Jumamosi, 17 Machi 2018

ALI SALUM 'KIROVA' - MAFUNZO YA ITIKADI NDIO NJIA MBADALA YA KUWAKOMBOA VIJANA WA CCM KIFIKRA


 MWAKILISHI wa Jimbo la Kwahani, Mhe Ali  Salum Haji akifungua mafunzo ya Darasa la Itikadi katika Tawi la CCM Sebleni.  
 KATIBU wa Siasa na Uenezi CCM Wilaya ya Mjini, Ndugu Fatma Haji Mohamed akizungumza na vijana na Wana CCM katika hafla hiyo ya ufunguzi wa Darasa la Itikadi.



 MWALIMU wa Darasa hilo  Ndugu Abdallah Juma Nafaika akitoa nasaha zake katika hafla hiyo.

 BAADHI ya washiriki wa mafunzo hayo wakifuatilia kwa makini nasaha mbali mbali zinazotolewa na viongozi katika hafla hiyo.



NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR.

VIJANA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wameshauriwa kujiunga na madarasa ya itikadi ili kunufaika na fursa mbali mbali zikiwemo kujua historia halisi ya Zanzibar, mwenendo wa kisiasa, uzalendo  pamoja na elimu ya kujitambua.

Ushauri huo umetolewa na Mwakilishi wa Jimbo la Kwahani Zanzibar Ali Salum Haji wakati akifungua mafunzo ya  darasa la Itikadi katika Tawi la CCM Sebleni Zanzibar.

Amesema baadhi ya vijana wa CCM wanapoteza muda katika vikundi visivyokuwa na faida badala ya kujiunga na madarasa hayo kwa lengo la kupata elimu  juu ya masuala ya siasa na historia.

Amefafanua kuwa mafunzo ya itikadi ndio njia mbadala ya kuwakomboa kifikra vijana wa Chama Cha Mapinduzi ili wawe makada imara wenye misimamo isiyoyumba kisiasa, kiungozi na kiitikadi.

 “ Vijana someni historia ya nchi yetu kwani kuna mambo mengi yanayopotoshwa na wapinzani kwa makusudi ili vijana mtoke katika msimamo wenu wa kulinda na kutetea maslahi ya Chama Cha Mapinduzi.”, amesema Salum.

Kupitia ufunguzi wa mafunzo hayo Mwakilishi huyo amesisitiza umuhimu wa Wana CCM kuifanyia kazi falsafa ya siasa na uchumi ili kuwa wabunifu wa kutumia vizuri fursa zilizowazunguka katika mazingira wanayoishi kwa lengo kujipatia kipato cha kujikwamua kiuchumi.

Pia ameahidi kuwalipia mafunzo ya ujasiriamali vijana wote watakaohitimu mafunzo hayo ya itikadi ili baada ya kupata ujuzi wajiajiri wenyewe.

Naye Katibu wa Siasa na Uenezi CCM Wilaya ya Mjini, Fatma Haji Mohamed amesema ufunguzi wa darasa hilo ni miongoni mwa mikakati ya kudumu iliyopangwa na Wilaya hiyo kupitia mpango kazi wao.

Amesema  lengo la kuanzia mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo vijana na wananchama juu ya  kutambua masuala ya Itikadi na Siasa zinazoendana na zama za sasa katika ushindani wa kisiasa.

Amesema mpango huo utakuwa endelevu katika Matawi na Wadi zote za Wilaya hiyo sambamba na kuwapatia vijana hao elimu ya ujasiria mali.

Jumla ya vijana 76 wameanza mafunzo hayo katika Tawi la Sebleni, na yatachukua muda wa miezi mitatu.

Jumamosi, 10 Machi 2018

MAWAKILI WA KUJITEGEMEA MSIWATETE WAZALILISHAJI



NA EMMANUEL MOHAMED, ZANZIBZR

NAIBU Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi Taifa wa Chama Cha Mapinduzi(CCM),Najma Murtaza Giga, amewataka mawakili wa kujitegemea kutojiingiza katika kuwatetea watu wanaofanya vitendo vya udhalilishaji.

Amesema vitendo hivyo vimekuwa vikiongezeka siku hadi siku visiwani humu ambapo imefika wakati watu hao wasionewe aibu ama muhali kupelekwa kwenye vyombo vya sheria.

Hayo aliyasema jana katika ufunguzi wa kikao cha Baraza la Jumuiya hiyo Mkoa wa Mjini, Naibu huyo alisema baada ya wananchi kupata elimu ya kutosha katika kujitokeza kutoa ushahidi sasa imebakia vyombo vya sheria kutoa ushirikiano kwao.

Najma aliongeza kuwa miongoni mwa majukumu ya jumuiya hiyo ni kukemea hali hiyo ambapo ni sehemu ya mmonyoko wa maadili kwa jamii na kwamba jumuiya inapaswa kuwa mstari wa mbele katika mapambano hayo.

"Sisi kama wanajumuiya tunawataka mtu ambaye amefanya vitendo hivyo wasisitetewe kutokana na nafasi yake ama kwa sababu anafanya kazi kutoka serikalini au sekta binafsi hivyo suala hili halitakiwi kuacha kiholela,"alisema 

katika maelezo yake Naibu huyo alisema jambo hili haitakiwi kutetewa ama kukingiwa kifua mtu ambaye anafanya vitendo hivyo akiwa ana nafasi ya kiongozi ama vyovyote vile.

"CCM tushatoa tamko kuwa yeyote aliyefanya akiwa mfanyakazi wa serikali ama kiongozi hatakiwi kutetewa mtu yeyote atakayekuwa anafanya vitendo hivyo,"alisema

Kwa upande wake Katibu wa Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Zanzibar, Kombo Hassan Juma, alisema jukumu la jumuiya ya wazazi ni kuhakikisha maadili ya jamii hayaharibiki.

Alisema jumuiya ya wazazi ina kazi ya kuwalea watoto na kwamba inapaswa kuwahamasisha vijana kutambua maadili ya jamii na kufanya kila mbinu kutekeleza kwa vitendo maneno yanayosemwa samaki mkunje angali mbichi.

Katibu huyo aliongeza kuwa jumuiya hiyo inapaswa kuwaaminisha vijana kuwa bila ya CCM nchi haitawezekana kwa kufanya hivyo itasaidia kurahisisha kazi za chama.

Awali Katibu huyo wa Idara hiyo alikabidhiwa gari aina ya "Hiace Custom" kwa jumuiya hiyo ya mkoa wa Mjini kwa ajili ya shughuli za kikazi ambapo limetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi Taifa Najma.

Naye Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Mjini, Ali Othaman, alishukuru kwa kupewa gari hilo ambalo litasaidia kurahisisha shughuli za kikazi za jumuiya hiyo.

Mwenyekiti huyo alisema gari hilo litatumika kwa utaratibu ambao utakuwa rahisi kutumika kwa kila ngazi ikiwemo jimbo, tawi, jumuiya hadi chama na kwamba ikiwezekana kukodisha kwa ajili ya biashara na kitakachopatikana kitagawewa.









HIMAHIMA YAFANYA USAFI PANGAWE


NA EMMANUEL MOHAMED,ZANZIBAR

TAASISI isiyokuwa ya kiserikali ya Hima Hima,imefanya usafi katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Mjini, visiwani humu ambapo ni sehemu ya kuzuia maambukizi ya magonjwa ya milipuko.

Akizungumza baada ya kufanya usafi huo,Katibu wa Uhusiano wa Taasisi hiyo,Othman Kibwana alisema taasisi hiyo inatarajia kufanya usafi endelevu kwenye majimbo yote ya mjini ambayo yako kwenye hali isio nzuri.

Katibu huyo aliongeza kuwa hatua hiyo itasaidia kutoa fursa kwa vijana ya kujiajiri kwenye ubebaji taka kama ilivyo agizwa na Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar(SMZ).

"Tumeamua kufanya hivi kutokana kuwa kipindi kinachokuja ni cha mvua hivyo mazingira ya yanapaswa kuwa safi ili kutotokea kwa magonjwa ya milipuko kama kipindipindu hivyo moja ya mipango yetu ni kufanya usafi kwenye maeneo hayo ya majimbo yasiokuwa safi,"alisema Katibu huyo.

Aliongeza kuwa Taasisi hiyo imeanzia kufanya usafi kwenye maeneo ya Pangawe kutokana na kuwa taasisi hiyo ya Hima Hima imefanya tafiti na kubaini kuwa sehemu hiyo ndio ina mazingira ya sio kuwa safi.

"Kuna maeneo ambayo yana taka nyingi lakini kutokana na sababu zisizotatulika ikiwemo kukosa vitendea kazi, magari ya kubebea taka ambapo taka nyingi zinakaa kwa muda mrefu hivyo leo tumeamua kuanzia hapa na kwengine ni Magogoni pamoja na sehemu ambazo milipuko ikija inakuwa ya mwanza kutokea,"alisema

Kwa upande wake Mwakilishi wa jimbo la Pangawe, Khamis Juma Mwalim,alisema hatua hiyo ya taasisi hiyo kufanya usafi kwenye maeneo hayo ya Pangawe itasaidia kutatua changamoto ambazo zilikuwa zikichochea kuwa na mazingira machafu.

Alisema kipindi hichi katika maeneo hayo ya Pangawe kumekuwa na wingi wa taka pamoja na vijana kujaribu kuzizoa na kwamba hatua hiyo ya taasisi hiyo itasaidia kuziondoa kwa uwepesi.

"Taka hizi zitaondoka kwa haraka kutokana na kuwa vifaa vya kubebea viko vingi ikiwemo magari ya taka na nguvu kazi ya kubebea taka hizo wako wengi hivyo usafi wa mazingira kwenye eneo la Pangawe litakuwa limekwisha,"alisema.  

Naye Mjumbe wa Taasisi hiyo ya Hima Hima,Nadra Juma Mohamed, alisema ufanyaji usafi huo ni moja ya hamasa katika kusafisha maeneo ya mbalimbali ya Zanzibar ili kuepuka na magonjwa hayo ya milipuko.

"Wananchi wanatakiwa kuhakikisha wanakuwa na tabia ya kufanya usafi na kwamba wasiingize na itikadi yeyote hivyo ni lazima tupende mazingira yetu yenyewe,"alisema

Mjumbe huyo alisena ufanyaji usafi ni moja ya fursa ya ajira kwa vijana na kwamba watu wakiwa wanatoa gharama za kulipia ili kubebewa taka wanapata kuwa na ajira ya uhakika hivyo kundi hilo linapaswa kuona umuhimu huo.





KATIBU WA IDARA YA UENEZI ZANZIBAR ATEMBELEA VYOMBO VYA HABARI BARA

Mkuu wa Idara ya Itikadi na Uenezi Zanzibar Nd. Catherine  Peter Nao  akisalimiana na Afisa Tawala wa wilaya ya Ilala ndugu Edward Mpogolo walipokutana katia kituo cha Redio cha cloud Media jijini Dar es salam picha na Emmanuel Ndege 

Mkuu wa Idara ya Itikadi na Uenezi Zanzibar, Nd Catherini Peter Nao  akiteta jambo na mangazaji wa kipindi cha leo tena wa cloud baada ya kutembelea kituo hicho jana Bi cathetini Peter  Nao yupo jijini dar es saalam kwa ajali ya ziara ya kwa vyombo vya habari .picha zote na Emmanuel  Ndege.

Mhariri Mkuu wa Gazeti la Matazanaia ndugu Kulwa Karedia akimkaribisha Mkuu wa Idara ya Itikadi na Uenezi Zanzibar Nd. Catherine Peter Nao wakati  alipomtembelea ofisni kwake sinza jijini Dae es ssalam 

Mkuu wa Idara ya Itikadi na Uenezi Zanzibar Nd. Catherine Peter Nao akisalimia na
Nd. Hussein Bashe mara tu baada ya kufika ofisni kwake  

Mkuu wa Idara ya Itikadi na Uenezi Zanzibar akiwa katika picha ya pamoja na Uongozi wa 
Sahara Media wamiliki wa  Star TV ,na Redio Free Afrika Ofisni kwao Jijini 

Mkuu wa Idara ya Itikadi na Uenezi Zanzibar akiwa katika picha ya pamoja na Uongozi wa  sahara media wamiliki wa  Star TV ,na Redio Free Afrika ofisni kwao jijini 





Ijumaa, 9 Machi 2018

KATIBU WA IDARA YA ORGANAIZESHENI ZANZIBAR ATEMBELEA JUMUIYA YA WAZAZI

Lengo la CCM ni kushinda Uchaguzi na sio vyengine. Kauli hiyo imesemwa na Katibu wa Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Organaizesheni Zanzibar Nd. Bakari Hamad Khamis wakati alipofanya Ziara katika Afisi Kuu za Jumuiya ya Wazazi Zanzibar iliopo hapo Kikwajuni.
Amesema Chama kinapendelea kuwa na wanachama wengi ambao watapelekea kuzidi kuimarisha zaidi Hivyo ameshauri jumuiya kuwa makini pindi wanapoingiza wanachama kufanya hivyo kutapelekea mafanikio makubwa ndani ya chama pamoja na jumuiya zake.
Ameleza kuwa lengo la Ziara yake ni kujitambulisha kwao iliwaweze kutambuana na  kufanya kazi kwa pamoja na sio vyengine. Pia alisema kuwa lengo la Chama cha Mapinduzi ni kuhakikisha kuwa kinashinda katika kila Chaguzi. Kwani ndio madhumuni na Malengo ya Chama bila hivyo lengo la chama litakuwa halikutimia.  Hivyo sasa ni wakati muafaka wa kuanza kazi nasio kuzembea tu.
Nae Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi Taifa Nd. Najma Murtaza Giga amempongeza katibu kwa kuteuliwa kuongoza Idara hiyo ya Organaizesheni Zanzibar. Hivyo ameahidi kuwa watatoa ushirikiano katika kila jambo ambalo litakalo kuwa hitajika kusaidia na kumalizia kusema kwani lengo letu ni moja tu kuhakikisha chama kinaongoza Dola nasio vyenginevyo. 

KATIBU wa Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Organaizesheni Zanzibar  Nd. Bakari Hamad Khamis akisaini kitabu cha Wageni mara tu baada ya kuwasli katika Afisi Kuu ya Jumuiya ya Wazazi Taifa iliopo  hapo Kikwajuni. (  Kulia ) Nd. Najma Murtaza Giga ambae ni Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi Taifa

Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi Taifa akimkaribisha katibu wa Idara ya Organaizesheni Zanzibar

Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi Taifa akimkabidhi Katibu huyo taarifa ya utekelezaji wa jumuiya ya Wazazi

KATIBU wa Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Organaizesheni Zanzibar  Nd. Bakari Hamad Khamis akitoa nasaha zake kwa Watumishi wa Jumuiya ya Wazazi

Alhamisi, 8 Machi 2018

KATIBU WA SUKI AWAFARIJI WAASISI WA CCM ZANZIBAR

Katibu wa Idara ya SUKI Zanzibar Nd. Kombo Hassan Juma Leo hii amewatembelea waasisi wa CCM Zanzibar na kuwafariji.
 Ambapo amewaelezea kuwa Chama cha Mapinduzi kipo pamoja nao.



 MKUU wa Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa CCM Zanzibar, Ndugu Kombo Hassan Juma akioneshwa picha  na Maalim Moh'd Ali mara tu Baada ya kuwasili hapo Nyumbani kwake



MKUU wa Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa CCM Zanzibar, Ndugu Kombo Hassan Juma (Kulia) akiwa nyumbani ( Magomeni - Zanzibar ) kwa Ndg. Said Kassim (katikati) ambae alikuwa Mtangazaji wa idhaa ya Redio Zanzibar

MKUU wa Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa CCM Zanzibar, Ndugu Kombo Hassan Juma akizungumza na Mwasisi wa CCM Bi. Johari Yussuf Akida mara tu baada ya kuwasili huko Chukwani ambako anaishi kwasasa mwasisi huyo.


Jumanne, 6 Machi 2018

KATIBU WA IDARA YA ORGANAZESHENI CCM Z'BAR ,BAKARI-AFANYA ZIARA MKOA WA KASKAZINI UNGUJA

 VIONGOZI  wa CCM Wilaya ya Kaskazini ‘A’ wakimkaribisha mgeni rasmi ambaye ni Katibu wa Kamti Maalum ya NEC, Idara ya organazesheni CCM Zanzibar ndugu Bakari Hamad Khamis katika ziara ya kujitambulisha kwa Secretarieti ya CCM ngazi za majimbo na Wilaya.

 BAADHI ya wajumbe wa Sekreterieti za majimbo na Wilaya ya Kaskazini ‘A’ wakimlaki mgeni rasmi mara baada ya kuwasili katika Ofisi ya Wilaya iliyopo Gamba Mkoa wa Kaskazini Unguja.

 KATIBU mwenezi CCM Wilaya kASKAZINI ''A'' Ali Chum Haji(kulia aliyesimama akizungumza), Katibu wa idara ya organazesheini CCM Zanzibar Bakar Hamad (katikati).

 Katibu wa Kamti Maalum ya NEC, Idara ya organazesheni CCM Zanzibar ndugu Bakari Hamad Khamis akizungumza na watendaji hao katika ziara ya kujitambulisha kwa Secretarieti ya CCM ngazi za majimbo na Wilaya ya Kaskazini ‘’A’’.

 KATIBU wa CCM Wilaya ya Kaskazini ‘’B’’ Ndugu Subira Mohamed Ameir (kulia) akizungumza baada ya mgeni rasmi kuwasili katika Wilaya hiyo kwa lengo la kujitambulisha.

 KATIBU wa Kamti Maalum ya NEC, Idara ya organazesheni CCM Zanzibar,ndugu Bakari Hamad Khamis  akizungumza na Kamati za Secretarieti ya CCM ngazi za majimbo na Wilaya.

BAADHI ya wajumbe wa Sekreterieti za majimbo na Wilaya ya Kaskazini ‘A’ wakimlaki wakisikiliza na kufuatilia nasaha za mgeni rasmi.
 KATIBU wa Kamti Maalum ya NEC, Idara ya organazesheni CCM Zanzibar ndugu Bakari Hamad Khamis akisisitiza umuhimu wa watendaji kuisoma na kuielewa Katiba ya CCM ya mwaka 1977.


NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR.


KATIBU wa  Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Organazesheni CCM Zanzibar ,Ndugu Bakari  Hamad Khamis amesema wanachama na watendaji wa CCM wanatakiwa kuandaa mipango endelevu ya kuhakikisha Chama kinashinda na kubaki madarakani katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.

Rai hiyo ameitoa katika ziara yake ya kujitambulisha kwa watendaji wa Chama na Jumuiya zake ambao ni wajumbe wa Sekreterieti za Wilaya na Majimbo ya CCM Mkoa wa Kaskazini Unguja, amesema Chama Cha Mapinduzi ili kishinde ni lazima maandalizi ya ushindi wake yaanze kwa sasa.

Alieleza kuwa pamoja na mambo mengine lengo la ziara hiyo ni kuwakumbusha watendaji hao majukumu yao ya msingi wanayotakiwa kuyafanyia kazi kabla ya uchaguzi mkuu ujao.

Amesema CCM ikiwa katika mfumo wa vyama vingi vya siasa ni lazima ifanye kazi kwa bidii ili kuleta mabadiliko chanya kwa wananchi wote bila ya ubaguzi.

Katibu huyo wa NEC ndugu Bakari, aliwambia Watendaji hao kuwa wanatakiwa kutumia uwezo wao wa kisiasa kuhakikisha baadhi ya majimbo yaliyopo katika mikono ya wapinzani yanarudi katika milki ya   Chama Cha Mapinduzi.  

“Dhana ya CCM mpya na Tanzania mpya sio upya wa kuwa ndio kimezaliwa leo bali ni kufanya kazi kwa bidii ili wananchi wanufaike na fursa zinazopatikana kwa serikali iliyotokana na Chama Cha Mapinduzi”, alisema Bakari.

Pia alisisitiza umuhimu wa viongozi na watendaji wa Chama na Serikali kutekeleza kwa wakati ahadi zilizotolewa katika kampeni za Uchaguzi uliopita kwa lengo la kumaliza madeni hayo ya kisiasa.

Aliwataka watendaji hao kusimamia utaratibu wa uimarishaji wa maskani za Chama hasa za vijana kwa lengo la kuongeza wanachama hai watakaofuata itikadi na siasa za CCM kwa vitendo.

Pia aliwaagiza Makatibu hao kuhakikisha wanaimarisha vikundi vya hamasa na burudani katika maeneo yao ili wanachama na wananchi kwa ujumla wapate sehemu ya kukutana mara kwa mara na kubadilishana mawazo.

Alisema  mabadiliko ya Katiba ya CCM ya mwaka 1977 yamebeba dhamira ya kuleta mageuzi ya kiutendaji kwa kila ngazi ya Chama na Jumuiya zake.

Sambamba na hayo amewataka baadhi ya watendaji wa ngazi za matawi hadi Mkoa wenye tabia za kutofungua Ofisi zao kwa wakati kuacha utamaduni huo na badala yake watekelezze wajibu wao ili wanachama wapate sehemu ya kuwasilisha changamoto zao.

Naye Katibu mwenezi Wilaya ya Kaskazini ‘A’  Ndugu Ali Chum Haji, alisema maelekezo yote yaliyotolewa na Katibu huyo wa Idara ya orgazanesheni yatafanyiwa kazi kwa wakati ili kwenda sambamba na siasa za maendeleo kwa jamii.

Kwa upande wake  Katibu wa CCM Wilaya ya Kaskazini ‘B’ Ndugu Subira Mohamed Ameir amesema Wilaya hiyo inakabiliwa na Changamoto mbali mbali za kijamii na kisiasa zinazotakiwa kutafutiwa ufumbuzi wa kudumu kupitia busara, hekima na uadilifu wa viongozi wakuu wa Chama na Serikali kabla ya uchaguzi Mkuu ujao.

Jumamosi, 3 Machi 2018

KATIBU MPYA WA IDARA YA SUK CCM Z'BAR AKABIDHIWA OFISI


 KATIBU mpya wa Idara hiyo Ndugu Kombo Hassan Juma akizungumza mara baada ya kukabidhiwa Ofisi ya Idara ya Siasa na uhusiano wa Kimataifa (SUK) CCM Zanzibar.

 KATIBU mstaafu wa Idara hiyo  Eng. Hamad Yussuf Masauni(kushoto)  akizungumza katika hafla hiyo ya makabidhiano, Katibu mpya wa Idara hiyo Ndugu Kombo Hassan Juma(kulia aliyekaa).

 MKUU wa Sehemu Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa CCM Zanzibar, Khamis Haji Khamis(kulia) akitoa ufafanuzi juu ya majukumu mbali mbali ya Idara katika hafla ya makabidhiano ya Ofisi kutoka kwa Katibu mstaafu wa Idara hiyo Hamad Yussuf Masauni na kumkabidhi Katibu mpya Maalim Kombo Hassan Juma.
 BAADHI ya Maafisa wa Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa(SUK) CCM Zanzibar. 
 Afisa wa Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa(SUK) CCM Zanzibar  Ndugu Mzee Khatib Abdallah akifuatilia kwa makabidhiano hayo.



NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR.

KATIBU wa Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa CCM Zanzibar, Ndugu Kombo Hassan Juma amesema ushindani wa kisiasa na mbinu za upinzani zinazidi kuongezeka hivyo Chama tawala ni lazima kiwe imara kukabiliana na mabadiliko yanayotokea katika uwanja wa kisiasa nchini.

Kauli hiyo ameitoa leo katika hafla fupi ya makabidhiano ya Ofisi ya Idara hiyo yaliyofanyika katika Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Zanzibar, amesema wanachama, viongozi na watendaji wa Chama Cha Mapinduzi wanatakiwa kubadilika na kuondokana na mazoea ya siasa za wakati  wa  mfumo wa chama kimoja na  badala yake waendane na siasa za ushindani.

Ameeleza kuwa ni lazima CCM iendelee kujifunza baadhi ya mbinu na mikakati ya kisiasa iliyopo katika vyama vingine vya kisiasa ili Chama kiweze kukabiliana na sera za vyama vyenye lengo la kukikondosha madarakani.

Katibu huyo mpya wa Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa ndugu Kombo alisema kazi kubwa ya CCM ni kusimamia viongozi mbali mbali wa Chama na Serikali waliopewa dhamana ya uongozi na wananchi wahakikishe wanatekeleza wajibu wao kwa ufanisi.

“ Tutaendelea kuikumbusha serikali mara kwa mara waendelee na kasi hiyo hiyo ya utekelezaji wa Ilani kwani ndio sehemu pekee ya mtaji wetu kisiasa ambao tunaamini ipo siku wananchi watahoji nini tumetekeleza katika maeneo yao”, amesema Ndugu Kombo.

Aidha Ngugu Kombo amemshukuru Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein kwa kumuamini kwa kumteuwa awe Mkuu wa Idara hiyo na kuongeza kuwa atafanya kazi kwa bidii ili CCM ishinde na kubaki madarakani katika uchaguzi Mkuu ujao.

Naye Katibu Mstaafu wa Idara hiyo Eng. Hamad Yussuf Masauni amesema ana imani kuwa idara hiyo ameikabidhi mikononi mwa Kiongozi makini mwenye uzoefu na weledi mkubwa ndani ya CCM na Serikali  kwa ujumla.

Amesema Idara hiyo ndio moyo wa Chama kwani ina dhamana ya kufuatilia hali ya kisiasa nchini pamoja na kuendeleza mahusiano mazuri na taasisi na wadau mbali mbali wa Kimataifa ili kukuza urafiki na ustawi wa kijamii baina ya Chama na taasisi hizo.

Hata hivyo amewasihi watendaji wa SUK Chama na Jumuiya kwa ujumla kumpa ushirikiano Katibu mpya ili kuimarisha shughuli za kisiasa na kiuchumi ndani na nje ya CCM.

Mapema Mkuu wa Sehemu katika Idara hiyo Ndugu Khamis Haji Khamis amesema makabidhiano hayo ni fursa kwa watendaji hao kutumia ujuzi na uzoefu wao katika kubuni mipango mbali mbali ya kiutendaji itakayoleta maendeleo ndani ya CCM.

Hafla hiyo imekuja mara baada ya Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein kuteuwa Wakuu wa Idara mbali mbali za Chama  ikiwemo Idara ya Siasa na uhusiano wa Kimataifa Zanzibar(SUK) ili waongoze idara hizo kwa miaka mitano ijayo.



DK.MABODI-AWATAKA WANANCHI KUJIUNGA NA VIKUNDI VYA UJASIRIA MALI

 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar akihutubia katika hafla ya maonyesho ya  wajasiriamali iliyofanyika huko Fuoni Skuli Zanzibar.

Naibu Katibu Mkuu CCM Zanzibar Dk.Mabodi awataka wajasiri wa Jimbo la Dimani kujinga na wajasiriamali kutoka sehemu mbali mbali za Dunia ili wapate ujuzi wa kutengeneza bidhaa bora zinazokubalika katika masoko ya biashara ya ndani na nje ya nchi.

Wito huo ameutoa leo wakati akizungumza na wajasiria mali hao huko Viwanja vya Skuli ya Fuoni  Unguja, amesema endapo wajasiriamali hao watatengeneza bidhaa bora watakuwa wamefungua fursa ya bidhaa zao kuongezeka thamani na kukunuliwa kwa wingi.


Amesema njia pekee ya kuongeza ubunifu katika utengenezaji wa bidhaa hizo kwa wajasiriamali hao ni kujifunza ubunifu kutoka kwa wenzao wenye uzoefu mkubwa wa utengenezaji wa bidhaa hizo kwa lengo la kujiongeza kibiashara na kuingiza kipato cha uhakika.

"Nimefurahi sana kuona baadhi ya bidhaa zetu za ndani zinawekwa katika vifungashio kwa kisasa na zinakuwa na muonekano mzuri ambao ni moja ya kivutio kikubwa katika masoko ya kimataifa",amewapongeza Wajasiriamali hao Dk.Mabodi.

Ameeleza kuwa huwezi kuzungumzia maendeleo katika nchi zilizostawi kiuchumi bila kutaja mchango wa Sekta ya ujasiriamali inayoingiza fedha nyingi kutoka katika mzunguko wa biashara na masoko.

Pamoja na hayo aliwambia wananchi kupitia hafla hiyo kuwa fursa hizo zinatokana na usimamizi mzuri wa Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015/2020 inayotekelezwa na Serikali zote mbili ya  Jamhuri ya Muungano inaongozwa na Dkt. Magufuli  na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ambayo inaongozwa na Dk. Ali Mohamed Shein .

 Amesema serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ina dhamira ya kuendelea kuimarisha ustawi wa vijana kwa kuwapatia mafunzo mbali mbali ya stadi za maisha ili wawe na ujuzi utakaowawezesha kujiajili wenyewe.

Pia ametoa wito kwa wananchi mbali mbali kuvisajili vikundi vyao kupitia utaratibu unaotambuliwa kisheria ili wanufaike  na huduma ya  mikopo yenye masharti nafuu  kupitia mfuko wa uwezeshaji.

Dk. Mabodi akisalimiana na Viongozi mbali mbali wa Chama na Serikali mara tu baada ya kuwasili katika Viwanja vya Skuli ya Msingi Fuoni kwa lengo la kukutana na wajasiriamali wa Jimbo la Dimani

Mbunge wa Dimani Ndg, Juma Ali Juma akimuonesha Dk. Mabodi moja ya bidhaa ambazo zinafanywa na
 wajasiriamali  wa Jimbo la Dimani

Dk. Mabodi akipata malezo kutoka kwa mmoja kati ya wakufunzi Ndg, Fuadi

Naibu akizidi kukagua bidhaa za wajasiriamali hao

Dk. Mabodi akipokea zawadi aliyotunukiwa na wajasiri amali hao kutoka Dimani

Dk. Mabodi akitizama kwa bashasha moja kati ya zawadi aliyotunukiwa na wajasiri amali hao kutoka Dimani

Dk. Mabodi akisalimiana na mmoja kati ya washirika wa maendeleo kutoka Canada

NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar akiwa katika picha ya pamoja na Wasiriamali na viongozi mbali mbali wa CCM Wilaya ya Dimani.