Jumatatu, 18 Desemba 2017

MATUKIO KATIKA PICHA MKUTANO MKUU WA TISA WA CCM TAIFA UNAOFANYIKA DODOMA-2017.

VIONGOZI wakuu wa Chama cha Mapinduzi(CCM) wakiwa katika Mkutano Mkuu wa Tisa wa CCM ambao ni Maalum kwa uchaguzi wa viongozi wa ngazi ya taifa ndani ya taasisi hiyo unaofanyika ukumbi wa JK Dodoma.
WAJUMBE wa Mkutano Mkuu wa Tisa wa CCM Taifa wakiwalaki viongozi mbali mbali katika mapokezi ya viongozi wakuu wa Chama cha Mapinduzi.

BAADHI ya Wazee  wa Chama cha Mapinduzi walioudhuria Mkutano Mkuu.

 MKUU wa Mkoa wa Njombe Chrispher Ole Sendeka(kushoto) akisalimiana na Katibu Mkuu mstaafu wa CCM, Mzee January Makamba (kulia).

 MANAIBU Makatibu wakuu wastaafu wa Chama cha Mapinduzi wakifuatilia matukio mbali mbali yanayoendelea katika Mkutano huo.

 Baadhi ya Wajumbe wa Mkutano Mkuu huo kutoka Zanzibar wakiwa katika Mkutano Mkuu huo.

 

 VIONGOZI wa Vyama vya upinzani walioalikwa katika Mkutano Mkuu huo kwa lengo la kuongeza mahusiano ya kisiasa.

 BAADHI ya wake wa viongozi walioshiriki katika mkutano huo.

 BAADHI ya Maspika wastaafu wa Bunge la  Jamhuri ya muungano wa Tanzania na Baraza la wawakilishi Zanzibar wakibadilishana mawazo katika Mkutano Mkuu wa tisa wa CCM Taifa.

 WAJUMBE wa Baraza la Wadhamini la Chama cha Mapinduzi walioshiriki katika Mkutano Mkuu huo.

 BAADHI ya wanachama na viongozi wa zamani wa vyama vya upinzani waliojiunga na CCM hivi karibuni.

 Baadhi ya waalikwa kutoka taasisi za elimu ya juu na makundi maalum walioudhuria mkutano huo

 
 KATIBU Mkuu wa CCM Taifa, Abdulrahman Omar Kinana akitoa taarifa ya utekelezaji ya chama cha mapinduzi ya miaka mitano iliyopita.

 BAADHI ya wasanii wa Bongo movie ambao ni wanachama wa CCM walioshiriki katika Mkutano Mkuu huo.

 MAKAMU Mwenyekiti wa  UVCCM Taifa, Tabia Maulid Mwita akiwa ni miongoni mwa wajumbe walioshiriki Mkutano Mkuu huo. 
 KUNDI la wagombea wa NEC, viti 15 kutoka Zanzibar.


 MWENYEKITI wa Baraza la vyama vya siasa Tanzania, John Shibuda akitoa salamu za vyama hivyo katika mkutano Mkuu huo.

 Mwanasiasa Mkongwe wa Chama cha UDP, Mzee John Cheyo akizungumza katika mkutano mkuu huo.


 BAADHI ya Wajumbe na Wagombea wa nafasi mbali mbali za uongozi kwa ngazi ya taifa wakifuatilia mkutano Mkuu huo.
 WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa akisoma taarifa ya utekelezaji ya Serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania.
 MAKAMU wa Pili wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapiduzi, Balozi Seif Ali Idd akisoma taarifa ya utekelezaji kwa upande wa  Zanzibar.

 BAADHI ya wagombea wa kundi la NEC, viti 15 kutoka Zanzibar.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni