Jumapili, 21 Januari 2018

MATUKIO KATIKA PICHA MKUTANO WA UCHAGUZI WA SHIRIKISHO LA VYUO VIKUU CCM SENETI YA UNGUJA.


 BAADHI ya Maafisa wa UVCCM na CCM Zanzibar wakimsubiri Mgeni rasmi katika  Mkutano wa Shirikisho la Vyuo Vikuu CCM  Seneti ya Unguja uliofanyika Afisi Kuu ya CCM  Kisiwandui Zanzibar.

 Mwenyekiti  mtaafu wa Shirikisho hilo Khamis Kheri Ame(kulia) akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla 'Mabodi'(kushoto) mara baada ya kuwasili Kisiwandui kwa ajili ya ufunguzi wa Mkutano huo.


 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Dk.Mabodi akipokelewa kwa nyimbo maalum za Chama baada ya kuingia katika Ukumbi wa Mkutano wa Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Zanzibar.

 BAADHI ya Wajumbe na Wagombea wa nafasi mbali mbali katika Mkutano huo wa Uchaguzi.

Mshereheshaji  wa Mkutano huo ambaye ni Katibu wa Hamasa Mstaafu wa Shirikisho hilo pia ni Afisa wa CCM Zanzibar akisoma Utaratibu wa matukio mbali mbali ya Mkutano huo katika Mkutano huo.

 KATIBU wa Shirikisho hilo Kassim Salum Abdi akisoma taarifa ya utekelezaji katika Mkutano huo.

 MSIMAMIZI wa Uchaguzi huo Bi.Asya akifafanu jambo juu ya utaratibu wa upigaji kura.

 Mwenyekiti mstaafu wa Shirikisho hilo Khamis Kheri Ame akizungumza katika Mkutano huo.

 MAKAMU Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Tabia Maulid Mwita akizungumza na vijana wa Shirikisho hilo.

 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk. Abdulla Juma Mabodi akifugua mkutano huo na kusisitiza umuhimu wa viongozi  na wanachama  Kusoma Katiba ya CCM pamoja na Kanuni zake.
 KIONGOZI wa  zamani wa Shirikisho hilo akitoa neno la shukrani kwa niaba ya shirikisho hilo.
  




MAKAMU Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Tabia Maulid Mwita (kushoto) akipeana mkono wa pongezi na aliyekuwa Mgombea mwenza katika Uchaguzi Mkuu wa UVCCM Taifa kwa nafasi ya Makamu Mwenyekiti Thuwaiba Pandu katika Mkutano wa Uchaguzi huo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni