Jumapili, 21 Januari 2018

CCM ZANZIBAR YASEMA HAIWEZI KURUDI KATIKA MEZA YA MAZUNGUMZO NA WAPINZANI

NAIBU Katibu Mkuu wa  CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma akizungumza katika ufunguzi wa Mkutano wa Uchaguzi wa Shirikisho la Vyuo Vikuu CCM Seneti ya Unguja.



CHAMA Cha Mapinduzi CCM Zanzibar kimesema kuwa kwa sasa hawana muda tena wa kukutana na wapinzani kuzungumzia masuala ya uchaguzi na kazi iliyo mbele yao ni kupanga maendeleo.
Kauli hiyo imetolewa leo na Naibu Katibu Mkuu CCM Zanzibar Abdalla Juma Mabodi alipokuwa akifunguwa mkutano mkuu wa Shirikisho la Vyuo Vikuu Mkoa huko Ofisi Kuu CCM KIsiwandui.

Msimamo huo umetolewa na Dk. Mabodi kufuatia baadhi ya viongozi wa Chama cha CUF kupitia mikutano yao ya ndani kuwambia wafuasi wao kuwa wanatarajia kurudi katika meza ya mazungumzo na CCM kujadili uchaguzi Mkuu uliopita.

Alisema wakati ambao kulikuwa na muda wa kufanya hivyo waliwazungusha na kufikia hata kuwahangaisha wazee wao na sasa muda haupo tena na kilichobakia ni kuangalia namna gani wanaweza kukiimarisha chama na kupanga mikakati ya kuwaletea wananchi wao maendeleo.

“Hakuna mazungumzo tena kwa sasa tukutane 2020 katika uchaguzi, washaona mambo yanakwenda vizuri wanaleta vidudu mtu”, alisema Mabodi.

“Walikuja wzungu hapa ofisini kwangu nikawaambia sisi suala la uchaguzi limekwisha tunapanga maendeleao”, aliongeza Naibu Katibu Mkuu huyo.

Aidha alisema kuwa wakati huo CCM iliwatumia wazee akina Dk.Salimin na Marais wengine wastaafu pamoja na wanasiasa wakongwe wa CCM ili kuzungumzia suala hilo lakini badala yake walikimbia na kuutia mpira kwapani.

“Tuliwaita mpaka wazee wetu mkatuzungusha  sasa hivi wanataka nini hatuna muda tena na Dk. Shein huyo anapepea yupo  nje ya nchi kutafuta pesa za kuwaletea maendeleo wananchi”, alisema.

Samabamba na hilo aliwataka wana CCM wa Shirikisho hilo kujitahidi kuwa mabalozi wazuri katika kipindi hichi cha kuelekea uchaguzi mkuu kwa kuingiza wanachama wapya na kuwashaiwishi kwenda kujiandikisha katika daftari la kupiga kura wale wote ambao tayari wameshafikia umri wa
kupiga kura.

Alisema kuwa CCM pamoja na kuwa na wafanyakazi wengi ndani ya ofisi na jumuiya zao lakini bado nguvu za wanachama wa nje zinahitajika ili kuweza kukiletea ushindi.

“Kama hatujawatumia wanaCCM waliopo nje ya Ofisi zetu hatutofika mbele, lazima tutumie jeshi la wanaCCM hawa kuwaelezea watu ili kutengeneza mazingira mazuri ya ushindi”, alisema.

Hata hivyo aliwataka wanashirikisho hilo kusoma katiba na kanuni za chama na kujenga ushirikiano na viongozi wao katika kujikjenga chama na inapotokea matatizo wayatatuwe kwa kulingana na katiba na kanuni zinavyoelekeza.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni