Jumamosi, 2 Februari 2019

NDG.CATHERINE : ATOA MAAGIZO MAZITO KWA TAWI LA CCM BAMBI, APOKEA WANACHAMA WAPYA 93.




 KATIBU wa Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar Catherine Peter Nao akitoa kadi kwa mwanachama mpya huko Tawi la CCM Bambi.

 
 KATIBU wa Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar Catherine Peter Nao akitoa kadi kwa mwanachama mpya huko Tawi la CCM Bambi.


 WANACHAMA wapya 10 waliopokea kwa niaba ya wenzao 93 wa CCM wakila kiapo cha uanachama mara baada ya kukabidhiwa kadi hizo.

  KATIBU wa Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar Catherine Peter Nao akiwahutubia wanachama wa CCM katika Tawi la CCM Bambi.

 KATIBU wa CCM Tawi la Bambi Said Hussrin Haji akisoma risala ya Tawi hilo.


NA IS-HAKA OMAR,ZANZIBAR.

KATIBU wa Kamati Maalum ya NEC,Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar Ndugu Catherine Peter Nao ameagiza uongozi wa Tawi la CCM Bambi Wilaya ya Kati Unguja kuanzisha Darasa la Itikadi kwa Vijana wa mbali mbali wa Tawi hilo.

Agizo hilo amelitoa leo katika hafla ya kuwakabidhi kadi za CCM wanachama wapya 93 waliojiunga na CCM kupitia Tawi hilo.

Amesema kila kijana wa CCM anatakiwa kupikwa kiitikadi, kiuongozi na kisiasa katika madarasa ya itikadi hivyo Tawi la Bambi na Matawi mengine ndani ya Mkoa wa Kusini Kichama Unguja yasiyokuwa na madarasa hayo wayaanzishe.

Ameeleza kwamba mwanachama mzalendo, mwadilifu na mchapakazi lazima apitie katika madarasa hayo yanayotoa elimu ya siasa na historia halisi ya Zanzibar na Chama cha Mapinduzi kwa ujumla.

Aidha ameeleza kuwa Serikali ya Awamu ya Saba chini ya Uongozi wa Rais wa Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein imetekeleza Ilani ya CCM ya mwaka 2015/2020 kwa ufanisi mkubwa mijini na vijini.

Katika maelezo yake Katibu huyo, amesema miundombinu ya Barabara za viwango vya lami , umeme,afya, elimu, maji safi na salama,kilimo, uvuvi vyote vimeimarika katika maeneo mbali mbali ya mijini na vijijini.

Amesema CCM chini ya Mwenyekiti wake ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.John Pombe Magufuli ameendelea kusimamia kwa vitendo siasa za maendeleo zinazoelekeza Chama kufanya siasa na uchumi.

Aidha amewasisitiza wanawake na vijana wa Bambi kuchangamkia fursa za ujariamali kwa kuanzisha vikundi mbali mbali ili waweze kupewa mikopo yenye masharti nafuu kutoka Serikalini na wajiajiri wenyewe.

Ndugu Catherine amewakumbusha amewataka wanachama wapya kuhakikisha wanalipia kwa wakati kadi zao pia wajifunze masuala mbali mbali kwa kusoma miongozo na kanuni za CCM.

Aidha amewambia wanachama hao kuwa kwa sasa CCM ipo katika wiki ya maadhimisho ya Sherehe za kuzaliwa kwake ambapo inatimiza miaka 42 toka kuasisiwa kwake kutoka katika Vyama vya Ukombozi vya ASP na TANU.

Naye Mwenyekiti wa Tawi hilo ndugu Silima Haji Vuai amesema bado wanaendelea na mikakati mbali mbali ya kukiimarisha chama hicho  ili kulinda historia halisi ya Kijiji cha Bambi ambacho ni miongoni mwa mashina na chimbuko la harakati za ukombozi wa Chama cha ASP.

Akisoma risala Katibu wa Tawi hilo,Ndugu Said Hussein Haji amesema kijiji cha Bambi na maeneo jirani wameimarika kisiasa na bado wanaendeleo kuongeza wanachama wapya ili kwenda sambamba na maelekezo ya Chama.

Kupitia hafla hiyo Chama Cha Mapinduzi kimevuna wanachama 93 na wamekabidhiwa kadi wanachama 10 kwa niaba ya wenzao.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni