Ijumaa, 22 Februari 2019

WALIMU,WAZEE NA WALEZI WATAKIWA KUFUATILIA MIENENDO YA WANAFUNZI.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiweka Jiwe la Msingi na kufungua Shule ya Sekondari ya Michenzani iliyopo katika Jimbo la Mkoani Pemba katika ziara yake ya kuweka mawe ya msingi, kuzindua na kukagua miradi mbali mbali inayotekelezwa katika Wilaya ya Mkoani.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akikagua darasa lenye viti na meza za kisasa zilizonunuliwa nchini China na SMZ kwa lengo la kupunguza tatizo la upungufu wa madawati katika shule za msingi na Sekondari  nchini.

VITI na Meza za kisasa zitakazotumiwa na wanafunzi katika madarasa yaliyozinduliwa katika Shule ya Sekondari Michenzani Pemba.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na wananchi,wanafunzi na viongozi mbali mbali mara baada ya kuzindua madarasa ya kisasa kaika Skuli ya Sekondari Michenzani iliyopo Wilaya ya Mkoani Pemba.

NAIBU Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe.Mmanga Mgengo kitoa ufafanuzi wa mipango endelevu ya Serikali katika kuimarisha Sekta ya Elimu nchini huko katka hafla ya uzinduzi wa Skuli ya Ssekondari Michenzani.

MJUMBE wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Ndugu Lailah Burhan Ngozi pamoja na viongozi mbali mbali wa Chama na Serikali wakiwa Katika Hafla ya ufunguzi wa Shule ya Sekondari Michenzani Pemba iliyozinduliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein.

MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa Kusini Pemba Mhe.Faida Mohamed Bakari (aliyevaa nguo ya njano ya CCM akiwa na miwani) pamoja na viongozi mbali mbali katika hafla ya uzinduzi wa madarasa ya Sekondari Michenzani.

MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa ndugu Mwanamkasi Rajab Aziz(aliyevaa mtandio mweusi) pamoja na wananchi mbali mbali wakiwa katika hafla ya uzinduzi wa madarasa ya shule ya Sekondari Michenzani Wilaya ya Mkoani Pemba.

NAIBU Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar ndugu Madina Mjaka akitoa maelezo ya kitaalamu juu ya ujenzi wa madarasa hayo katika shule ya Sekondari Michenzani.

MWALIMU Mkuu Masaidizi Shule ya Sekondari Michenzani Pemba Mwl.Wanu Is-haka Ngwali akizungumza katika Kipindi Maalum Cha 'KUTOKA KISIWANDUI' kinachofuatlia matukio mbali mbali katika ziara nzima ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein Kisiwani Pemba.

BAADHI ya Wanafunzi wa Shule ya Sekondari na Msingi ya  Michenzani Pemba wakiwa katika hafla ya ufunguzi wa majengo mbali mbali katika shule hiyo,

NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Mabodi akisalimiana na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Dk.Ali Mohamed Shein mara Baada ya Kuwasili katika uzinduzi wa majengo ya shule ya Sekondari Michenzani Pemba.
(PICHA NA KITENGO CHA HABARI NA MAWASILINO AFISI KUU CCM ZANZIBAR)

NA IS-HAKA OMAR,PEMBA.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekitii wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, amewakumbusha wazazi,walezi kushirikiana na walimu katika kufuatilia mienendo ya watoto wao pindi wanapokuwa shule na majumbani ili viwango vya ufaulu viongezeke zaidi. 

Dk.Shein amesema kwamba wanafunzi wanahitaji uangalizi wa hali ya juu kwa kila madau wa elimu ili kuhakikisha wanapata elimu bora na yenye kiwango kinachostahiki ili wafaulu vizuri katika mitihani yao ya shuleni na ya kitaifa kwa ujumla.

Rai hiyo ameitoa Dk.Shein katika  ufunguzi wa jengo la skuli ya sekondari Michenzani, Wilaya ya Mkoani Pemba, ikiwa ni ziara yake ya kwanza katika Wilaya za Pemba mara baada ya kuhitimisha ziara yake kwa upande wa Unguja.

Dk.Shein ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, ameeleza kuwa elimu bora na viwango bora vya ufaulu wa wanafunzi wa ngazi mbali mbali za kielimu vitaongezeka endapo wananchi wataamua kushirikiana ipasavyo na Sekta ya elimu kwa kuwajengea watoto mazingira Rafiki ya kupenda kusoma kwa bidi.

Amesema walimu wana dhima kubwa katika kuwaendeleeza kielimu ya wanafunzi, hivyo akawataka kujikita katika kusomesha kwa kuzingatia maadili ya kazi zao.

Ameeleza kuwa  maendeleo ya nchi yoyote ile hutegemea upatikanaji wa elimu bora kwa wananchi wake, hivyo akasisitiza haja ya walimu kujikita katika ufundishaji na kuepuka kasoro zinarudisha nyuma kiwango cha elimu.

Amewasihi wanafunzi hao kusoma kwa bidi huku wakiepuka kufanya kazi au biashara hali ya kuwa wao bado ni wanafunzi. 

Amesema ni kazi ya Serikali kuwajengea mazingira bora wanafunzi kwa kuwapatia huduma zote muhimu, ikiwemo vifaa na madawati.

Ameeleza kuwa Serikali kununua madawati 44,000 kutoka nchini China, na kubainisha kuwa nusu ya samani hizo zimewasili na kugawiwa katika skuli mbali mbali Unguja na Pemba.

Naye Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe.Mmanga Mjengo Mjawili amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeandaa mazingira bora ya kuwezesha wanafunzi kusoma kwa utulivu bila ya kuwepo na kikwazo chochote hatua inayotakiwa kupongezwa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni