Jumamosi, 16 Desemba 2017

DKT.TULIA-ATOA DOZI KWA UWT, ASISITIZA MSHIKAMANO KWA AKINA MAMA.

NAIBU Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Dkt. Tulia Ackson Mwansasu akizunguma katika hafla ya kuwakaribisha viongozi wapya wa UWT Taifa Mjini Dodoma.

NA IS-HAKA OMAR, DODOMA.

NAIBU Spika wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Tulia Ackson Mwansasu amesema UWT itavuka vikwazo vya kisiasa na kiuchumi endapo viongozi na watendaji wa umoja huo wa ngazi za juu  watakuwa tayari kufanya kazi kwa ushirikiano na viongozi wa ngazi za chini.

Rai hiyo ameitoa leo wakati akizungumza katika mapokezi ya viongozi wa UWT ngazi ya Taifa yaliyofanyika leo katika viwanja vya White house Makao Makuu ya CCM Dodoma.

Amesema umoja na mshikamano ndio nyenzo ya kuimarisha Umoja huo wenye jukumu la kuwaunganisha wanawake na kusimamia malezi ya vijana hasa wa kike.

Amewasihi wanawake nchini kuwa mstari wa mbele katika kuunga mkono mafanikio yanayoletwa na usimamizi mzuri wa Sera imara za CCM.

" Wanawake ni hazna ya CCM kisiasa na kiuchumi hivyo tuonyeshe uwezo wetu kama tunaweza kweli kuleta maendeleo endelevu wenyewe bila ya kusimamiwa na mtu yeyote bali tujiongoze na kujisimamia wenyewe", amesema Dkt.Tulia.

Mwanataaluma huyo wa Sheria ameeleza kwa kuongeza kwamba anaona ishara ya mafanikio kupitia viongozi wa UWT waliochaguliwa kwa ngazi zote hasa taifa kwani wote ni wachapakazi na wenye wivu wa maendeleo.


Amewakumbusha  Akina mama hao kuwa mara baada kupatikana viongozi hao kazi iliyobaki ni kuijenga UWT ili iwe kituo cha matumaini ya Wanawake wa Tanzania nzima. 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni