Jumamosi, 3 Machi 2018

DK.MABODI-AWATAKA WANANCHI KUJIUNGA NA VIKUNDI VYA UJASIRIA MALI

 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar akihutubia katika hafla ya maonyesho ya  wajasiriamali iliyofanyika huko Fuoni Skuli Zanzibar.

Naibu Katibu Mkuu CCM Zanzibar Dk.Mabodi awataka wajasiri wa Jimbo la Dimani kujinga na wajasiriamali kutoka sehemu mbali mbali za Dunia ili wapate ujuzi wa kutengeneza bidhaa bora zinazokubalika katika masoko ya biashara ya ndani na nje ya nchi.

Wito huo ameutoa leo wakati akizungumza na wajasiria mali hao huko Viwanja vya Skuli ya Fuoni  Unguja, amesema endapo wajasiriamali hao watatengeneza bidhaa bora watakuwa wamefungua fursa ya bidhaa zao kuongezeka thamani na kukunuliwa kwa wingi.


Amesema njia pekee ya kuongeza ubunifu katika utengenezaji wa bidhaa hizo kwa wajasiriamali hao ni kujifunza ubunifu kutoka kwa wenzao wenye uzoefu mkubwa wa utengenezaji wa bidhaa hizo kwa lengo la kujiongeza kibiashara na kuingiza kipato cha uhakika.

"Nimefurahi sana kuona baadhi ya bidhaa zetu za ndani zinawekwa katika vifungashio kwa kisasa na zinakuwa na muonekano mzuri ambao ni moja ya kivutio kikubwa katika masoko ya kimataifa",amewapongeza Wajasiriamali hao Dk.Mabodi.

Ameeleza kuwa huwezi kuzungumzia maendeleo katika nchi zilizostawi kiuchumi bila kutaja mchango wa Sekta ya ujasiriamali inayoingiza fedha nyingi kutoka katika mzunguko wa biashara na masoko.

Pamoja na hayo aliwambia wananchi kupitia hafla hiyo kuwa fursa hizo zinatokana na usimamizi mzuri wa Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015/2020 inayotekelezwa na Serikali zote mbili ya  Jamhuri ya Muungano inaongozwa na Dkt. Magufuli  na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ambayo inaongozwa na Dk. Ali Mohamed Shein .

 Amesema serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ina dhamira ya kuendelea kuimarisha ustawi wa vijana kwa kuwapatia mafunzo mbali mbali ya stadi za maisha ili wawe na ujuzi utakaowawezesha kujiajili wenyewe.

Pia ametoa wito kwa wananchi mbali mbali kuvisajili vikundi vyao kupitia utaratibu unaotambuliwa kisheria ili wanufaike  na huduma ya  mikopo yenye masharti nafuu  kupitia mfuko wa uwezeshaji.

Dk. Mabodi akisalimiana na Viongozi mbali mbali wa Chama na Serikali mara tu baada ya kuwasili katika Viwanja vya Skuli ya Msingi Fuoni kwa lengo la kukutana na wajasiriamali wa Jimbo la Dimani

Mbunge wa Dimani Ndg, Juma Ali Juma akimuonesha Dk. Mabodi moja ya bidhaa ambazo zinafanywa na
 wajasiriamali  wa Jimbo la Dimani

Dk. Mabodi akipata malezo kutoka kwa mmoja kati ya wakufunzi Ndg, Fuadi

Naibu akizidi kukagua bidhaa za wajasiriamali hao

Dk. Mabodi akipokea zawadi aliyotunukiwa na wajasiri amali hao kutoka Dimani

Dk. Mabodi akitizama kwa bashasha moja kati ya zawadi aliyotunukiwa na wajasiri amali hao kutoka Dimani

Dk. Mabodi akisalimiana na mmoja kati ya washirika wa maendeleo kutoka Canada

NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar akiwa katika picha ya pamoja na Wasiriamali na viongozi mbali mbali wa CCM Wilaya ya Dimani.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni