Jumamosi, 6 Januari 2018

BARAKA SHAMTE -ASEMA MAALIM SEIF HANA JIPYA

 
 MWANASIASA Mkongwe visiwani Zanzibar  ambaye pia amewahi kuwa Katibu Mkuu wa kwanza wa Chama cha Afro-Shiraz Party iliyoungana na TANU ikazaliwa CCM, Ndugu  Baraka Mohamed Shamte.


MWANASIASA Mkongwe visiwani humu Baraka Shamte amesema Katibu  Mkuu wa CUF, Seif Sharif Hamad hana jipya na kwamba anachotakiwa  kukifanya wakati huu ni kuwapotosha  Watanzania juu ya mustakabali wa uhai wa Chama chake.

Amesema Katibu Mkuu huyo amemalizwa kisiasa na Mwenyekiti wake Profesa Ibrahim Lipumba hivyo ni ishara tosha kuwa anamuogopa  hivyo anachopaswa kukielezea muafaka wao umefikia wapi kati yao.

Akizungumza  Shamte amesema kuwa siku za hivi karibuni Maalim Seif aliitisha mkutano na waandishi wa habari na kuelezea kuwa viongozi  wanapaswa kuwasikiliza viongozi wa dini wakati kwa upande wake  ndani ya chama chake hasikilizi ushauri wa mtu.

"Maneno haya ni ya kisiasa kabisa angekuwa anasema haya ndani ya Chama chake anasikiliza ushauri tungemuona wa maana  lakini hataki ushauri alafu unaongea maneno hayo hiyo ni ishara kuwa siasa imeanza kumtupa mkono,"amesema.

Shamte ameongeza kuwa Katibu Mkuu huyo mara nyingi ameambiwa  achie uongozi kutokana na kuchokwa kwake lakini kila anayemwambia anafukuzwa unachama ndani ya chama chake hakuna demokrasia ya kweli badala yake anajifanya mfalme.

Amesema mwanasiasa huyo ndani ya chama chake hataki kuambiwa ukweli ambapo  ametaja mfano kuwa baadhi ya wanachama  wake walimshauri ashiriki kwenye uchaguzi wa marudio wa mwaka 20 lakini alikataa na kuwafukuza watu hao. Katika maelezo yake Shamte amefafanua kuwa Katibu huyo hataki ushauri ndani ya chama chake wala kusikiliza la kuambiwa badala  yake anawasikiliza wafadhili wake kutoka  baadhi ya nchi zinazounga mkono mfumo wa siasa za Kiliberali.

"Maalim Seif amechoka kisiasa hana tena jipya yeye anazua mambo ambayo  watanzania hawataki kuyasikia na kwamba wanataka kufahamu  mustakabali wa chama chake watu wanajiuliza hali yake na  Profesa Lipumba iko je kwa sasa, kuna kipindi fulani Aboubakar  ambaye  ni mwanachama wa CUF alichukua fomu katika mkutano mkuu wa kujaza fomu ya kugombea nafasi ya Katibu,  Seif alikataa na alitaka agombee pekee yake,"amefafanua  Shamte.

Mwanasiasa huyo ameeleza  kuwa ndani ya CUF hakuna demokrasia  badala ya kuzungumza mustakabali wa chama chake anasema mambo ya uongo hiyo ni dalili kuwa siasa sasa basi tena kwake.

"katika mkutano mkuu huo ambao ulifanyika Bwawani Seif  alijitangaza mshindi kabla ya kutangazwa na chama chake hivyo  akitaka kuzungumza siku nyingine mambo hayo ya kuwa viongozi  wasikilize viongozi wenzao aanze yeye kusikiliza viongozi  wenzake ndani ya chama chake,"amesema  Shamte.

Ameongeza kuwa Maalim  Seif asitake kuwadanganya watu kwa kuzungumza mambo  yasio kuwa  na  maana na kwamba Watanzania watambue kuwa  Profesa Lipumba ametwaa ubingwa wa kisiasa ndani ya CUF hali inayopelekea Maalim Seif kukosa ajenda za kuwambia wafuasi wake.

Shamte ambaye kisiasa ni mwalimu wa walimu anayestahiki kupewa heshima ya  kuwa Profesa wa siasa na historia, ameeleza kwamba kutokana na migogoro iliyokomaa ndani ya CUF  Maalim Seif anatakiwa kuachia madaraka kwa viongozi Vijana yasije kumkuta kama  yaliyotokea Zimbabwe enzi za mwisho za Rais mstaafu wa nchi hiyo  Robert  Mgabe.

“ Siasa za zama hizi Maalim Seif haziwezi tena tayari afya yake kimwili na kiakili zimechoka japokuwa kiumri kwangu ni mdogo sasa lakini kawa mzee na kuzeeka kifikra kutokana na kukumbatia  visasi,chuki na siasa za kuwachonganisha  wananchi  badala ya kuwaunganisha”,, amesema Shamte na kumshauri mwasiasa huyo ajiweke kando na siasa kutokana na kukosa sifa za kuwatumikia wafuasi wa Chama chake.







Hakuna maoni:

Chapisha Maoni