Jumapili, 7 Januari 2018

DK.SHEIN: TIBIRINZI NI SOKO LA WANANCHI WOTE.

 RAIS wa Zanzibar  na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akizindua Soko la Tibirinzi lililopo Chakecheke Pemba.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, amesema kuwa miongoni mwa malengo ya mapinduzi matukufu ya mwaka 1964, ni kuzifanya hali za maisha ya wazanzibari kuwa bora.

Dk. Shein alieleza hayo huko Tibirinzi Chakechake, mara baada ya kulizindua soko jipya la Tibirinzi, ikiwa ni miongoni mwa shamra shamra za kutimia miaka 54 ya mapinduzi.

Amesema ujenzi wa soko la Tibirinzi, umelenga kuinua maisha ya wananchi sambamba na kujipatia mahitaji yao na kamwe lisitumike kama kichocheo cha kubaguana misingi ya vyama, dini, jinsia au mahala mtu anapotokea.

Amesisitiza kuwa jengo soko hilo jipya ni ukombozi kwa wakulima, wafanyabiashara, wafugaji, wavuvi, wajasiriamali na wananchi wote kwa jumla kwa kuwaongezea kipato chao kitakachoimarisha maisha yao.

Amesema si vyema soko hilo likahusishwa na masuala ya kisiasa kwani ni soko la watu wote wa vyama vyote, dini zote na jinsia zote huku akiwataka wafanyabiashara watakaolitumia soko hilo kuleta bidhaa zenye ubora zitakazolingana na hadhi ya soko hilo.

Ameeleza  kuwa ujenzi wa soko hilo ni katika hatua za kutafsiri mapinduzi ya mwaka 1964 kwa vitendo kwa kuwaletea wananchi maendeleo zaidi bila ya ubaguzi.

Ametumia  fursa hiyo kueleza mafanikio sambamba na azma ya mapinduzi matukufu ya Januri 12, 1964 ambayo yamewakomboa wananchi wa Zanzibar na kukata minyororo ya chuki, udhalimu na manyanyaso.

Ameeleza  madhumuni ya mapinduzi ya Zanzibar ni kuwa huru hatua ambayo imepekea kupanga mambo bila ya kuingiliwa na mtu na kuweza kuongoza nchi sambamba na kuandaa mipango ya muda mrefu na muda mfupi na wakati.

Amesema kuwa Zanzibar imepata maendeleo makubwa katika kukuza uchumi wake ndani ya kipindi cha miaka 54 huku akieleza kuwa mabadiliko makubwa ya kiuchumi, sera ya serikali maisha ya watu ambayo yote hayo ni maendeleo.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni