kujenga utamaduni wa kuwatembelea mara kwa mara wananchi wa maeneo hayo ili kubaini changamoto zinazowakabili na kuzitafutia ufumbuzi.

Alisema kwa sasa hakuna nafasi ya viongozi na watendaji wa CCM na jumuiya zake kulala na kusubiri kazi za maofisini bali wanatakiwa kwenda kwa wananchi kuratibu na kubaini kasoro zilizopo kwa wananchi ili zitatuliwe na taasisi husika.

Mapema akizungumza Mwenyekiti wa Tawi la CCM Ndagaa, Abdulrahman Abdallah Said alisema kwa niba ya kamati ya siasa ya Tawi hilo watalifanyia kazi agizo hilo lenye lengo la kuongeza ufanisi ndani ya Chama Cha Mapinduzi.

Naye Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kusini, Ndugu Ramadhan Abdullah Ali alimpongeza Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk. Mabodi kwa utaratibu wake wa kuwa karibu na wananchi wa rika zote wakati wote.
Mwenyekiti huyo alikiri kuwa ajali hiyo iliyosababisha vifo vya watu watatu kwa wakati mmoja na kuongeza kuwa imeuweka katika simanzi Mkoa huo na kuwasihi madereva wote wa gari na pikipiki kuendesha vyombo vyao kwa mwendo wa kawaida ili kuepuka na ajali.

Ajali hiyo iliyotokea ilitokea katika eneo la Kibuteni Augost 9 mwaka huu ambapo gari aina ya Noah iliyokuwa na abiria 15 kati ya hao watatu wamefariki hapo hapo na sita kupelekwa hospitalini wakitoka kijiji cha Ndagaa Wilaya ya Kati na kwenda kijiji cha Makunduchi harusini. 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni