Alhamisi, 8 Oktoba 2020

DK.MWINYI- ATAKA WAWEKEZAJI WACHANGIE MAENDELEO



MGOMBEA Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM amesema endapo atapewa ridhaa ya kuwa rais wa zanzibar,atahakikisha wawekezaji wanachangia maendeleo ya jamii inayowazuka.

 Alisema katika utawala wake ni lazima kila mwekezaji anachangia maendeleo ya kijamii kwa kujenga shule,hospitali na miundombinu ya maji safi na salama. 

 Kauli hiyo ameitoa wakati akizungumza na makundi mbalimbali ya kijamii ya wafanyabiashara wadogowadogo wakiwemo mama lishe,walinzi wa mahoteli, wavuvi na wafanyabisha za maduka ya vileo katika Kijiji cha Kiwengwa Wilaya ya Kaskazini "B" Unguja. 

 Dk.Mwinyi, alisema haiwezekani wawekezaji wanufaike na rasilimali za nchi huku wenyeji wakibaki katika lindi la umaskini. 

 "Sekta ya utalii ni muhimu kwa maendeleo ya nchi yetu, hivyo ni lazima matokeo ya uwepo wa sekta hiyo yaonekane kuanzia kwa jamii zilizopo katika ukanda wa utalii ziwe na miundombinu bora na rafiki ya kijamii. 

 sio dhambi wawekezaji kusaidia maendeleo katika maeneo waliyowekeza japokuwa wapo baadhi wanatoa wanaotoa michango yao lakini wengi bado hawajahamasika",alisema Dk.Mwinyi.

 Akizungumzia suala la ajira kwa walinzi wa mahoteli Dk.Mwinyi, alisema atahakikisha watu hao wanapatiwa mikataba inayozingatia haki na maslahi yao pindi wanapomaliza mikataba hiyo ama kustaafu.

 Aidha,akizungumzia suala la Kodi na leseni kwa wafanyabiashara ndogondogo,alifafanua kuwa atahakikisha panatengenezwa mfumo mmoja wa ulipaji wa kodi kulingana na kipato cha mfanyabiashara sambamba na kupatiwa kipambulisho maalum kitakacholipiwa kila mwaka.

 "Nimeambiwa tayari serikali imeanza mchakato wa kutoa vitambulisho kwa kila mfanyabiashara na kuweka kiwango maalum cha ulipaji wa Kodi ambacho kitaondosha kero hiyo.",alisema Dk.Mwinyi.

 Akijibu hoja za wananchi Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM Dk.Hussein Ali Mwinyi,alisema lengo la ziara hiyo ni kusikiliza changamoto za wafanyabiashara wadogo wadogo.

 Alisema kero za wafanyabiashara amezisikia hasa kuhusu suala la Kodi hivyo amesema kuwa akipata ridhaa naa kuwa rais suala Hilo atalitafutia ufumbuzi. 

 Alisema lengo la kugombea nafasi ya Urais wa Zanzibar ni kuhakikisha kila mwananchi anapata haki na kudhibiti vitendo vyote vya dhuruma. 

 Aliwambia wananchi hao kuwa katika utawala wake hatoruhusu vitendo vya uvunjaji wa sheria kwa wananchi vinavyosadikiwa kufanywa na viongozi ama watendaji wa serikali. 

 Alisema vitendo vya ubaguzi hatoruhusu viendelee kwani wananchi wa Tanzania ni wamoja na kwamba ubaguzi ni adui wa maendeleo. 

 Akizungumzia wajasiriamali alisema katika serikali yake watapatiwa mafunzo,watapewa mikopo na mitaji ya masharti nafuu na kuwatafutia masoko ya uhakika. 

 Dk.Mwinyi, akizungumza na waendesha pikipiki wa wilaya hiyo(bodaboda), aliwambia atahakikisha wanatambuliwa kisheria,kupewa mikopo ya masharti nafuu na kupatiwa huduma ya bima ya Afya ili pindi wanapopata ajali wawe na uhakika wa kupata matibabu.

 Katika maelezo yake Dk.Hussein,alisema suala la uvuvi wa kisasa ni sehemu ya ajenda ya serikali ijayo kupitia mfumo wa uchumi wa blue(blue economy), kwa kufanya uvuvi wa kisasa mpaka ufugaji wa samaki sambamba na kuwawezesha nyenzo za kisasa za uvuvi.

 Aliwambia wajasiriamali wa kuanika na kuuza dagaa kuwa atatatua changamoto zao kwa kuwawekea miundombinu rafiki katika utendaji wa kazi zao za kila siku.

 Pia alikemea tabia ya rushwa kwa baadhi ya watendaji wa halmashauri ya wilaya hiyo wanaotuhumiwa na kujihusisha na rushwa. 

 Alitumia nafasi hiyo kuomba kura na kuwaombea wagombea wote wa CCM kura za ndio ifikapo octobar 20, mwaka huu ili Chama kiendelee kuongoza dola. 

 Mama lishe Zainab Hussein,amesema wanakabiliwa na changamoto ya Halmashauri kuwatoza fedha nyingi ambazo ni shilingi 5000 kwa mwezi. 

 Alisema kila mwaka wanalipa shilingi 10,000 kwa leseni,wahudumu wa migahawa wanapimwa Afya kwa gharama za shilingi 60,000. 

 kwa upande wa Mama lishe Zuwena Kassim, wanakabiliwa na changamoto ya upungufu wa maji safi na salama kwa zaidi ya miaka 20. 

 Alisema wanakabiliwa na changamoto ya kuwa vibarua bila kupewa mikataba ya kulinda maslahi yao na kukosa michango ya kuweka katika mfuko wa hifadhi ya jamii Zanzibar (ZSSF) na kiinua mgongo.

 "Tunabaguliwa sana sisi jamii ya wamasai Kama vile sio binadamu Kama walivyo wengine tunaomba sana ukiwa rais uweke mazingira ya kulinda haki zetu,''alisema john. 

 Alisema kuwa katika eneo la Kiwengwa maeneo mengi hayana vyoo Jambo ambalo ni hatari kiafya.

 Alisema kuwepo kwa utalii ni Jambo Jema lakini wengine wanauza hadi chakula cha mama lishe na wengine kufanya kazi ambazo wenyeji wanaweza kufanya.

 Katibu wa jumuiya ya waanika dagaa Saleh Khatib Makame, kuwa na eneo maalum la godown,kujengewa ofisi ya jumuiya ya waanika dagaa na kupunguziwa Kodi na Halmashauri ya wilaya hiyo.

DK.MWINYI-ASEMA ATATATUA CHANGAMOTO ZA WAWEKEZAJI

 


MGOMBEA urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema akipata ridhaa ya kuiongoza Zanzibar, ataweka misingi imara kwa wafanyabiashara ili wafanye biashara zitakazoleta tija nchini.

Dk. Mwinyi alisema hayo alipokuwa akizungumza na wafanyabiashara kusikiliza changamoto zinazowakabili ikiwa ni mwendelezo wa kampeni za mgombea huyo, mkutano uliofanyika katika hoteli ya Golden Tulip, Malindi.

Alisema sekta biashara ni muhimu katika kukuza uchumi wa nchi na kuongeza pato la taifa hivyo atahakikisha anafungua milango ili wafanyabiashara waitumie kuimarisha mifumo ya biashara.

Dk. Mwinyi alisema ni vyema kwa wafanyabiashara wa ndani kuwa tayari kuitumia milango hiyo kwa kufanya biashara kubwa ndani ya nchi na kutokaa pembeni kupoteza fursa zitakazojitokeza.

“Ninagombea nafasi hii, kwa lengo la kuwatumikia wananchi na wafanyabiashara ni sehemu muhimu ya wananchi hivyo ninawaomba mjipanga vyema tukashirikiane na kwenda sambamba na matakwa ya wanachi wetu,” alieleza Dk. Mwinyi.

Alisema ili kufikia azma hiyo, serikali atakayoiongoza itashirikiana na jumuiya za wafanyabiashara na kuangalia sheria, kanuni, masuala ya kodi na ukataji wa leseni za biashara ili kuondoa vikwazo katika shughuli za biashara na viwanda nchini.

Akizungumzia sekta ya utalii, Dk. Mwinyi alisema ataiendeleza ili kuinua kiwango cha idadi ya watalii wanaoingia nchini lakini pia kuongeza thamani na aina za utalii kama njia moja wapo ya kuongeza mapato yanayotokana na sekta hiyo.

Alisema pamoja na Zanzibar kuendelea kuwa sekta kiongozi katika kuchangia pato la taifa, bado inapaswa kutangaza vivutio ilivyonavyo zikiwemo fukwe na kwa kuwekewa mipango madhubuti itakayowavutia watalii kuongezeka.

Kwa upande wa maendeleo ya viwanda, Dk. Mwinyi alisema sekta hiyo inahitaji mapinduzi makubwa ili isaidia ustawi wa wananchi wote wakiwemo wawekezaji wazawa kuwekeza kupitia sekta hiyo.

“Sekta ya viwanda itakapoimarika, wakulima na wafanyabiashara wadogo wataweza kutumia viwanda kwa kazi tofauti ili zilete tija kwao na taifa kwa ujumla,” aliemeza Dk. Mwinyi.

Mapema Akiwazungumza katika mkutano huyo, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Zanzibar (ZNCC), Ally Amour, alisema serikali ya awamu ya saba imefanya mengi kwa wafanyabiashara hali ambayo imepelekea kwa kiasi kikubwa kukua kwa uchumi wa nchi.

Alisema ni vyema anapoingia madarakani kiongozi huyo kusaidia kutayarisha mazingira mazuri ya biashara ili nchi iweze kusonga mbele zaidi kimaendeleo.

Baadhi ya washiriki wa mkutano huo, walimuomba kiongozi huyo kuzipa kipaumbele baadhi ya changamoto zilizobakia hususani kupitia sekta ya kilimo kwa kukipa kipaumbele kilimo cha umwagiliaji maji ili kuongeza uzalishaji utakaokidhi mahitaji ya ndani chakula.

Mbali na hayo walimuomba akiingia madarakani kulipatia ufumbuzi tatizo ufungaji wa maduka ya kubadilisha fedha za kigeni ya watu binafsi kwani imechangia kuvuruga mfumo wa maisha na biashara za baadhi nya wafanyabiashara wanaofanya shughuli hizo.


DK.HUSSEIN-AZUNGUMZA NA WAFANYABIASHARA

 


MGOMBEA urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema akipata ridhaa ya kuiongoza Zanzibar, ataweka misingi imara kwa wafanyabiashara ili wafanye biashara zitakazoleta tija nchini.

Dk. Mwinyi alisema hayo alipokuwa akizungumza na wafanyabiashara kusikiliza changamoto zinazowakabili ikiwa ni mwendelezo wa kampeni za mgombea huyo, mkutano uliofanyika katika hoteli ya Golden Tulip, Malindi.

Alisema sekta biashara ni muhimu katika kukuza uchumi wa nchi na kuongeza pato la taifa hivyo atahakikisha anafungua milango ili wafanyabiashara waitumie kuimarisha mifumo ya biashara.

Dk. Mwinyi alisema ni vyema kwa wafanyabiashara wa ndani kuwa tayari kuitumia milango hiyo kwa kufanya biashara kubwa ndani ya nchi na kutokaa pembeni kupoteza fursa zitakazojitokeza.

“Ninagombea nafasi hii, kwa lengo la kuwatumikia wananchi na wafanyabiashara ni sehemu muhimu ya wananchi hivyo ninawaomba mjipanga vyema tukashirikiane na kwenda sambamba na matakwa ya wanachi wetu,” alieleza Dk. Mwinyi.

Alisema ili kufikia azma hiyo, serikali atakayoiongoza itashirikiana na jumuiya za wafanyabiashara na kuangalia sheria, kanuni, masuala ya kodi na ukataji wa leseni za biashara ili kuondoa vikwazo katika shughuli za biashara na viwanda nchini.

Akizungumzia sekta ya utalii, Dk. Mwinyi alisema ataiendeleza ili kuinua kiwango cha idadi ya watalii wanaoingia nchini lakini pia kuongeza thamani na aina za utalii kama njia moja wapo ya kuongeza mapato yanayotokana na sekta hiyo.

Alisema pamoja na Zanzibar kuendelea kuwa sekta kiongozi katika kuchangia pato la taifa, bado inapaswa kutangaza vivutio ilivyonavyo zikiwemo fukwe na kwa kuwekewa mipango madhubuti itakayowavutia watalii kuongezeka.

Kwa upande wa maendeleo ya viwanda, Dk. Mwinyi alisema sekta hiyo inahitaji mapinduzi makubwa ili isaidia ustawi wa wananchi wote wakiwemo wawekezaji wazawa kuwekeza kupitia sekta hiyo.

“Sekta ya viwanda itakapoimarika, wakulima na wafanyabiashara wadogo wataweza kutumia viwanda kwa kazi tofauti ili zilete tija kwao na taifa kwa ujumla,” aliemeza Dk. Mwinyi.

Mapema Akiwazungumza katika mkutano huyo, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Zanzibar (ZNCC), Ally Amour, alisema serikali ya awamu ya saba imefanya mengi kwa wafanyabiashara hali ambayo imepelekea kwa kiasi kikubwa kukua kwa uchumi wa nchi.

Alisema ni vyema anapoingia madarakani kiongozi huyo kusaidia kutayarisha mazingira mazuri ya biashara ili nchi iweze kusonga mbele zaidi kimaendeleo.

Baadhi ya washiriki wa mkutano huo, walimuomba kiongozi huyo kuzipa kipaumbele baadhi ya changamoto zilizobakia hususani kupitia sekta ya kilimo kwa kukipa kipaumbele kilimo cha umwagiliaji maji ili kuongeza uzalishaji utakaokidhi mahitaji ya ndani chakula.

Mbali na hayo walimuomba akiingia madarakani kulipatia ufumbuzi tatizo ufungaji wa maduka ya kubadilisha fedha za kigeni ya watu binafsi kwani imechangia kuvuruga mfumo wa maisha na biashara za baadhi nya wafanyabiashara wanaofanya shughuli hizo.



DK.MWINYI -AWEKA WAZI NEEMA KWA WANANCHI WA KASKAZI 'B' UNGUJA



MGOMBEA Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM Dk.Hussein Ali Mwinyi, amesema endapo atakuwa rais wa Zanzibar atahakikisha anajenga bandari mpya ya kisasa ya mafuta na gesi asililia ili kukuza uchumi wa nchi. 

 Alisema ujenzi wa bandari hiyo hautoathiri shughuli za wananchi hasa wanaojishughulisha na uvuvi katika maeneo ya wilaya hiyo. 

Ahadi hiyo ameitoa katika mwendelezo wa mikutano ya kampeni za CCM katika wilaya ya Kaskazini ‘B’ huko katika skuli ya bumbwini Wilaya ya kaskazini ‘B’ Unguja.

 Alisema bandari hiyo ikikamilika itakuwa ndio kitovu cha uchumi wa nchi kwani itasaidia kutoa ajira nyingi.

 Aidha, alisema atavipa kipaumbele vikundi vya ujasiriamali kwa kuvipatia mikopo na mafunzo ili wanufaike na fursa hizo. 

 Alisema atahakikisha wananchi wa wilaya hiyo wananufaika na ufugaji wa kisasa wa samaki ili waende sambamba na dhana ya uchumi.

 Pia alijiombea kura na kuwaombea kura wagombea wote wa CCM ili CCM iendelee kuongoza dola.

Pamoja na hayo aliwataka wananchi walinde amani ya nchi na wasikubali kuchokozeka na vitendo vinavyofanywa na baadhi ya wapinzani.

Alisema atajenga hospitali ya wilaya,kununua vifaa tiba vya kisasa na kuajiri wafanyakazi wa sekta ya afya ili huduma zitakazotolewa zikidhi mahitaji ya wakaazi wa wilaya ya kaskazini ‘B’ Unguja. 

 Pia ameahidi kujenga barabara ya bumbwini hadi mahonda ili kukuza uchumi wa wananchi wa maeneo hayo.

 Aidha alisema watajenga skuli ya ghorofa na daharia pamoja na kuthibiti changamoto ya wizi wa mifugo ili wananchi wanufaike na fursa za ufugaji.

 Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar ambaye pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, alisema historia ya Zanzibar imeanzia mbali kwani toka utawala wa wareno na waoman.  

Dk.Shein, alisema toka mwa 1957 zilifanyika chaguzi mbalimbali lakini wazawa hawakuwahi kushinda uchaguzi huo kutokana na kuwepo kwa njama za ukandamizaji.

 Alisema baada ya utawala wa ukandamizaji wa wakati huo,Wazee wa kiafrika chini ya uongozi wa marehemu Abeid Amani Karume wakaamua kuondosha utawala huo kupitia mapinduzi ya mwaka 1964.

 Dk.Shein, alisema baada ya mapinduzi hayo nchi ilikuwa huru na kuweka viongozi kwa awamu mbalimbali toka awamu ya kwanza mpaka hivi sasa tunaelekea awamu ya nane.

 Alisema kuna baadhi ya viongozi wa kisiasa wanajifanya hawatambui mapinduzi kutokana na sababu zao za kisiasa. 

Alisema kwa sasa nchi ipo katika harakati za uchaguzi hivyo wananchi, wasikubali kuongozwa na watu wabaguzi wa kidini.kikabila na kisiasa. 

Alieleza kuwa CCM imemteua Dk.Mwinyi kwa kuwa ana sifa zinazokubalika ndani ya jamii yake sambamba na kuwa na sifa za ziada za kuwa mpole,mvumilifu,mcheshi,mcha mungu na mwadilifu.

 Alisema Dk.Hussein, ana sifa nyingine tofauti na wagombea wengine mwani ana uzoefu wa kiutendaji ndani ya serikali na ni msomi wa fani ya udaktari. 

 Alieleza kuwa CCM imemkabidhi Dk.Mwinyi, bendera na ilani ya uchaguzi ya mwaka 2020/2025 ili vimuongoze katika kusimamia maslahi ya CCM. 

Dk.Shein, alisema ushindi wa CCM wa mwaka huu ni mkubwa ambao utakuwa ni wa kihistoria katika siasa za afrika mashariki kwani CCM imejipanga vizuri kuhakikisha inashindwa kwa njia za kidemokradsia. 

Alisema hakuna njia ya mkatoa ya kuingia ikulu na kwamba ni lazima chama kishinde kupitia uchaguzi huru na wa haki. 

Alieleza kuwa kwa mara ya kwanza Zanzibar itaendesha uchaguzi kwa fedha zake za ndani bila ya kutegemea ufadhili, hatua ambayo ni kubwa kimaendeleo.

Pamoja na hayo aliwaombea kura za ndio wagombea wote wa CCM wakiwemo wagombea wa nafasi za Urais,wabunge,wawakilishi na madiwani.

Naye Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla, alisema kuwa CCM imetekeleza ilani yake kwa zaidi ya asilimia 100 kwa kuwafikishia wananchi huduma zote za msingi.

Alisema Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Shein, aliasisi mfumo wa kupunguza masafa baina ya chama na serikali kwa kwa kufuatana na viongozi wa CCM kila anapofanya ziara zake za kikazi.

Alisema CCM inaendelea kufanya kampani zake za kisayansi za kuwafuata wananchi katika maeneo yao na kuwaeleza sera zake na namna kitakavyotekeleza miradi mipya ya maendeleo kwa maslahi ya wananchi wote. 

“ Tumetekeleza kwa kiwango kikubwa ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015/2020 na mengine mazuri yamo katika ilani mpya ya uchaguzi ya mwaka 2020/2025”, alisema Dk.Mabodi. 

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Kaskazini Unguja ,Idd Ali Ame alisema wananchi wa mkoa huo wanamshukru Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, kwa utekelezaji mzuri wa Ilani ya uchaguzi ya mwaka 2015/2020. 

Alisema serikali ya awamu ya saba imetekeleza mambo mengi ya maendeleo zikiwemo utengenezaji wa barabara za kisasa,vituo vya afya,majengo ya kisasa ya skuli za msingi na sekondari, ujenzi wa kituo cha mafunzo ya amali, huduma za maji safi na salama. 

Alisema wananchi wa mkoa huo watafikisha shukrani zao kupitia upigaji wa kura za ndio kwa kuwachagua wagombea wa CCM ili chama kishinde na kuendelea kuongoza dola.

Akizungumza kwa niaba ya wagombea wa nafasi ya uwakilishi, mgombea uwakilishi jimbo la Donge, Dkt.Khalid Salum Mohamed alisema wanamshukru Rais wa Zanzibar Dk.Shein kwa kuasisi ujenzi wa bandari kubwa katika maeneo ya bumbwini kwani itasaidia kuongeza ajira kwa wananchi wa maeneo hayo na vijiji jirani.

Pia alisema wamejipanga kutekeleza kwa vitendo falsafa ya uchumi wa kupitia rasilimali za bahari(blue economy), na kwamba wananchi wa maeneo hayo ya kaskazini Unguja wananufaika na bahari. 

Pamoja na hayo aliwasihi wananchi kuwapigia kura za ndio wagombea wote waliosimamishwa na Chama Cha Mapinduzi na kuhakikisha wanashinda.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Anna Agata msuya ,amesema amani ya Tanzania inategemea Zanzibar hivyo ni muhimu wananchi kuwapigia kura nyingi za ndio wagombea walioteuliwa na CCM.

Jumatano, 7 Oktoba 2020

KUMEKUCHA BUMBWINI, DK.MWINYI KUMWAGA SERA, DK.SHEIN KUWATAMBULISHA WAGOMBEA.


MGOMBEA Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi(CCM), Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwasili katika kiwanja cha skuli ya Bumbwini kwa ajili ya Mkutano wa kampeni za CCM ambao mgeni rasmi ni Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar  Dk.Ali Mohamed Shein,  Wilaya ya Kaskazini 'B' Mkoa wa Kaskazini Unguja 

BAADHI ya Vijana wa Chama Cha Mapinduzi wa kundi la hamasa wakiburudisha kwa kuimba nyimbo mbalimbali katika mkutano huo wa kampeni za CCM.


VIONGOZI mbalimbali wa Chama Cha Mapinduzi wakiwa wamekaa jukwaa kuu wakisubiri mgeni rasmi awasili kwa lengo la kuanza kwa mkutano huo wa kampeni za CCM.


MAELFU ya Wana CCM na wananchi kwa ujumla wamejitokeza kwa wingi katika viwanja vya skuli ya Bumbwini kwa ajili ya kuhudhuria mkutano wa kampeni za CCM za kuwanadi,kuwatambulisha na kuwaombea kura za ndio  wagombea wa CCM kwa ngazi za Urais wa Zanzibar na jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wabunge, Wawakilishi,madiwani na wagombea kupitia viti maalum.

Mkutano huo ni miongoni mwa mwendelezo wa kampeni za CCM zinazofanyika nchini na kuhudhuriwa na wananchi wengi.

Kupitia mkutano huo mgeni rasmi ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar ambaye pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, atawatambulisha  na kuwaombea kura za ndio wagombea wote wa CCM.

Pia Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM Dk.Hussein Ali Mwinyi ataomba kura na kueleza kwa kina sera na vipaumbele vyake ili wananchi wa wilaya ya kaskazini 'B' wafanye maamuzi sahihi ya kuchagua wagombea wanaotoka katika chama chenye sera zinazotekelezeka.

tutaendelea kupata taarifa mbalimbali kupitia blog hii,,,,,,

Imeandaliwa na Kitengo cha Habari Afisi Kuu CCM Zanzibar.