Ijumaa, 29 Desemba 2017

MAKAMU MWENYEKITI WA UVCCM TAIFA TABIA MWITA-AMTEMBELEA MWANAMAPINDUZI RAMADHANI HAJI FAKI.

 MWASISI wa Mapinduzi ya Zanzibar ya Mwaka 1964, Brigedia Jenerali Mstaafu  Ramadhani Haji Fakii(kushoto) akizungumza na Makamu Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Tabia Mwita(kulia) alipofika nyumbani kwake Maisara Unguja kwa ajili ya kumtembelea.


NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR.

MAKAMU wa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Tabia Mwita amemtembelea  Brigedia Jenerali mstaafu Ramadhani Haji Faki, ambaye ni miongoni wa wanamapinduzi 14 waliofanikisha  Mapinduzi ya mwaka 1964.

Brigedia Jenerali  Faki  kati ya wanapinduzi  hao 14 ndiye  aliyebakia hai na pia alikuwa Waziri Kiongozi wa kwanza katika Baraza la Mapinduzi  baada ya Mapinduzi hayo kutokea.

Akizungumza  nyumbani kwake baada ya kutembelewa na Makamu huyo Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Tabia, Mwanapinduzi huyo amesema kuna umuhumi wa kuhakikisha vijana wa sasa kuyaenzi na kulinda dhana ya mapinduzi hayo yaliyotekelezwa na vijana wa enzi za ASP.

"Nilimwambia Mzee Abeid Amani Karume kuwa lazima tuipindue serikali ya Sultan kwani ilikuwa wakiwadhalilisha  Waafrika ambao ni wazawa  na namshukru mungu mipango yetu ikafanikiwa  toka mwaka 1964 Zanzibar ilikuwa huru kiuchumi, kijamii, kimaendeleo na kisiasa.,"alisema.

Mwanapinduzi huyo amesema  baada ya kuipindua serikali ya Kisultani serikali ya Mapinduzi ilitangaza kuwa elimu ni bure na wananchi walihimizwa kusoma kutokana uamuzi wa serikali ya mapinduzi kutangaza bure ili kupata wataalamu wa kuiletea nchi maendeleo.

Faki alimtaka Makamu Mwenyekiti huyo ambaye ni kamanda mkubwa wa vijana Tanzania kuhakikisha vijana nchini wanapaswa kuyalinda kwa hali na mali.

"Sidhani kuwa kama kuna mtu atakuja kuyapindua Mapinduzi haya na kwamba labda ayafanyie nchi nyingine na si Zanzibar mapinduzi haya ni ya mwisho na sifikiri tena kama kuna mtu atakuja kuyafanya mapinduzi mengine,"alisema Faki.

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti huyo Tabia, amemuhakikishia Mwanapinduzi huyo kuwa UVCCM itahakikisha yanayalinda  mapinduzi hayo ambayo yalitokea mwaka 1964.

Amesema  amejifunza mambo mengi kutoka kwa mwanamapinduzi huyo ambapo amebaini umuhimu wa kuwatumia vijana kuwafunza kuwa katika hali ya uimara na uzalendo mkubwa kwa kuyalinda mapinduzi hayo.

"Nikiwa mimi ni Makamu Mwenyekiti wa UVCCM,ninawaeleza vijana wenzangu kuwa hakutatokea Mapinduzi yeyote isipokuwa kuyaendeleza na kuyawekea mipango ya kufanya  kuleta maendeleo,"alisema

Makamu huyo amesema kupitia UVCCM mpya ambayo ni imara itaendelea kuyadumisha na kwamba yasifanyike mambo yakaleta fikra ya kutokea kwa mapinduzi mengine wakati yalishafanyika kwa mwaka 1964.

"Leo nimeona na nimesisimuka sana baada ya kupata historia ya kutokea kwa mapinduzi haya na kwamba yalikuwa lazima kutokea kutokana na unyama wa serikali ya Sultani aliyafanya na udhaifu wa kuongoza serikali,"alisema.

Tabia amefafanua  kuwa amekuja kujifunza taarifa za ndani za mahusiano ya ndani kati ya Chama Cha Mapinduzi(CCM), kilipotoka na kinapoelekea na kutoka Chama cha Afro shiraz Party (ASP) na TANU hadi CCM na kwamba elimu aliyopata ni umuhimu wa uzalendo kwa vijana katika kutetea nchi kwa kujitolea.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni