Jumatatu, 18 Februari 2019

DK.MABODI AIFARIJI FAMILIA YA MAREHEMU ALI HAJI PANDU


 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Mabodi akitoa ubani kwa familia ya marehemu Ali Haji Pandu, kwa niaba ya Ofisi ya Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein ambayo ni Afisi Kuu ya CCM Zanzibar.

 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Mabodi akiwafariji jamaa,ndugu na marafiki wa Familia ya marehemu Ali Haji Pandu aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Jimbo la Bumbwini aliyefariki juzi ghafla huko nyumbani kwake Bumbwini Makoba.

 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Mabodi akisalimiana na Wazee wa Bumbwini Makoba wakati akielekea msibani kuifariji familia ya Mwenyekiti wa CCM Jimbo la Bumbwini marehemu Ali Haji Pandu.


NA IS-HAKA OMAR,ZANZIBAR.

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar kimepokea kwa mshutuko,majonzi na simanzi kubwa taarifa za kifo cha Mwenyekiti wa CCM Jimbo la Bumbwini ndugu Ali Haji Pandu (70) aliyefariki ghafla nyumbani kwake Bumbwini Makoba Wilaya ya Kaskazini ‘B’ Unguja.




Akizungumza Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla ‘Mabodi’ wakati akiifariji familia ya marehemu huyo, amewaomba ndugu,jamaa na marafiki wa karibu wa marehemu kuwa na subira katika kipindi hichi cha msiba huo.

Dk.Mabodi amesema kuwa Chama Cha Mapinduzi kitaendelea kuthamini juhudi za uchapakazi,uzalendo,uongozi bora na weledi wa marehemu Ali Haji enzi za uhai wake alikuwa ni kiongozi na muumini wa kweli wa kuimarisha maendeleo ya taasisi hiyo.

Amesema taasisi hiyo imepoteza kiongozi shujaa aliyepigania maslahi ya CCM kwa vitendo na aliweza kusimamia mipango endelevu ya ushindi wa CCM katika jimbo alilolioongoza.

Katika maelezo yake Dk.Mabodi amesema kwa sasa jambo la pekee la kumsaidia marehemu huyo ni Vuongozi,Wanachama, Watendaji na Wananchi kwa ujumla kumuombea Dua Marehemu ili aweze kupokelewa katika makaazi mema peponi amin.

Naibu Katibu Mkuu huyo wa CCM Dk.Mabodi alifuatana na Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Kaskazini Unguja chini ya Mwenyekiti wa Mkoa huo ndugu Idd Ali Ame.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni