Jumatano, 13 Februari 2019

DK.SHEIN AWATAKA WAJASIRIA MALI WA KUKAUSHA DAGAA BUBUBU KIHINANI KUTENGENEZA BIDHAA ZITAKAZOUZIKA SOKO LA DUNIA.



 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akizindua Kituo cha Kuanikia Dagaa cha Bububu Kihinani.

 MKUU wa Mkoa Mjini Magharibi Mhe.Ayoub Mohamed Mahmoud akitoa ufafanuzi namna Serikali inavyowasaidia wananchi wanaojiajiri wenyewe katika eneo hilo.
Dagaa linalokaushwa na kuuzwa na wajasiriamali katika eneo la Bububu Kihinani.

 MKURUGENZI wa Baraza la Manispaa Magharibi 'A'  ndugu Amour Ali Mussa akisoma taarifa ya maendeleo ya eneo hilo la kukausha Dagaa.
 
 BAADHI ya Wananchi waliojiajiri katika eneo hilo uko Bububu Kihinani wakisikiliza hotuba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi aliyefika katika eneo hilo.


NA IS-HAKA OMAR,ZANZIBAR.
WANANCHI waliojiajiri katika ujasiriamali wa kukausha na kuuza dagaa katika eneo la Bububu Kihinani, wametakiwa kufanya kazi zako kwa kufuata taratibu za Kisheria.
Wito huo umetolewa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein mara baada ya kuzindua kituo cha kukaushia Dagaa, huko Bububu Kihinani Unguja.
Amewasihi wananchi hao kuwa Serikali inawajali na kuwathamini hivyo waendelee kufuata sheria za nchi ili waweze kunufaika na fursa mbali mbali kutoka Serikalini.
 Amewataka wajasiriamali hao kuendelea na shughuli zao na kuuza bidhaa zilizo bora ndani na nje ya nchi bila ya woga.
Ameeleza kuwa Zanzibar imebarikiwa kuwa na bahari yenye rasilimali kadhaa, hivyo ni vyema ikatumika katika kuwakomboa wananachi kuoka katika lindi la umasikini.
Amewataka kuuza dagaa bora litakalokubalika katika soko la Dunia na sio Afrika mashariki na nchi jirani pekee.
Ameiagiza Wizara ya kilimo, Mifugo na Uvuvi, kubuni njia bora zaidi ili kuwawezesha wajasiriamali na wafanyabiashara wa dagaa waweze kutumia mbinu bora za ukaushaji.  
Aidha, Dk. Shein amewasihi wajasiriamali hao kuwa makini katika matumizi ya mashine hiyo wakati wa ukaushaji ili kuepuka athari zinazoweza kujitokeza na kuharibu ubora wa bidhaa zao.
Amesema serikali inaendelea na juhudi za kuimarisha sekta ya uvuvi kwa kununua meli mbili mpya, sambamba na kuliimarisha  shirika la ZAFICO , azma inayokwenda sambamba na ujenzi wa viwanda vya Mwani, kwa mashirkiano na washirika wa maendeleo.
Dk Shein, amewapongeza wananchi hao kwa utulivu na usikivu wao wa kukubali kuhama katika eneo la Maruhubi walipokuwa wakiendesha shughuli hizo na kuhamia Kihinani.
Mapema, Waziri wa Nchi (OR) Tawala na Mikoa, Serikali za Mitaa na Vikosi vya SMZ, Haji Omar Kheir  amesema Serikali inatatua hatua kwa hatua changamoto mbali mbali zinazowakabili wajasiriamali hao.
Amesema  Serikali haina lengo la kuwaonea wananchi wake, akibainisha kuwa utekelezaji huo unakwenda sambamba na Ilani ya CCM katika kuwawezesha wananchi kiuchumi.
Ameeleza kuwa serikali imelenga kuliendeleza eneo hilo kwa kufanikisha utekelezaji wa mradi mkubwa wa ujenzi wa Bandari ya kisasa, hatua itakayochangia ustawi mkubwa uchumi wa Taifa.
Nae, Mkurugenzi wa Baraza la Manispaa Magharibi 'A' Amour Ali Mussa amesema Baraza hilo limetumia zaidi ya Shilingi Milioni 17.1 kwa ajili ya  kulipa fidia wananchi waliokuwa wakilitumia eneo hilo la Kihinani.
Ametaja changamoto ya ufinyu wa nafasi kwa ajili ya wafanyabiashara, ambapo eneo la eka 1.3 limeazimwa kutoka Chuo cha Mwalimu Nyerere na hivi sasa linahitajika kwa matumizi ya chuo hicho.
Amesema jumla ya wananchi 1,396 wananufaika kwa kuendesha shughuli za ujasiriamali katika sehemu hiyo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni