Ijumaa, 22 Februari 2019

VISIWA VIDOGO VIDOGO PEMBA NA UNGUJA KUPATA VIVUKO VYA KISASA.


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na viongozi wa Wilaya ya Mkoani na Chama Cha Mapinduzi katika Majumuisho ya ziara yake huko Skuli ya Sekondari ya Mohamed Juma Pindua.

NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Mabodi akitoa salamu za CCM katika majumuisho hayo.


KATIBU wa CCM Wilaya ya Mkoani Mohamed Ali Abdalla akisoma taarifa ya CCM katika majumuisho hayo.

BAADHI ya Viongozi mbali mbali wa CCM wakiwa katika majumuisho hayo.

BAADHI ya Maziri wa SMZ wakiwa katika majumuisho ya ziara ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein katika Wilaya ya Mkoani Pemba.

WAZEE wa Chama Cha Mapinduzi Pemba wakiwa katika majumuisho.


 NA IS-HAKA OMAR, PEMBA.

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Zanzbar Dk.Ali Mohamed Shein,a mesema serikali inaendelea na juhudi za kutafuta vivuko vya kisasa vyenye uwezo wa kuwavusha kwa usalama wananchi wanaoishi katika visiwa vidogo vidogo Pemba na Unguja.

Amesema mipango hiyo inaendelea kwa umakini Zaidi wa kupata vivuko hivyo vilivyokuwa katika viwango vya kimataifa ili wananchi wa visiwa vyote wawe na uhakika wa usafiri wa baharini.

Ameeleza kuwa mkakati huo unaenda sambamba na uimarishaji wa ulinzi wa maeneo yote ya Bahari, kikosi  cha KMKM kwa lengo la kudhibiti uhalifu na magendo katika maeneo ya bahari.

Dk.Shein ameeleza kwamba fursa hizo zinatokana na utekelezaji mzuri wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM, inayoangazia kumaliza changamoto zote zinazowakabili wananchi ili kujenga taifa imara lililoendelea kiuchumi na kijamii.

Amefafanua kwamba CCM imekuwa ni taasisi yenye viongozi waadilifu wanaoahidi na wakatekeleza kwa vitendo masuala mbali mbali yayosaidia jamii bila ya kuwabagua watu kidini na kikabila.

Ameeleza kwamba kabla ya mwaka 2020 Zanzibar itakuwa ni miongoni mwa Nchi ya Visiwa yenye maendeleo ya kupigiwa mfano katika Nyanja mbali mbali za kiuchumi, kisiasa na kimaendeleo.

Amewambia baadhi ya Viongozi na watendaji wa Serikali kuwa asiyeweza kutekeleza Ilani ya CCM huyo atakuwa hatoshi kuwa kiongozi hivyo ni bora akajiondoa mapema katika nafasi anayoitumikia.

Ameeleza kwamba kwa sasa Chama kinahitaji viongozi wabunifu na wachapakazi ili kwenda sambamba na Sera imara za kukuza uchumi wa Nchi.
Alisoma taarifa ya utekelezaji wa majukumu mbali mbali ya CCM katika Wilaya hiyo Katibu wa CCM Wilaya ya Mkoani Mohamed Ali Abdallah, amesema kutokana na utekelezaji mzuri wa Ilani ya CCM, umekuwa ni kivutio kikubwa cha wanachama wengi wa upinzani kisiwani Pemba wakiwemo vigogo kujiunga na CCM.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mkoani Mhe,Issa Juma Ali,akisoma taarifa ya Wilaya hiyo ameeleza kuwa Serikali imetekeleza kwa ufanisi masuala mbali mbali yakiwemo kuimarisha Sekta za Afya, Elimu, Kilimo,Uvuvi, Mazingira na miundombinu ya Majini na Nchi Kavu.

Akitoa salamu za CCM Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Dk.Abdulla Juma Mabodi ameeleza Chama kinaridhishwa na kasi ya kiutendaji kwa upande wa Serikali na Chama kwa ujumla.

Amesema kazi iliyobaki kwa sasa ni kila mwanachama kujipanga vizuri katika kuhakikisha CCM inashinda katika majimbo yote yaliyomo katika Wilaya hiyo.







Hakuna maoni:

Chapisha Maoni