NA IS-HAKA
OMAR, DAR ES SAALAM.
MAKAMU Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa Tanzania Dk.Abdalla Juma Saadalla 'Mabodi' |
BARAZA la Vyama vya Siasa Tanzania limekutana jana Januari 18, 2018 pamoja na mambo mengine wajumbe wa Baraza hilo wamemchagua na kumthibitisha Makamu Mwenyekiti mpya Dk.Abdalla Juma Saadalla ‘Mabodi'.
Mara baada ya Baraza hilo kumthibitisha
Dk.Mabodi ameahidi kusimamia mshikamano wa Kitaifa, kulinda utamaduni wa
maridhiano ya kisiasa sambamba na kuheshimu tunu za kitaifa kwa lengo la kuenzi
dhana ya demokrasia kwa vyama vyote nchini.
Akizungumza katika Mkutano huo uliofanyika Ofisi
ndogo ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dar es saalam.
Dk.Mabodi
ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Ameeleza kwamba misingi
hiyo ndio chimbuko la kuwaunganisha
Watanzania bila kujali asili ya uzawa itikadi za kisiasa na kidini.
“Nitaheshimu itikadi za vyama vyote vya
kisiasa nchini lakini nasisitiza tulinde demokrasia maana kama demokrasia ikipote gharama za kuirejesha ni
kubwa kuliko tunavyofikria “,.alisema Mabodi na kusisitiza kuwa kila chama kina
wajibu wa kulinda haki na utu wa wananchi kupitia sera huru zinazohimiza Amani
na Utulivu wa kudumu.
Pia amehimiza utaratibu wa kujenga hoja imara
za kuhamasisha maendeleo na kulinda rasilimali za nchi.
Dk.Mabodi amesema akiwa ni kiongozi ndani ya
Baraza hilo atalinda Katiba zote mbili ya jamhuri ya muungano wa Tanzania ya
mwaka 1977 na Katiba ya Zanzibar ya Mwaka 1984 pamoja na kutoa kipaumbele kwa
wananchi kupata habari, maoni na ushiriki katika siasa kwa mujibu wa Katiba na
miongozo ya kisiasa.
Kupitia hotuba yake Dk.Mabodi aliwahakikishia
Wajumbe wa Baraza hilo na wananchi kwa ujumla kuwa hatoruhusu baadhi ya
wanasiasa watakaohubiri sera na ajenda za kudhihaki mihimili ya Dola iliyopo
Kikatiba, kwani kufanya hivyo ni sawa na kuzalisha mbegu za chuki na migogoro
isiyokuwa ya lazima nchini.
Aidha alisema kupitia Baraza hilo ni lazima
kila Chama cha siasa nchini kijielekeze katika kufanya siasa za kuwaunganisha
wananchi katika masuala mbali mbali ya maendeleo .
“ Siasa za jino kwa jino ncha ya upanga kwa
ncha ya upanga zimepitwa na wakati hivyo ni muhimu sana sisi viongozi kupitia
vyama vyetu tujitathimini na kuwa mfano bora kwa wananchi”,alisema
Makamu Mwenyekiti huyo.
Hata hivyo amewashukru wajumbe wa baraza hilo
kwa kumuamini na kumchagua ili aweze kutoa mchango wake wa kiuongozi na
kiutendaji kwa maslahi ya Taifa kwa ujumla.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza hilo,
John Shibuda alisema kila chama kina wajibu wa kuthamini juhudi za serikali
katika utekelezaji masuala mbali mbali yanayowanufaisha wananchi wote bila
ubaguzi.
Katika Mkutano huo walifanya uteuzi wa Kamati
nne za kudumu za Baraza hilo ambazo ni Kamati ya fedha, Kamati ya Bunge na
Siasa, Kamati ya Maadili na uhusiano pamoja na Kamati ya Sheria na Utawala bora
zenye dhamana ya kusimamia mwenendo wa
utendaji wa vyama pamoja na Kamati ya uongozi ya baraza la vyama vya siasa.
Sambamba hayo pia Baraza hilo lilipokea maoni
ya vyama vya siasa na mapendekezo ya wadau mbali mbali juu ya marekebisho ya
sheria ya vyama vya siasa ya mwaka 1992 pamoja na mapendekezo yake.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni