Alhamisi, 14 Desemba 2017

MWENYEKITI MPYA WA UVCCM AAGIZA UHAKIKI WA MALI ZA JUMUIYA UANZE MARA MOJA

 MWENYEKITI wa UVCCM Taifa Kheir Denice James akihutubia katika hafla ya mapokezi ya viongozi wapya wa Umoja huo ngazi ya Taifa yaliyoandaliwa na UVCCM Mkoa wa Dodoma.

NA IS-HAKA OMAR, DODOMA.
MWENYEKITI mpya wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM ) Kheir Denice James amesema atahakikisha anasimamia kwa nguvu zake zote  madhumuni, kanuni, dira na malengo ya jumujiya kipindi cha mwaka 2017 hadi 2022 kwa nia ya kuleta ustawi na mageuzi mukubwa ndani ya UVCCM.
Amesema anajua kuwa ada na ujira wa kusema kweli huwa haupendwi na wengi ila yeye huona raha na fahari kusema kweli hata kama ukweli huwa unauma.
Mtamshi hayo ameyatoa jana kwenye hafla fupi alipozungumza na wana UVCCM  kwenye viunga vya Makao Makuu ya CCM White House mkoani hapa.
Kheir alisema mpango na mkakati wa serikali katika utoaji wa asilimia 5 kwa vijana na wanawake si hisani wala fadhgila hivyo halmashauri ambazo bado zinasuasiuua katika utoaji wa fedha hizo zihakikishe zinatimiza wajibu huo.

Alisema ikiwa mkurugenzi wa halmashauri yoyote nchini anaona uzito wa kutoa asilimia hizo kwa vijana na wanawake ni viziri akamueleza Raia kama kazi aliyopewa imemshinda ili aqweze kukaa pembeni.

"Asilimia hizo lazima zitoke ili kuwasaidia vijana kujiendelkeza kimiradi na kujipatia vipato vyuao kiuchumi.Ikiwa tutaamua kunyamaza iko siuku tutyapigwa mawe kwa kushindwa kuwasaidia vijana wakati serikali imeweka utaratibu mzuri wa utoaji wa mikopo hiyo" Alisema Kheir.

Aidha aliwapongeza wajumbe wa mkutano mkuu wa UVCCM kwa uwamuzi wao wa kumchagua na kuwa Mwenyekiti wa jumujiya ya Vijana ya chama cha mapinduzi huku akipiga marufuku kwa mwanachama asiye na dhamana ya kimamlaka kuisemea jumuiya.

Mwenyekiti huyo mpya wa UVCCM alisesma kuanzia sasa kiongozi atakayekuwa akiisemea jumuiya ni yule mwenye mamlaka ya kikanuni na kikatioba akiwemo Mwenyekiti wa jumuiya , katibu mkuu,Makamu mwenyeiti ,wenyeviti wa mikoa na wilaya sio vinginevyo.

Pia aliwataka vijana ambao bado wako upinzani kurudi haraka ndani ya chama tawala kwani kubaki kwao nje hakjuitaweza kuwasaidia kutokana na vyama vyao kuwa vichanga na havina uwezo wa kuiondoaha ccm madarakani.

"Asiyeungana na CCM sasa ni kama mtu anayepishana na gari lenye mishahara.Yeye wakati anatokna nje gari la mishahara linaingia ndani,Tutaendelea kuwaeleimisha vijana wenzetu kewas kusimamia malengo yretu,kuonyesha umoja,mshikamano bila ya kugonganagongana"Alieleza Kheir.

akizungumzia rasilimali na mali za chama ,Mwenyekiti huyo wa UVCCM alisema kabla makao makuu haijaikagua mikoa ,wilaya na kata watendaji katika ngazi hizo ni vyema wakajikagua wao wenyewe na kuaninisha ipo miradi mingapi,majengo na vitega uchumo.

"Nataka kujua mali,vitega uchumi  na  rasilimali za jumuiya kuanzia zanzibar hadi Tanzania Bara na kila kitu kionyeshwe  kinavyozalisha tija na faida zake kwa njia za uwazi bila kujkjitokeza ubabaishaji"Alisisitiza.

Hata hivvyo alisema wakati wa  aina ya wanachama vibaraka na wasaliti kubaki ndani ya chama au kwenye jumnuiya za chama umekwisha hivyo ni lazima wajulikane na kutoswa mara moja.kweani wakiachwa ni hatari kwqa chama na utawi wake.

Akielezea suala la kuimarisha nidhamu na maadili,Kheir alisema wale wote ambao wanakishambulia chama kwenye mitandao ya kijamii kwasababu za kipuuzi ili kukidhoofisha wa watanyooshwa kwa kutiwa adabu.

"Hiwezekani mtu awe analipwa mshahara na serikali za ccm au jumuiya zake kisha yeye awe kiranja wa kukivuruga chama au jumuiya kwa kuandika uopngozo na uzushi kwenye mitandao na mtu huyo aachwe akitamba"Alionya.


Kwenye hafla hiyo jumla ya wanachama 200 toka vyama vya upinzani wengi wakiwa ni kutoka ACT Wazalendo,Chadema na CUF wamejiunga na CCM na kupewa kadi mpya za uanachgama akiwemo aliyekuwa Afisa wa kitengo cha sheria ACT Wazalendo Mwamtumu Mgonja na Mkurugenzi wa siasa wa chama hicho Mkoa Mara Pascal Warioba.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni