Jumatano, 27 Desemba 2017

SHAKA-ATOA YA MOYONI KATIKA HAFLA YA MAPOKEZI YA VIONGOZI WAPYA WA UVCCM ZANZIBAR

Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa Shaka Hamdu Shaka akizungumza katika hafla hiyo

NA IS-HAKA OMAR,ZANZIBAR.


KAIMU Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa Shaka Hamdu Shaka, amesema licha ya Umoja huo kupita katika misukosuko na mawimbi makubwa ya changamoto za kisiasa na kiutawala lakini bado viongozi wake wamebaki imara na wenye misimamo isiyopinda katika kusimamia maslai ya vijana.

Hayo ameyabainisha leo wakati akizungumza katika hafla ya mapokezi ya viongozi wa UVCCM Taifa waliofika Zanzibar leo kwa mara ya kwanza toka wachaguliwe kupitia Mkutano Mkuu wa Umoja huo uliofanyika hivi karibuni.  

Shaka amesema Umoja huo umepitia katika kipindi kigumu cha misukosuko ambayo wakati mwingine iliwayumbisha baadhi ya viongozi lakini baadae wakarudi katika mstari ulionyooka kutokana na nasaha za viongozi wa CCM.

Ameeleza kuwa maendeleo endelevu ya umoja huo yataletwa na vijana wenye nia, maono na uzalendo wa kweli katika kujenga hoja zenye uhalisia wa kuisaidia jumuiya hiyo na sio kuibomoa.

“ Namshukru mungu toka nimekuwa kiongozi ndani ya umoja huu nilipoanzia Zanzibar hadi kuteuliwa na kuhamishiwa Tanzania bara kwa wanaoijua UVCCM nilivyoikuta wanakiri kuwa kwa sasa ina maendeleo kuliko ilivyokuewa wakati wa nyuma.”, amefafanua Shaka.

Shaka amesema huu sio wakati wa maneno na porojo bali ni muda mwafaka wa kila kijana kutumia elimu, maarifa na mbunu mbadala katika kuishauri jumuiya iweze kufanya mambo mazuri yenye tija kwa maslahi ya Chama na Taifa kwa ujumla.

Ameahidi kuwa ataendelea kushirikiana na vijana wote bila kujali tofauti za kijinsia, umri, rangi,kabila na dini kwa lengo la kuhakikisha malengo ya UVCCM yanatimia kwa asilimia 100 kabla ya mwaka 2022.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni