Jumatano, 31 Mei 2017

BALOZI SEIF ALI IDD: AONGOZA MAMIA YA WANANCHI KATIKA MAZISHI YA MAMA MZAZI WA NAIBU KATIBU MKUU MSTAAFU WA CCM Z'BAR-VUAI ALI VUAI











MAMIA ya Wananchi wameudhuria mazishi ya Mama mzazi wa Naibu Katibu Mkuu mstaafu wa CCM Zanzibar.Vuai Ali Vuai, Marehemu Bi.Mwanaisha Hassan Vuai huko Kijijini kwao Bwejuu, Mkoa wa Kusini Unguja.

Mazishi hayo yameongozwa na Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd, aliyeambatana na viongozi mbali mbali wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar  pamoja na  jamhuri ya muungano Tanzania.

Bi. Mwanaisha amefariki jana wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Tasakhtaa  iliyopo  Vuga  Mjini  Zanzibar.

Akizungumza mara baada ya mazishi hayo, Naibu Katibu Mkuu mstaafu wa CCM Zanzibar, Nd. Vuai Ali Vuai alisema kifo cha Mama yake mzazi kimeacha pengo kubwa katika  familia hiyo  kwani marehemu huyo alikuwa akitegemewa na jamii kutokana na busara zake.

Aidha  Vuai amewashukru wananchi mbali mbali waliojitokeza kumuunga mkono katika mazishi hayo na kuwasihi waendelee kuwa na umoja wa kushirikiana katika mambo mbali mbali ya kijamii.
“  Mama yetu tulimpenda sana lakini ndio hivcyo amefariki sasa kilichobaki kwetu sisi tuliobaki ni kumuombea dua yeye pamoja na wazee wetu wengine waliofariki kabla yake.”, alisema  Naibu Katibu Mkuu huyo.

Mbali na Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar  Balozi Seif Ali Idd pia  Mazishi hayo yameudhuriwa na Viongozi  mbali mbali  wakiwemo Katibu Mkuu wa CCM   Abdulrahman Omar Kinana, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar   Dkt. Abdalla Juma Saadala “ Mabodi”,  Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Tanzania Shaka Hamdu Shaka,  Mkuu wa Mkoa kusini Unguja    Dk.Idrissa  Muslim Hija, Katibu  wa Kamati Maalum  ya NEC, Idara ya Itikadi na Uenezi Zanzibar, Waride Bakari  Jabu.

Viongozi wengine ni Mkuu wa Wilaya ya Kusini Unguja, Idrissa  Kitwana  Mustafa, Mnadhimu wa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi  wa CCM, Ali Salum Haji pamoja na baadhi ya Mawaziri, Manaibu Mawaziri  na Makatibu wakuu wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Bi.Mwanaisha Hassan Vuai amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 85 ameacha watoto tisa (9) pamoja na wajukuu kadhaa.
Mungu ailaze roho ya marehemu pahali pema peponi-Amin.

Ijumaa, 26 Mei 2017

DKT.MABODI AWATAKA WAWAKILISHI, WABUNGE NA MADIWANI KUJITATHIMINI

NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Dkt. Abdalla Juma Saadala  “ Mabodi”  amewataka viongozi wa kisiasa wa chama hicho waliopewa dhamana ya kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2015/2020 kwa wananchi waanze kujitathimini mapema kabla ya uchaguzi mkuu ujao.

Rai hiyo ameitoa katika hafla ya utekelezaji wa Ilani hiyo iliyoandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Donge, Nd. Sadifa Juma  katika jimbo hilo huko Kaskazini “B” Unguja.

Dkt. Mabodi aliwambia viongozi wa kisiasa waliochaguliwa na wananchi kuanzia ngazi za Madiwani, Wawakilishi, Wabunge na Rais wa Zanzibar  kuwa utaratibu wa kubuni na kutekeleza miradi ya maendeleo sambamba na kuimarisha miradi ya huduma za kijamii sio suala la hiari bali ni lazima kwa kila aliyetumia tiketi ya chama hicho kuomba  ridhaa ya kuwatumikia wananchi.

Naibu Katibu Mkuu huyo amesifu juhudi za baadhi ya viongozi wanaoendelea kutekeleza ahadi walizoahidi kwa wananchi awamu kwa awamu kuanzia ngazi za chini hadi taifa, na kuwataka waliojisahau kurudi Majimboni mwao kutatua kero zinazowakabili wananchi.

“ Njia pekee ya CCM kubaki madarakani ni kutatua kero za wananchi mijini na vijijini bila kujali itikadi za kisiasa na kidini ili jamii endelee kujenga imani na upendo wa kudumu kwa Chama kilichoiweka serikali madarakani”, alisema Dkt. Mabodi.

Hata hivyo Naibu Katibu Mkuu huyo Dkt. Mabodi alitoa ahadi ya shilingi 300,000 kwa skuli ya maandalizi Mkataleni pamoja na kusaidia ujenzi wa vyoo vya skuli hiyo ili watoto waweze kusoma katika mazingira bora.

Akizungumza  Mbunge wa Jimbo hilo, Nd. Sadifa Juma mara baada ya kutoa mabati 400 yenye thamani ya shilingi milioni saba ili kuezekea Hospitali ya Vijibweni, Maskani ya Kitaruni, Maskani ya Karange, vijibweni “B” Maskani, Donge bridge, pamoja na Skuli ya maandalizi ya Mkataleni.

Aidha  Nd.Sadifa mbali na kugawa mabati hayo pia alitoa fedha taslimu zaidi ya shilingi milioni 1.5 kwa hospitali ya Vijibweni inayotegemewa na wananchi wa Jimbo hilo na maeneo jirani kwa huduma mbali mbali za afya ili kiweze kufanyiwa matengenezo na kuwa cha kisasa.

Akitoa shukrani zake Daktari dhamana wa Kituo hicho, Bi.Miza Ali Ussi alipongeza juhudi za mbunge huyo na alisema msaada huo umepatikana kwa wakati mwafaka kwani kwa muda mrefu walikuwa wakikabiliwa na changamoto za upungufu wa vifaa tiba na mabati ya kuezekea baadhi ya nyumba za hospitali hiyo.








Jumanne, 23 Mei 2017

Chagueni Viongozi wenye sifa na uwezo

NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR.

NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar,  Abdalla Juma Saadala "Mabodi" amezitaka jumuiya za Chama hicho kutumia vizuri fursa ya uchaguzi kuwapitisha viongozi wenye sifa na uwezo wa kukiletea ushindi chama katika Uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.

Kauli hiyo ameitoa wakati akifungua mafunzo elekezi ya kuwajengea uwezo viongozi wa majimbo Tisa (9) ya Chama na Jumuiya za Mkoa wa Mjini juu ya mabadiliko ya Katiba ya CCM ya 1977 yaliyofanyika hivi karibuni yaliyofanyika Katika ukumbi wa mkoa huo Aman Unguja.

Alisema uchaguzi  unaofanyika hivi sasa katika kwa ngazi mbali mbali za Chama hicho ndio uwanja wa kuandaa jeshi kamili la kisiasa lililokamilika kila idara na lenye ujuzi na mafunzo yote ya vita ya kisiasa litakaloweza kupambana kwa ujasiri na kufanikisha ushindi katika uchaguzi mbali mbali za Dola ili CCM iendelee kushinda na kutawala kupitia utaratibu wa Kidemokrasia.

Aliwasihi washiriki wa mafunzo hayo kutumia vyema mafunzo hayo ya siku moja ili waweze kuwa na uelewa mpana wa Mabadiliko kadhaa yaliyofanyika ndani ya katiba ya CCM ili watekeleze kwa ufanisi majukumu yao na kuwaelimisha wanachama wengine juu ya taaluma hiyo.

Dkt.Mabodi alieleza kwamba matarajio ya taasisi hiyo ya kisiasa ni kuona   kasi ya mabadiliko ya kiutendaji kwa haraka hasa kwa viongozi na watumishi wa Chama na jumuiya zake.

Pia aliongeza kwamba mbali na matarajio hayo mafunzo hayo yatamaliza mizozo na malalamiko yaliyokuwa yalisababisha kutokuwepo kwa ufanisi mzuri wa kiutendaji kwa baadhi ya maeneo ndani ya Mkoa huo.

Naibu Katibu Mkuu huyo alisema hatovumilia tabia za kupangwa safu za viongozi  kwani kufanya hivyo ni kukiuka Kanuni za maadili na miongozo ya uchaguzi huo.

" Tumekuwa tukisema siku zote kuwa CCM ndio mwalimu wa Demokrasia yaani hivyo vyama vya upinzani demokrasia na ustaarabu wa kisiasa tumewafunza sisi hivyo dhana hizo lazima tuzisimamie na kuzitekeleza kwa vitendo kupitia uchaguzi unaoendelea ndani ya taasisi yetu.", alisema Dkt.Mabodi na kuzitaka kamati za uchaguzi na maadili kufuatilia kwa kina mwenendo wa uchaguzi na watakapobaini kasoro watoe taarifa kwa ngazi husika ili zitafutiwe ufumbuzi wa haraka.

Alifafanua kwamba kupitia uchaguzi huo panatakiwa kupatikana viongozi na watendaji watakaoendeleza siasa za upendo, maendeleo, umoja pamoja na mshikamano unaojali misingi ya kidemokrasia ndani na nje ya taasisi hiyo.

Hata hivyo alieleza dhamira ya chama hicho kupitia mabadiliko yaliyofanyika katika Katiba ya Taasisi hiyo kuwa ni pamoja na kila mwanachama kujipanga kisaikolojia kusaidia kuimarisha uchumi wa CCM kupitia rasilimali zilizopo sambamba na kubuni miradi mingine ya kimaendeleo.

Sambamba na hayo kupitia Mafunzo hayo Dkt.Mabodi aliwakumbusha washiriki hao kwamba ili wafanikiwe katika utendaji wao ni lazima watumie vizuri rasilimali watu ya wazee wa CCM pamoja na wastaafu katika sekta za umma na binafsi kwani wana uwezo na uzoefu mkubwa  wa kushauri na kutoa maelekezo mazuri juu ya masuala mbali mbali ya kiutendaji ndani ya Chama hicho.

Mapema akizungumza katika mafunzo hayo Mwenyekiti wa Mkoa huo, Nd. Bora afya Juma Silima alisema Mkoa huo umejipanga kufanikisha kwa ufanisi uchaguzi huo ili kulinda historia ya chama hicho katika kufanikisha uchaguzi unaoheshimu misingi ya utawala bora na demokrasia kwa wananchi wote.

.

..

Jumanne, 16 Mei 2017

CCM Z'BAR YAAHIDI KUENZI USHIRIKIANO NA CHAMA CHA CPC CHA CHINA

Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dkt. Abdalla Juma Saadala akizungumza na Balozi mdogo wa China Zanzibar Bw. Xie Xiaowu juu ya masuala mbali mbali ya kimaendeleo huko  Afisi Kuu Zanzibar.


NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Dkt. Juma Abdalla Saadala “Mabodi” amesema Chama cha mapinduzi (CCM) kitaendelea kuenzi kwa vitendo ushirikiano uliodumu zaidi ya karne moja baina ya chama hicho na Chama Cha Ukombozi cha China (CPC).

Kauli hiyo ameitoa wakati akizungumza na Balozi Mdogo China Zanzibar Bw. Xie Xiaowu uliotembelea Afisi Kuu Kisiwandui Zanzibar.

Amesema ushirikiano uliopo baina ya vyama na serikali za nchi hizo zimeimarika na kuzaa matunda yanayowanufaisha wananchi wa pande zote  mbili katika nyanja za kiuchumi, kisiasa na kijamii.

Dkt. Mabodi alieleza kwamba njia pekee ya kulinda hazina hiyo ni kuwarithisha Vijana  Elimu na ujuzi zitakazowasaidia kupata uwezo wa kitaaluma  wa kulinda urithi huo dhidi ya maadui na wapinga maendeleo wa nchi hizo.

 “ Ushirikiano baina ya CPC na CCM ni ya muda mrefu hivyo sisi vizazi vya sasa ni lazima tujivunie huku tukiyalinda ili tuendele kunufaika na fursa za nchi hizo.

Kwa upande wake Balozi Mdogo wa China Bw. XIE XIAOWU ameahidi kwamba China itatoa ushirikiano wa Ari na Mali ili kuhakikisha Zanzibar inakuwa nchi yenye nguvu kiuchumi na kijamii.

Alisema lengo la ziara hiyo ni kuimarisha mahusiano baina ya vyama hivyo na serikali zake ili viweze kutekeleza kwa ufanisi mikakati ya kimaendeleo iliyoachwa na Viongozi Wakuu wa taasisi hizo toka enzi za kusaka uhuru wa nchini hizo.

Sambamba na hayo Balozi huyo Bw. Xie Xiaowu alisifu juhudi za maendeleo zinazofanywa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inayotokana na CCM kuwa zinaongeza ushawishi na nia ya China kuendelea kusaidia sekta mbali mbali nchini ili ziweze kufanya kazi kwa ufanisi.

Pamoja na Hayo alimpongeza Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Dkt. Mabodi kuwa ni kiongozi mchapakazi kutokana na kuwa karibu na taasisi za kimataifa pamoja na wananchi kwa ujumla licha ya kuteuliwa kushika nafasi hiyo kwa muda mfupi.

“  China inathamini juhudi mikakati mbali mbali ya maendeleo inayofanywa na Serikali ya Mapinduzi kwa lengo la kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya Chama Tawala, hivyo na sisi  bado tuna nia na mikakati ya muda mrefu ya kuwaunga mkono kupitia  sekta za Afya, Elimu, Uvuvi na Miundombinu”, alifafanua Balozi huyo wa China.

Baada ya ziara hiyo Ujumbe wa China ulitembelea sehemu mbali mbali za makumbusho zikiwemo sehemu aliyouliwa aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Zanzibar na mwenyekiti wa balaza la mapinduzi  Marehemu Mzee Abeid Karume kisiwa ndui mjini     zanzbar.















DKT.MABODI ASHIRIKI UJENZI WA MSKITI WA IJITIMAI YA KIMATAIFA UNGUJA.

Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Dkt. Abdalla Juma Saadala “ Mabodi” amewasihi viongozi na waumini wa dini ya kiislamu kutumia fursa ya Ijitimai kuliombea taifa liendelee kudumu katika hali ya Amani na Utulivu. 

Nasaha hizo amezitoa mara baada ya kushiriki katika shughuli za ujenzi wa Msikiti wa Ijitimai ya Kimataifa huko katika kijiji cha Kidoto Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Alisema mamia ya waumini wa dini ya kiislamu watakaoshiriki katika ijitimai hiyo watakuwa ni sehemu muhimu ya kufanya dua mbali mbali za kuimbea nchini inusurike na maafa ili wananchi waendelee na shughuli zao za kijamii. 

Alieleza kwamba CCM inaunga mkono juhudi zinazofanywa na taasisi za kidini nchini katika kuhubiri amani na mshikamano kwa wananchi wa visiwa vya Zanzibar na Tanzania kwa ujumla. Alisema licha ya Chama hicho kuwa ni taasisi ya kisiasa bado kina jukumu kubwa la kushiriki kikamilifu katika shughuli za kidini zinazoendeshwa na wananchi wa wa itikadi tofauti za kisiasa.

Aidha kwamba Chama Cha Mapinduzi Zanzibar kitatoa msaada wa kupeleka nguzo za umeme katika nyumba ya wageni pamoja na kununua vifaa vya samani za ofisi ya jumuiya inayosimamia Ijitimai hiyo ili waweze kufanya kazi zao kwa ufanisi. Akitoa taarifa juu ya maendeleo ya Ijitimai hiyo, Katibu wa Jumuiya hiyo, Sheikh Mwalim Hafidh amesema bado wanaendelea kumalizia ujenzi wa msikiti utakaochukua waumini zaidi ya 5100 kwa wakati mmoja.

Alisema bado wanakabiliwa na changamoto za upungufu wa vifaa vya ujenzi wa mabanda yatakayotumika wakati wa Ijitimai pamoja na ujenzi wa shule , chuo cha madrasa, hospitali na maktaba pamoja na miundombinu mingine nyingine ya kijamii. Aidha ameupongeza uongozi wa CCM kwa ziara hiyo na kueleza kuwa taasisi nyingi za kisiasa zimekuwa hazishiriki ipasavyo katika masuala ya kidini hali inayosababisha kutokuwepo na ushirikiano mzuri kwa taasisi hizo.

Naye Makamo Mwenyekiti wa Jukumiya Fiysabilillah Tabligh Markaz Zanzibar, Sheikh Wakat Hassan Bakar Alisema lengo la jumuiya hiyo ni kukifanya kijiji hicho kuwa chimbuko la uislamu na ibada. Naibu Katibu Mkuu huyo ameambatana na baadhi ya ujumbe kutoka Baraza la Wazee CCM Zanzibar, Uongozi wa CCM Mkoa wa Kaskazini Unguja na Mkuu wa Mkoa huo, Vuai Mwinyi Mohamed. Ijitimai hiyo inatarajiwa kufanyika Mai 19, mwaka huu na kuudhuriwa na wageni kutoka nchi za Kenya, Burundi, Rwanda, Malawi, Uganda, Ethiopia na Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo. 

































Jumamosi, 13 Mei 2017

Mabodi " Awataka wanaCCM pamoja na wananchi wote kujenga utamaduni wakujitolea"


Naibu katibu Mkuu Zanzibar Dkt. Abdalla Juma Sadala akishirikiana na wananchi, wanachama wa CCM na Viongozi mbali mabali wa Chama Cha Mapinduzi katika Ujenzi wa Nyumba ya Balozi wa Nyumba kumi Ndugu Asha Abdalla  huko Fuoni Migombani leo hii.


Nyumba hio ambayo ilipata maafa ya mvua kubwa ambazo zinaendelea kunyesha visiwani humu