Jumatano, 27 Desemba 2017

PICHA MBALI MBALI ZA MAPOKEZI YA MWENYEKITI NA MAKAMU MWNYEKITI WA UVCCM ZANZIBAR

AFISA kutoka Idara ya Itikadi na Uenezi Asha choum (kulia wa mwanzo aliyevaa mtandio wa rangi ya kijani) akitoa historia ya aliyekuwa Rais wa kwanza wa Zanzibar  Marehemu Mzee Abeid Karume kwa Msafara wa viongozi wapya wa UVCCM Taifa wakiongozwa na Mwenyekiti Kheir James na Makamu Mwenyekiti Tabia Mwita, katika eneo la kumbukumbu ambayo aliuwawa kiongozi huyo na wapinga maendeleo akiwa katika eneo la kucheza mchezo wa dhumna hapo Afisi Kuu ya CCM  Kisiwandui Zanzibar.

 VIONGOZI mbali mbali wa UVCCM pamoja na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk. Abdalla Juma Mabodi wakiomba dua katika Kaburi la Marehemu Mzee Abeid Amani Karume lililopo katika  eneo la Afisi Kuu ya CCM Zanzibar 

MSAFARA wa viongozi hao wakitoka katika kaburi la marehemu Mzee Karume mara baada ya kuomba dua. 

 MWENYEKITI wa UVCCM Taifa Kheir James(kushoto wa kwanza)  akitoa Shukrani kwa mapokezi aliyopewa na Uongozi wa Chama cha Mapinduzi Zanzibar pamoja na SMZ kupitia Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Ayoub Mohamed kama wanavyoonekana katika picha hiyo.

 MWENYEKITI  wa UVCCM Kheir James na Makamu Mwenyekiti Tabia Mwita wakivishwa sikafu na vijana wa Chipukizi mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Gymkhana.

 BAADHI ya vijana wa UVCCM waliobeba mabango yenye picha za viongozi wa UVCCM katika mapokezi hayo.

 MWENYEKITI wa UVCCM Taifa akisalimiana na viongozi na wanachama wa UVCCM na CCM kwa ujumla.



VIONGOZI wa UVCCM wakiwa meza kuu mara baada ya kuwasili katika ukumbi wa Gmkhana.






 VIONGOZI wa UVCCM Taifa Makamu Mwenyekiti Tabia Maulid(kushoto) pamoja na Mwenyekiti wa UVCCM Taifa wakivishwa maua maalum yanayobeba utamaduni wa Zanzibar ikiwa ni ishara ya kuwakaribisha visiwani humo.

 MWENYEKITI akipewa jezi na sikafu ya Zanzibar Heroes akiwa ni ishara ya kuwa ni mdau wa Soka la Zanzibar


 MAKAMU Mwenyekiti Tabia Mwita akipewa zawadi maalum iliyopo kwenye chupa ambayo ni zawadi maalum ya kumkaribisha nyumbani.

 BAADHI ya viongozi wa UVCCM na Jumuiya zingine za CCM Zanzibar.

 Kaimu Katibu Hamasa wa Chipukizi wa Umoja wa Vijana waChama cha Mapinduzi (UVCCM) Jokate Mwongelo.

 KAIMU Naibu Katibu Mkuu wa UVCCM Zanzibar Abdulghafari Idrissa Juma akizungumza katika mapokezi hayo.

 MAKAMU Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Tabia Maulid Mwita akizungumza katika hafla ya  mapokezi hayo kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti.

Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa Shaka Hamdu Shaka akizungumza katika hafla hiyo

 MWENYEKITI wa UVCCM Taifa Kheir James akiwahutubia vijana wa UVCCM katika hafla hiyo.

 BAADHI ya viongozi wakongwe( MACOMRADE) wa Zamani wa UVCCM ambao kwa sasa ni viongozi wa Chama na Jumuiya zingine za CCM wakiwa katika hafla hiyo.



 BAADHI ya viongozi wa UVCCM walioudhuria katika hafla hiyo wakisoma dua.

VIONGOZI wa UVCCM wakisoma dua ya kuhitimisha hala hiyo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni