Alhamisi, 8 Oktoba 2020
DK.MWINYI- ATAKA WAWEKEZAJI WACHANGIE MAENDELEO
DK.MWINYI-ASEMA ATATATUA CHANGAMOTO ZA WAWEKEZAJI
MGOMBEA urais wa Zanzibar kupitia
Chama cha Mapinduzi (CCM), Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema akipata ridhaa ya
kuiongoza Zanzibar, ataweka misingi imara kwa wafanyabiashara ili wafanye
biashara zitakazoleta tija nchini.
Dk.
Mwinyi alisema hayo alipokuwa akizungumza na wafanyabiashara kusikiliza
changamoto zinazowakabili ikiwa ni mwendelezo wa kampeni za mgombea huyo,
mkutano uliofanyika katika hoteli ya Golden Tulip, Malindi.
Alisema
sekta biashara ni muhimu katika kukuza uchumi wa nchi na kuongeza pato la taifa
hivyo atahakikisha anafungua milango ili wafanyabiashara waitumie kuimarisha
mifumo ya biashara.
Dk.
Mwinyi alisema ni vyema kwa wafanyabiashara wa ndani kuwa tayari kuitumia
milango hiyo kwa kufanya biashara kubwa ndani ya nchi na kutokaa pembeni kupoteza
fursa zitakazojitokeza.
“Ninagombea
nafasi hii, kwa lengo la kuwatumikia wananchi na wafanyabiashara ni sehemu
muhimu ya wananchi hivyo ninawaomba mjipanga vyema tukashirikiane na kwenda
sambamba na matakwa ya wanachi wetu,” alieleza Dk. Mwinyi.
Alisema
ili kufikia azma hiyo, serikali atakayoiongoza itashirikiana na jumuiya za
wafanyabiashara na kuangalia sheria, kanuni, masuala ya kodi na ukataji wa
leseni za biashara ili kuondoa vikwazo katika shughuli za biashara na viwanda
nchini.
Akizungumzia
sekta ya utalii, Dk. Mwinyi alisema ataiendeleza ili kuinua kiwango cha idadi
ya watalii wanaoingia nchini lakini pia kuongeza thamani na aina za utalii kama
njia moja wapo ya kuongeza mapato yanayotokana na sekta hiyo.
Alisema
pamoja na Zanzibar kuendelea kuwa sekta kiongozi katika kuchangia pato la
taifa, bado inapaswa kutangaza vivutio ilivyonavyo zikiwemo fukwe na kwa
kuwekewa mipango madhubuti itakayowavutia watalii kuongezeka.
Kwa
upande wa maendeleo ya viwanda, Dk. Mwinyi alisema sekta hiyo inahitaji mapinduzi
makubwa ili isaidia ustawi wa wananchi wote wakiwemo wawekezaji wazawa kuwekeza
kupitia sekta hiyo.
“Sekta
ya viwanda itakapoimarika, wakulima na wafanyabiashara wadogo wataweza kutumia
viwanda kwa kazi tofauti ili zilete tija kwao na taifa kwa ujumla,” aliemeza
Dk. Mwinyi.
Mapema
Akiwazungumza katika mkutano huyo, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara
Zanzibar (ZNCC), Ally Amour, alisema serikali ya awamu ya saba imefanya mengi
kwa wafanyabiashara hali ambayo imepelekea kwa kiasi kikubwa kukua kwa uchumi
wa nchi.
Alisema
ni vyema anapoingia madarakani kiongozi huyo kusaidia kutayarisha mazingira
mazuri ya biashara ili nchi iweze kusonga mbele zaidi kimaendeleo.
Baadhi
ya washiriki wa mkutano huo, walimuomba kiongozi huyo kuzipa kipaumbele baadhi ya
changamoto zilizobakia hususani kupitia sekta ya kilimo kwa kukipa kipaumbele
kilimo cha umwagiliaji maji ili kuongeza uzalishaji utakaokidhi mahitaji ya
ndani chakula.
Mbali na hayo walimuomba akiingia
madarakani kulipatia ufumbuzi tatizo ufungaji wa maduka ya kubadilisha fedha za
kigeni ya watu binafsi kwani imechangia kuvuruga mfumo wa maisha na biashara za
baadhi nya wafanyabiashara wanaofanya shughuli hizo.
DK.HUSSEIN-AZUNGUMZA NA WAFANYABIASHARA
MGOMBEA urais wa Zanzibar kupitia
Chama cha Mapinduzi (CCM), Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema akipata ridhaa ya
kuiongoza Zanzibar, ataweka misingi imara kwa wafanyabiashara ili wafanye
biashara zitakazoleta tija nchini.
Dk.
Mwinyi alisema hayo alipokuwa akizungumza na wafanyabiashara kusikiliza
changamoto zinazowakabili ikiwa ni mwendelezo wa kampeni za mgombea huyo,
mkutano uliofanyika katika hoteli ya Golden Tulip, Malindi.
Alisema
sekta biashara ni muhimu katika kukuza uchumi wa nchi na kuongeza pato la taifa
hivyo atahakikisha anafungua milango ili wafanyabiashara waitumie kuimarisha
mifumo ya biashara.
Dk.
Mwinyi alisema ni vyema kwa wafanyabiashara wa ndani kuwa tayari kuitumia
milango hiyo kwa kufanya biashara kubwa ndani ya nchi na kutokaa pembeni kupoteza
fursa zitakazojitokeza.
“Ninagombea
nafasi hii, kwa lengo la kuwatumikia wananchi na wafanyabiashara ni sehemu
muhimu ya wananchi hivyo ninawaomba mjipanga vyema tukashirikiane na kwenda
sambamba na matakwa ya wanachi wetu,” alieleza Dk. Mwinyi.
Alisema
ili kufikia azma hiyo, serikali atakayoiongoza itashirikiana na jumuiya za
wafanyabiashara na kuangalia sheria, kanuni, masuala ya kodi na ukataji wa
leseni za biashara ili kuondoa vikwazo katika shughuli za biashara na viwanda
nchini.
Akizungumzia
sekta ya utalii, Dk. Mwinyi alisema ataiendeleza ili kuinua kiwango cha idadi
ya watalii wanaoingia nchini lakini pia kuongeza thamani na aina za utalii kama
njia moja wapo ya kuongeza mapato yanayotokana na sekta hiyo.
Alisema
pamoja na Zanzibar kuendelea kuwa sekta kiongozi katika kuchangia pato la
taifa, bado inapaswa kutangaza vivutio ilivyonavyo zikiwemo fukwe na kwa
kuwekewa mipango madhubuti itakayowavutia watalii kuongezeka.
Kwa
upande wa maendeleo ya viwanda, Dk. Mwinyi alisema sekta hiyo inahitaji mapinduzi
makubwa ili isaidia ustawi wa wananchi wote wakiwemo wawekezaji wazawa kuwekeza
kupitia sekta hiyo.
“Sekta
ya viwanda itakapoimarika, wakulima na wafanyabiashara wadogo wataweza kutumia
viwanda kwa kazi tofauti ili zilete tija kwao na taifa kwa ujumla,” aliemeza
Dk. Mwinyi.
Mapema
Akiwazungumza katika mkutano huyo, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara
Zanzibar (ZNCC), Ally Amour, alisema serikali ya awamu ya saba imefanya mengi
kwa wafanyabiashara hali ambayo imepelekea kwa kiasi kikubwa kukua kwa uchumi
wa nchi.
Alisema
ni vyema anapoingia madarakani kiongozi huyo kusaidia kutayarisha mazingira
mazuri ya biashara ili nchi iweze kusonga mbele zaidi kimaendeleo.
Baadhi
ya washiriki wa mkutano huo, walimuomba kiongozi huyo kuzipa kipaumbele baadhi ya
changamoto zilizobakia hususani kupitia sekta ya kilimo kwa kukipa kipaumbele
kilimo cha umwagiliaji maji ili kuongeza uzalishaji utakaokidhi mahitaji ya
ndani chakula.
Mbali na hayo walimuomba akiingia
madarakani kulipatia ufumbuzi tatizo ufungaji wa maduka ya kubadilisha fedha za
kigeni ya watu binafsi kwani imechangia kuvuruga mfumo wa maisha na biashara za
baadhi nya wafanyabiashara wanaofanya shughuli hizo.
DK.MWINYI -AWEKA WAZI NEEMA KWA WANANCHI WA KASKAZI 'B' UNGUJA
Jumatano, 7 Oktoba 2020
KUMEKUCHA BUMBWINI, DK.MWINYI KUMWAGA SERA, DK.SHEIN KUWATAMBULISHA WAGOMBEA.
BAADHI ya Vijana wa Chama Cha Mapinduzi wa kundi la hamasa wakiburudisha kwa kuimba nyimbo mbalimbali katika mkutano huo wa kampeni za CCM. |
VIONGOZI mbalimbali wa Chama Cha Mapinduzi wakiwa wamekaa jukwaa kuu wakisubiri mgeni rasmi awasili kwa lengo la kuanza kwa mkutano huo wa kampeni za CCM. |
MAELFU ya Wana CCM na wananchi kwa ujumla wamejitokeza kwa wingi katika viwanja vya skuli ya Bumbwini kwa ajili ya kuhudhuria mkutano wa kampeni za CCM za kuwanadi,kuwatambulisha na kuwaombea kura za ndio wagombea wa CCM kwa ngazi za Urais wa Zanzibar na jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wabunge, Wawakilishi,madiwani na wagombea kupitia viti maalum.
Mkutano huo ni miongoni mwa mwendelezo wa kampeni za CCM zinazofanyika nchini na kuhudhuriwa na wananchi wengi.
Kupitia mkutano huo mgeni rasmi ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar ambaye pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, atawatambulisha na kuwaombea kura za ndio wagombea wote wa CCM.
Pia Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM Dk.Hussein Ali Mwinyi ataomba kura na kueleza kwa kina sera na vipaumbele vyake ili wananchi wa wilaya ya kaskazini 'B' wafanye maamuzi sahihi ya kuchagua wagombea wanaotoka katika chama chenye sera zinazotekelezeka.
tutaendelea kupata taarifa mbalimbali kupitia blog hii,,,,,,
Imeandaliwa na Kitengo cha Habari Afisi Kuu CCM Zanzibar.
Jumatano, 15 Julai 2020
MAELFU YA WANA CCM WAMPOKEA DK.HUSSEIN MWINYI ZANZIBAR.
MAELFU ya Wana CCM wakiwa katika msafara wa mapokezi ya Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM Dk.Hussein Ali Hassan Mwinyi kutoka uwanja wa ndege wa kimataifa wa Zanzibar. |
Jumamosi, 4 Julai 2020
KAMATI MAALUM Z'BAR YAPENDEKEZA MAJINA MATANO YA MAKADA WANAOWANIA URAIS
KAMATI Maalum ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) Taifa Zanzibar leo imependekeza majina matano ya makada wa CCM waliojitokeza kuchukua fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea nafasi ya Urais wa Zanzibar kati ya makada 31.
Akizungumza na Waandishi wa Habari Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi, alisema kamati hiyo ni sehemu muhimu ya maandalizi na uchujaji wa majina ya wagombea watano wanaotakiwa kuwasilishwa katika Kamati Kuu kwa ajili ya kujadiliwa tena na kumtafuta mgombea mzuri mwenye sifa 12 zikiwemo hekima,kuaminika,kuthamini muungano na Mapinduzi ya Zanzibar.
Dk.Mabodi alisema baada ya Kamati kuu kujadili kwa kina majina hayo matano itapendekeza majina matatu na kuyapeleka Halmashauri Kuu ya CCM Taifa ambayo itachagua jina la mtu mmoja ambaye atapeperusha bendera ya CCM kwa nafasi ya Urais wa Zanzibar.
Alisema kuwa baada ya hatua hiyo mgombea huyo atapelekwa katika Mkutano Mkuu wa CCM kwa ajili ya kudhibitishwa na kupata baraka za Wajumbe wote wa kamati kuu na kuendelea na michakato mingine.
Dk.Mabodi, alisema baada ya kukamilika kwa mchakato huo itaendelea awamu ya pili ya uchukuaji wa fomu kwa nafasi za Ubunge, uwakilishi na Udiwani na kufuata utaratibu wa miongozo ya CCM.
Katika maelezo yake Naibu Katibu Mkuu huyo, amewasifu viongozi kwa ukomavu wao wa kisiasa Kwa kufuata Katiba,miongozo na Kanuni za CCM kwa kutobeba wagombea mifukoni.
Alisema kuwa kikao hicho kimesisitiza usiri kwa wagombea hao kwani ndani ya Chama ikibainika miongoni mwao kuna mtu kakiuka utaratibu anaweza kuondolewa na kuchaguliwa mtu mwingine.
"Lazima tuenzi siri za vikao hivyo ni muhimu sana watu wote kuheshimu maamuzi ya vikao na kufuata utaratibu uliowekwa ndani ya CCM," alisema Dk.Mabodi.
Mchakato wa kuchukua na kurejesha fomu ulianza Juni 15 hadi 30, mwaka huu ambapo jumla ya makada 32 walijitokeza kuchukua fomu hiyo ambao ni Mbwana Bakari Juma, Ali Abeid Karume,Mbwana Yahya Mwinyi,Omar Sheha Mussa,Hussein Ali Mwinyi,Shamsi Vuai Nahodha,Mohamed Jafar Jumanne Mohamed Hijja Mohamed,Issa Suleiman Nassor.
Wengine ni Prof.Makame Mnyaa Mbarawa,Mwatum Mussa Sultan,Haji Rashid Pandu,Abdulhalim Mohamed Ali,Jecha Salum Jecha,Dk.Khalid Salum Mohamed,Rashid Ali Juma,Khamis Mussa Omar,Mmanga Mjengo Mjawiri,Hamad Yussuf Masauni Mohamed Aboud Mohamed, Bakari Rashid Bakar,Mgeni Hassan Juma, Ayoub Mohamed Mahmoud,Hashim Salum Hashim,Fatma Kombo Masoud,Hasna Attai Masoud, Maalim Hamad Idd Hamad Idd,Pereira Ame Silima,Shaame Mcha,Mussa Aboud Jumbe na Moudline Cyrus Castico.
Jumanne, 30 Juni 2020
MHE.SAMIA AANZA ZIARA YA KUIMARISHA CHAMA KUSINI UNGUJA.
WAJUMBE
wa Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa kusini Unguja,wakifuatilia maelekezo
yanayotolewa na mgeni rasmi Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Mhe.Samia Suluhu
Hassan. |
Jumatano, 24 Juni 2020
FATMA KOMBO ACHUKUA FOMU YA KUOMBA RIDHAA YA URAIS WA ZANZIBAR.
HASNA ATTAI ACHUKUA FOMU YA URAIS ZANZIBAR
Jumanne, 23 Juni 2020
MWANAMICHEZO HASHIM SALUM ACHUKUA FOMU YA KUWANIA URAIS WA ZANZIBAR.
KADA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Hashim Salum Hashim leo amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea Urais wa Zanzibar kupitia CCM.
MOHAMED HIJA AREJESHA FOMU YA KUOMBA URAIS
RASHID, MASAUNI,RC AYOUB NA BHAA NAO WAJITOSA MBIO ZA URAIS ZNZ
MAKADA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakiwemo mawaziri wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni baadhi ya wanachama waliochukua fomu, kuomba ridhaa ya kupeperusha bendera ya CCM katika nafasi ya urais wa Zanzibar.
Mwingine aliyechukua fomu ya CCM kuwania urais wa Zanzibar ni Hussein Ibrahim Makungu maarufu kama ‘’Bhaa’’.