Jumapili, 24 Februari 2019

MATUKIO KATIKA PICHA ZIARA YA DK.SHEIN WILAYA YA MICHEWENI AKIKAGUA MACHIMBO YA MCHANGA HUKO SHUMBA VIAMBONI PEMBA.


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akikagua eneo jipya la Shumba Viamboni  linalochimbwa Mchanga katika Wilaya ya Micheweni Pemba katika mwendelezo ya ziara yake ya kukagua Utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2015/2020  katika Wilaya Mbali Mbali za Unguja na Pemba.

KATIBU Mkuu Wizara ya Kilimo,Maliasili, Mifugo na Uvuvi Mhe.Mariam  Juma Mabodi(aliyevaa mtandio wa rangi nyekundu),akitoa maelezo juu ya uchimbaji wa mchanga katika eneo hilo la Shumba viamboni  katika Wilaya ya Micheweni Pemba.

ENEO Mmaalum la Shumba viamboni linalochimbwa mchanga kwa ajili ya matumizi mbali mbali ya ujenzi na n.k huko Wilaya ya Micheweni Pemba.

VIONGOZI mbali mbali wa SMZ na CCM wakiwa katika ziara ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein katika ziara yake ya kukagua machimbo ya Mchanga huko Shumba Viamboni.

VIONGOZI mbali mbali wa CCM wakiwa katika ziara ya Dk.Shein huko katika machimbo ya mchanga ya Shumba Viamboni Wilaya ya Micheweni Pemba.

VIONGOZI mbali mbali wa CCM wakiwa katika ziara ya Dk.Shein huko katika machimbo ya mchanga ya Shumba Viamboni Wilaya ya Micheweni Pemba.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni