Jumatatu, 20 Agosti 2018

DK.BASHIRU AITAJA MIKAKATI YA KUKUZA UCHUMI WA CCM

 VINGOZI mbalimbali wa CCM na UVCCM wakiwa katika uwanja wa ndege wa Pemba kwa ajili ya kumuaga Katibu Mkuu wa CCM Tanzania Dk.Bashiru Ally ambaye amehitimisha ziara yake  kisiwani Pemba.

 MAKATIBU wa Idara za CCM Zanzibar  Katibu wa Kamati maalum ya NEC, Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa ambaye pia ni Mjumbe wa kamati kuu ya CCM Taifa Mwl.Kombo Hassan Juma (kushoto wa kwanza), Katibu wa kamati maalum ya NEC, Idara ya Uchumi na Fedha CCM Zanzibar ambaye  Mjumbe wa kamati kuu ya CCM Taifa Afadhali Taib Afadhali (wa pili kushoto), Katibu wa Kamati maalum ya NEC, Idara ya Organazesheni CCM Zanzibar Ndugu Bakar  Hamad Khamis (kulia) wakiwa uwanja wa ndege wa Pemba kwa ajili ya kumuaga Katibu Mkuu wa CCM Tanzania Dk.Bashiru Ally.

NAIBU Katibu Mkuu wa UVCCM Zanzibar Ndugu Shaka Hamdu Shaka(kulia) akiagana na Katibu mkuu wa CCM  Tanzania Dk.Bashiru aliyekuwa kisiwani Pemba kwa ajili ya ziara.


Katibu mkuu wa CCM  Tanzania Dk.Bashiru Ally akisalimiana na Makamu Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Tabia Maulid Mwita katika uwanja wa ndege wa Pemba. 






 Katibu wa kamati maalum ya NEC, Idara ya Uchumi na Fedha CCM Zanzibar ambaye  Mjumbe wa kamati kuu ya CCM Taifa Afadhali Taib Afadhali (kushoto) akiagana na Katibu Mkuu wa CCM Tanzania Dk.Bashiru Ally.


Katibu Mkuu wa CCM Tanzania Dk.Bashiru Ally akiwapungia mkono viongozi mbali mbali wa CCM waliokuwa uwanja wa ndege kwa ajili ya kumuaga na kumsindikiza baada ya kumaliza ziara yake na kuelekea Dar es saalam kwa ajili ya majukumu yake.



NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR.

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Dk.Bashiru Ally amesema Chama hicho kinadhibiti ubadhilifu wa mali na matumizi mabaya ya rasilimali fedha ili kijitegemee kiuchumi.

 Amesema endapo rasilimali hizo zitatumika vizuri na kuanzishwa kwa miradi mingine mikubwa ya uzalishaji wa kipato katika ngazi mbali mbali za chama na jumuiya ili ziwanufaishe wanachama wote badala ya watu wachache.

Kauli hiyo katika ziara yake kisiwani Pemba wakati akizungumza na viongozi na wanachama wa Chama cha Mapinduzi wa Mikoa Miwili katika ukumbi wa Fidel Castro uliopo, Mkoa wa Kusini Pemba.

Dk.Bashiru ameeleza kuwa lengo la kusimamia dhana ya ukuaji wa uchumi ndani ya chama kupitia vyanzo vyake vya mali na fedha ni kukiondosha chama katika mazoea ya kutegemea ufadhili wa watu wenye fedha wanaokuwa na malengo ya kujinufaisha wenyewe kisiasa.

Pia ameyataja malengo mengine kuwa ni uimarishaji wa maslahi ya watumishi wa CCM na jumuiya zake kwani bado maslahi yao ni ya kiwango cha chini ambayo hayaendani na hadhi ya taasisi yenyewe.

Ameeleza kuwa malengo hayo yakifanikiwa utakuwa ni ushindi mkubwa kwa wanachama wa CCM wote kwani tabia za rushwa na makundi ya kusaka nafasi za uongozi kwa kutumia fedha yatakuwa yamedhibitiwa.

Amewasisitiza viongozi wote wa taasisi hiyo kuunga mkono malengo hayo kwa kuhakikisha wanapunguza matumizi holela ya fedha na badala yake waanzishe miradi itakayowasaidia kujiendesha ili kulinda heshima na hadhi ya CCM mbele ya jamii.

Pamoja na hayo amezitaka taka jumuiya zote hasa ya umoja wa vijana (UVCCM) kuhakikisha wanakuwa wabunifu kwa kutumia rasilimia walizonazo kwa kuanzisha miradi mikubwa ya kilimo, uvuvi na viwanda vidogo vidogo ili vijana wajiajiri wenyewe.

Katibu Mkuu huyo Dk.Bashiru amewaka  wazi msimamo wa Chama Cha Mapinduzi kuwa wale wote waliohusika na kutapeli na kujimilikisha mali za taasisi hiyo kinyume na utaratibu wote watachukuliwa hatua za kisheria.

Naye Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Mabodi alisema wanachama wote wana haki ya kuunga mkono mambo mema yanayotekelezwa na taasisi hiyo kwa nia ya kuongeza ufanisi.

Amesema wakati wa vyama vya ukombozi vya ASP na TANU viongozi wa wakati huo walifanikiwa kupanga mambo ya maendeleo yaliyodumu kwa muda mrefu kutokana na umoja na mshikamano waliokuwa nao hasa katika masuala ya kuvijenga kimaendeleo vyama vyao.

Dk. Mabodi ameeleza  kuwa suala la uzalendo katika kusimamia maslahi ya kitaifa ni jambo muhimu hasa kwa viongozi wanaoaminiwa na kupewa dhamana za kuongoza jamii.

Akizungumzia ushindi wa CCM visiwani Zanzibar mwaka 2020 alisema mpaka sasa Zanzibar hakuna upinzani bali kuna vikundi vidogo vidogo vya watu wanaojivisha joho la upinzani wakati wao ni madalali wa kisiasa waliofilisika kifikra.

Naibu Katibu Mkuu huyo amesema  CCM itashinda kisayansi kutokana na serikali zake kutekeleza mahitaji ya wananchi wa mijini na vijijini kupitia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2015/2020.

.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni