Alhamisi, 31 Januari 2019

MATUKIO KATIKA PICHA ZIARA YA NAIBU KATIBU MKUU WA U.W.T Z'BAR NDG.TUNU JUMA KONDO ALIPOKUTANA NA MABARAZA YA WILAYA YA AMANI NA MJINI YA UMOJA HUO.


NAIBU Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi UWT Zanibar Ndugu Tunu Juma Kondo akiwahutubia Wajumbe wa Mabaraza ya Wilaya za Amani na Mjini za Umoja huo, ikiwa ni ziara yake ya mwanzo toka ateuliwe kushika nafasi hiyo na kujitambulisha pamoja na kupanga mikakati ya kuimarisha UWT.

 MWENYEKITI wa UWT Mkoa wa Mjini Ndugu Ghanima Sheha akizungumza namna Mkoa wake ulivyojipanga katika kusimamia maslahi na fursa za wanawake katika nyanja za kiuchumi,kisiasa na kijamii.

 KATIBU wa CCM Mkoa wa Mjini Ndugu Mohamed Nyawenga akizungumza katika hafla hiyo iliyofanyika katika Ukumbi wa CCM Mkoa wa Mjini Amani Unguja.

 KATIBU wa UWT Mkoa wa Mjini Ndugu Stahamili Omar akisoma risala ya Umoja huo mbele ya Naibu katibu Mkuu wa UWT Zanzibar Ndugu Tunu Juma Kondo katika hafla ya kujitambulisha.



NAIBU Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi UWT Zanibar Ndugu Tunu Juma Kondo akikabidhi kadi za UWT kwa wanachama wapya wa Umoja huo.




 WANACHA wapya wa UWT wakila kiapo cha utii kwa kusoma ahadi za mwanachama wa CCM mara baada ya kukabidhiwa kadi hizo.



 KATIBU wa UWT Wilaya ya Mjini Ndugu Khadija Juma Khamis akisoma ratiba ya Hafla hiyo.

 BAADHI ya Wajumbe wa Mabaraza ya Wilaya a Mjini na Amani za Umoja huo wakiimba kwa shangwe nyimbo mbali mbali za Chama na UWT.


 BAADHI ya Waasisi na Waanzilishi wa UWT wakiwa katika hafla hiyo.








Jumatano, 30 Januari 2019

HOSPITALI YA WILAYA KASKAZINI 'A' KIVUNGE YAKABIDHIWA VIFAA TIBA.


 MWENYEKITI wa Kikundi cha Hamasa Afisi Kuu ya CCM Zanzibar Ndugu Shaaban Ali Othman (kushoto) akimkabidhi Daktari dhamana Tamim Hamad Said(kulia)  Friji mbili za kuhifadhi dawa za hospitali zilizotolewa na kikundi cha hamasa cha vijana wa  Afisi Kuu CCM Zanzibar.

 
MWENYEKITI wa Kikundi cha Hamasa Afisi Kuu ya CCM Zanzibar Ndugu Shaaban Ali Othman (wa pili kushoto) akizungumza mara baada ya kuwasili katika Hospitali ya Wilaya ya Kaskazini ‘A’ Unguja, Daktari dhamana Tamim Hamad Said (wa kwanza kushoto) pamoja na Katibu wa CCM Wilaya ya Kaskazini ‘A’ Haji Machano Juma(wa kwanza kulia) wakiwa katika hafla ya makabidhiano ya vifaa tiba vilivyotolewa na kikundi cha hamasa.

 KATIBU wa Kikundi cha Hamasa  cha Afisi Kuu ya CCM Zanzibar ndugu Suleiman Mohamed Rashid (wa kwanza kushoto aliyesimama) akizungumza katika kikao cha hafla ya makabidhiano ya mafriji mawili yaliyotolewa na kikundi cha hamasa.

 KATIBU wa CCM Wilaya ya Kaskazini 'A' ndugu Haji Machano Juma akizungumza katika hafla hiyo.

 Daktari Dhamana wa Hospitali hiyo Tamim Hamad Said, akizungumza katika hafla hiyo ya makabidhiano ya mafriji ya kuhifadhi  dawa.

 Katibu Msaidizi wa Taasisi hiyo Ndugu Khamis Salum Abdi , akizungumzia mafanikio yaliyofikiwa na CCM.

 Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Kaskazini Unguja, Ndugu Pandu Salum Sungura .

 BAADHI ya vijana wa kikundi cha hamasa cha Afisi Kuu ya CCM Zanzibar wakisikiliza kwa makini nasaha za viongozi mbali mbali wa CCM, UVCCM na Hospitali ya Wilaya Kivunge katika hafla ya makabidhiano ya Vifaa Tiba iliyofanyika leo Tarehe 30/01/2019

 Picha ya pamoja  ya Wajumbe wa Kikundi cha Hamasa cha Afisi Kuu ya CCM Zanzibar pamoja na Uongozi wa Hospitali ya Wilaya Kivunge , Mkoa wa Kaskazini Unguja, mara baada ya hafla ya makabidhiano ya vifaa tiba.
 
NA IS-HAKA OMAR,ZANZIBAR.
VIJANA mbali mbali nchini wameshauriwa kuendeleza utamaduni wa kujitolea katika kuisaidia jamii katika masuala mbali mbali ya kiuchumi, kijamii, kisiasa na kimaendeleo.

Rai hiyo imetolewa leo na Mwenyekiti wa Kikundi cha Hamasa cha Afisi Kuu ya CCM Zanzibar Ndugu Shaaban Ali Othman wakati akikabidhi Friji(Jokofu) mbili zilizotolewa na kikundi hicho na kukabidhi Uongozi wa Hospitali ya Kivunge ya Wilaya Kaskazini 'A' Unguja.

Amesema vifaa hivyo vimetolewa kwa ajili ya kusaidia uhifadhi wa vifaa tiba vya hospitali hiyo hasa dawa za matumizi ya binadamu zinazohitaji hali ya baridi muda wote.

Ameutaka uongozi wa Hospitali hiyo kuvitunza na kuvitumia katika matumizi yaliyokusudiwa ili vitoe huduma endelevu kwa wananchi mbali mbali wanaofika hopitalini hapo kwa ajili ya matibabu.

Pamoja na hayo amebainisha kuwa vifaa hivyo ni sehemu ya kuunga mkono juhudi zinazofanywa na viongozi wa CCM ambao ni Mwenyekiti wa CCM Taifa Dkt.John Pombe Magufuli pamoja na Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein wanaotekeleza kwa kasi  mipango ya maendeleo kwa maslahi ya wananchi wote.

Ameeleza kwamba vijana nchini wana wajibu wa kutekeleza kwa vitendo masuala mbali mbali ya kijamii kwa lengo la kuwasaidia wananchi wanaokabiliwa na changamoto katika mazingira wanayoishi.

Katika maelezo yake Mwenyekiti huyo Shaaban,amesema endapo vijana wa Zanzibar wataweka mbele dhana ya uzalendo,umoja, mshikamano na kuelekezana mambo mema ya kuisaidia jamii, itasaidia Zanzibar kuwa nchi bora zaidi duniani iliyopiga hatua kubwa za kimaendeleo.

Awali Katibu wa Kikundi hicho cha Hamasa, Suleiman Mohamed Rashid amefafanua kuwa kikundi hicho kitaendelea kusaidia masuala mbali mbali ya kijamii katika maeneo mbali mbali yaliyopo katika Wilaya zote za Unguja na Pemba.

Amesema Chama Cha Mapinduzi kipo mstari wa mbele kushughulikia changamoto  zinazoikabili jamii katika maeneo ya mijini na vijijini.

Akizungumza mara baada ya kupokea vifaa hivyo Daktari Dhamana wa Hospitali hiyo Tamim Hamad Said, amesema uongoizi wa hospitali hiyo umefurahi kupokea vifaa hivyo kwani vilikuwa ni miongoni mwa mahitaji muhimu ya taasisi hiyo.

Dr.Tamim ameahidi kuvitumia kwa malengo yaliyokusudiwa hasa kuhifadhi dawa na vifaa mbalimbali vinavyotumika katika matibabu ili wananchi wapate huduma bora za Afya.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Kaskazini Unguja, Ndugu Pandu Salum Sungura amesema vijana wa mkoa huo wapo imara katika kuunga mkono juhudi za vijana wenzao wa kikundi cha hamasa kutoka Afisi Kuu ya CCM Zanzibar, kilichoonyesha mfano bora wa kutoa vifaa hivyo kwa hospitali ili viwasaidie wananchi wa Mkoa huo.

Akizungumza katika hafla hiyo kwa niaba ya Afisi Kuu ya CCM Zanzibar, Katibu Msaidizi wa Taasisi hiyo Ndugu Khamis Salum Abdi amesema Chama Cha Mapinduzi kinaendelea kusimamia na kutekeleza Ilani yake ya Mwaka 2015/2020 kwa ufanisi mkubwa kwa lengo la kumaliza kero zinazoikabili jamii.

Amesema suala la kuwapelekea wananchi maendeleo halina itikadi za kisiasa hivyo kila mwananchi, kikundi pamoja na taasisi yoyote wana wajibu wa kutatua changamoto za wananchi.

Jumamosi, 19 Januari 2019

MATUKIO KATIKA PICHA UZINDUZI WA KAMATI NDOGO NDOGO ZA UWT Z'BAR TAREHE 19/01/2019.


 NAIBU Katibu Mkuu wa UWT Zanzibar Ndugu Tunu Juma Kondo akitoa ufafanuzi wa majukumu mbali mbali ya Kamati hizo ambazo ni nne zilizozinduliwa kutokana na Matakwa ya Kanuni ya Umoja huo.

 BAADHI ya Wajumbe wa Kamati ndogo ndogo za UWT wakifuatilia kwa makini maelekezombalimbali yanayotolewa na Viongozi wa UWT wa Afisi Kuu ya Umoja huo Zanzibar.



KATIBU wa Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar ambaye pia ni Mjumbe wa  Kamati zilizozinduliwa Ndugu Catherine Peter Nao akizungumzia akichangia mada juu ya uimarishaji wa Kamati zilizozinduliwa na UWT kwa lengo la kuongeza ufanisi wa Kiutendaji wa Umoja huo. 
 WAJUMBE wa Kamati Ndogo ndogo za UWT wakisoma Dua mara baada ya kukamilisha hafla ya uzinduzi wa Kamati za Nne za Kiutendaji za mwaka 2019-2020. 

 WAJUMBE wa Kamati Nne za UWT Zanzibar zilizozinduliwa leo Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Zanzibar wakiwa katika Picha ya Pamoja mara baada ya uzinduzi wa Kamati hizo.(PICHA NA IS-HAKA OMAR)


UWT Z'BAR YAZINDUA RASMI KAMATI NNE NDOGO NDOGO ZA KUCHAPA KAZI KUELELEA 2020.

 MAKAMU Mwenyekiti wa UWT Taifa Ndugu Thuwayba Kisasi akizungumza na Wajumbe wa Kamati Nne ndogo ndogo za Umoja huo zilizozinduliwa leo Tarehe 19/01/2019  rasmi kwa lengo la kuongeza ufanisi wa Kiutendaji. 



NA IS-HAKA OMAR,ZANZIBAR.

UMOJA wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi(UWT) Tanzania kwa upande wa Zanzibar, leo umezindua rasmi kamati ndogo ndogo nne zitakazokuwa na majukumu mbali mbali ya kufanisha kwa ufanisi kazi za umoja huo kwa mwaka 2019/2020.

Akizungumza mara baada ya uzinduzi huo Makamu Mwenyekiti wa UWT Taifa Ndugu Thuwayba Kisasi amezitaja kamati zilizozinduliwa kuwa ni pamoja na Kamati ya Uchumi, Mipango na Fedha, Kamati ya Mawasiliano kwa Umma, Kamati ya Elimu,Malezi na Mafunzo pamoja na Kamati ya Mahusiano na Taasisi za Wanawake ndani na nje ya Nchi.

Amesema kuzinduliwa kwa kamati hizo ni matarajio makubwa zaidi ni kuwafikia Wanawake  na Vijana pamoja na makundi mbali mbali yaliyopo katika jamii na watoto ili kushinda Uchaguzi ujao mwaka 2020.

Katika maelezo yake Makamu Mwenyekiti huyo amewasisitiza Wajumbe wote wa Kamati hizo kufanya kazi kwa ushirikiano mkubwa ili kufikia malengo yaliyokusudiwa katika utekelezaji wa majukumu ya msingi ya UWT pamoja na CCM kwa ujumla.

“Wanawake ni Jeshi kubwa tena la ukombozi ndani ya Chama Cha Mapinduzi, nasaha zangu kwenu ni kwamba tutumie nafasi hii kuhakikisha tunawafikia wanawake wote hasa waliopo Vijijini na Pembezoni kwa nia ya kuwaweka karibu na kufanya nao shughuli zetu za kisiasa.

Pia Wanawake wa UWT lazima tupate Sauti zetu kila mmoja kwa nafasi yake ndani ya Umoja Wetu kuyasema mambo mema yanayotekelezwa na CCM chini ya Viongozi wetu Wakuu ambao ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein pamoja na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli wanaoendelea kusimamia kwa vitendo Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015/2020.”, amesema Makamu Mwenyekiti Thuwayba Kisasi.

Amewataka Wanawake nchini kushirikiana katika malezi ya Watoto ili waweze kukuwa wakiwa katika malezi na maadili bora yatakayowasaidia kupambana na changamoto za mmomonyoko wa maadili.

Awali akizungumza Naibu Katibu Mkuu wa UWT Zanzibar Ndugu Tunu Juma Kondo , ameeleza kuwa UWT imejipanga kufanya kazi zake Kisayansi zaidi kwa lengo la kufanikisha kwa wakati malengo waliyojiwekea ndani ya Umoja huo.

Aidha amesema Kamati hizo zilizozinduliwa zitakuwa ni chachu ya kubuni miradi mipya ya kiuchumi itakayoongeza kipato ndani ya UWT pamoja na kupatikana fursa ya mahusiano mazuri na Taasisi mbali mbali za Wanawake Duniani.

Kwa upande wake Mjumbe wa Kamati tekelezaji WUT Taifa Ndugu Lucy  Mwakembe amesema Umoja huo utaendelea kupanga mikakati mbali mbali ya kimaendeleo ili kujiinua kiuchumi.



Jumamosi, 12 Januari 2019

MATUKIO KATIKA PICHA MAADHIMISHO YA MIAKA 55 YA MAPINDUZI-PEMBA.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Mkuu wa Brigedi ya Nyuki Zanzibar, Brigedia Jenerali Fadhil Omar Nondo, alipowasili katika viwanja vya Gombani Kisiwani Pemba, kuhudhguria Maadhimisho ya Miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti  wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akiwapungua Mkono Wananchi akiwa katika gari Maalum ya Jeshi la Wananchi Tanzania JWTZ, wakati akiingia katika Uwanja wa Gombani Kisiwani Pemba kuhudhuria Maadhimisho ya Miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar, akiwa Mkuu wa Brigedi ya Nyuki Zanzibar, Brigedia Jenerali Fadhil Omar Nondo.

 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akipokea shatu ya Gwaride rasmin la maadhimisho ya Miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar, yaliofadhimishwa kisiwani Pemba katika Uwanja wa Gombani.

 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe,Ali Mohamed Shein, akikagua Gwaride rasmin la Sherehe za Mapinduzi kuadhimisha Miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar zilizofanyika katika Uwanja wa Gombani Kisiwani Pemba. 


 ASKARI wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ, wakionesha jinsi ya uchezaji wa Gwarige la kimya, wakati wa Sherehe za Miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar zilizofanyika Uwanja wa Gombani.



 MKE wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Marehe Mzee Abeid Amani Karume, Mama Fatma Karume, Mke wa Rais Mstaaf wa Tanzania Mama Anna Mkapa na Mke wa Rais Mstaaf wa Zanzibar Mama Shadya Karume, wakifuatilia Hutuba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, katika Uwanja wa Gombani Kisiwani Pemba.

 VIONGOZI mbali mbali wa Kitaifa wakiwa katika uwanja wa Gombani Pemba.