Jumanne, 27 Februari 2018

BI.CATHERINE AVITAKA VYOMBO VYA HABARI KUONGOZA MAPAMBANO YA VITA YA UDHALILISHAJI WA KIJINSIA

 KATIBU wa Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar  Bi. Catherine Peter Nao akizungumza na viongozi na watendaji wa Zenj Fm Radio katika ziara yake kwenye vyombo vya Habari Zanzibar.

 MENEJA wa Zenj Fm Winifrida Mayao(kushoto) Meneja Mkuu wa Zanzibar Media Corperations Ramadhan Sender(kulia) wakizungumza na wageni kutoka Afisi Kuu CCM Zanzibar wakiongozwa na Mkuu wa Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar Bi.Catherine Peter Nao.

 KATIBU wa Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar Bi.Catherine Peter Nao (kulia) akizungumza na Mkurugenzi Iland Media Group  Bw.Fauz Abdul Razaki (kushoto).
 KATIBU wa Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar Bi.Catherine Peter Nao, akiwa katika studio za Zenj Fm.

Mkurugenzi Iland Media Group  Bw.Fauz Abdul Razak (kushoto), akitoa ufafanuzi wa vifaa vya kurushia matangazo ya TV katika Chumba maalum cha kuzalisha vipindi.

 BAADHI ya wafanyakazi wa Coconut Fm Radio wakiwa katika Chumba Cha Habari mara baada ya kuupokea Ugeni kutoka CCM ulioongozwa na Katibu wa Idara ya NEC, Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar  Bi.Catherine Peter Nao aliyetembelea Radio hiyo.
 Katibu wa Idara ya NEC, Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar  Bi.Catherine Peter Nao akiwa katika Studio za Coconut Fm Radio iliyopo Migombani Mnara wa Mbao Zanzibar.


 Muhariri Mkuu Mtendaji wa Bomba Fm Radio Mwinyi Sadala (wa tatu kulia) akiwakaribisha wageni hao walioongozwa na Katibu  wa Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar  Bi. Catherine Peter Nao katika mwendelezo wa ziara.

 KATIBU msaidizi Mkuu  Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar Daud Ismail Juma akitambulisha maafisa mbali mbali wa CCM waliofustana na Mkuu wa Idara hiyo.

 Katibu  wa Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar  Bi. Catherine Peter Nao akiwa katika studio za Bomba Fm Radio.
 Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar  Bi. Catherine Peter Nao (kushoto) akizungumza na Bw. Aziz(kulia)  Mkuu wa udhibiti wa fedha wa Bomba FM Radio. 
Katibu  wa Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar  Bi. Catherine Peter Nao katika mwendelezo wa ziara, akiwa katika Chumba Cha kuzalisha Vipindi vya Iland TV.



 MKUU wa Vipindi  Tifu TV Bw. Mwanjie Saleh Mgeni (kulia wa mwanzo) akitoa ufafanuzi juu wa chumba cha matangazo cha Tifu TV, Katibu wa Idara ya Itikadi na Uenezi akifuatilia kwa makini maelezo hayo.
 Chumba cha kurushia matangazo cha Tifu TV.
 Meneja Mkuu wa Tifu TV  Bw.Abdalla Kesi Shaaban(kulia) akizungumza na Katibu  wa Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar  Bi. Catherine Peter Nao akizungumza na viongozi na watendaji wa Zenj Fm Radio katika ziara yake kwenye vyombo vya Habari Zanzibar.



NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR.


KATIBU wa Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar Catherine Peter Nao amesema Vyombo vya Habari ni taasisi muhimu zinazotakiwa kuwa mstari wa mbele kukemea na kuibua vitendo vya udhalilishaji wa wanawake na watoto ili wahalifu wa matukio hayo waweze kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

Kauli hiyo ameitoa katika mwendelezo wa ziara yake kwenye Vyombo vya Habari nchini, amesema taasisi hizo zenye dhamana ya kuelimisha,kuburudisha,kukosoa na kushauri zina jukumu kubwa la kueleza kwa upana athari mbaya zinazotokana na vitendo hivyo.

Alisema Chama Cha Mapinduzi kitaendelea kuishauri serikali na wadau mbali mbali wa haki za binadamu kutekeleza wajibu wao wa kuvisimamia vyombo vya kisheria kuharakisha uendeshaji wa kesi hizo na kutoa hukumu kali kwa watu wanaotiwa hatia kwa makosa hayo.

Pia, alilitaka Jeshi la Polisi nchini kuondokana na mfumo duni wa upelelezi juu ya kesi za udhalilishaji badala yake waongeze kasi na kutumia weledi na uaminifu kama kanuni na miongozo ya jeshi hilo inavyowaelekeza.

Katibu huyo alisema tayari serikali imeanza kuchukua hatua ikiwemo Baraza la wawakilishi kupitisha mswaada wa sheria mpya ya mwaka 2018, inafuta sheria ya adhabu kwa makosa ya jinai ya mwaka 2004, hivyo baada ya Rais wa Zanzibar kuitia saini na kuwa sheria kamili kinachobaki ni wananchi na wadau wengine kuunga mkono juhudi hizo.

“ CCM ni taasisi inayojali misingi ya haki za binadamu na utu kwa watu wote bila kujali tofauti za kisiasa, hivyo hawezi kubaki kimya huku nchi yetu inaendelea kuangamia kwa vitendo viovu vya ubakaji kila sehemu, ni muhimu kila mtu kupambana kwa nafasi yake ili tuondoshe janga hili.

Lakini pia taasisi zinazosimamia masuala ya utekelezaji wa Kisheria sasa tunawambia huu ndio muda wa kujitathimini na kufanya kazi vinginevyo Chama Cha Mapinduzi kitachukua hatua kali za kimaadili kwa baadhi ya viongozi wakuu wa Taasisi hizo ambao hawatekelezi wajibu wao kiutendaji”, alisema Bi,Catherine.

Hata hivyo alieleza kuwa Zanzibar haikuwa na utamaduni wa kesi za aina hiyo lakini vitendo hivyo vimeongezeka kutokana na utandawazi unaopelekea baadhi ya wananchi kuacha utamaduni wa asili na kuiga masuala ya kigeni.

Akizungumzia mchango wa vyombo vya Habari katika ukuaji wa Demokrasia, Catherine amesema taasisi hizo za kihabari zimekuwa mstari wa mbele kuandika na kuripoti vipindi, makala na habari mbali mbali za kisiasa zinazochangia ukuaji wa kidemokrasia kwa wananchi.

Alisema Vyombo vya habari  sio tu kutangaza  habari za kisiasa bali hata katika ukuaji wa kiuchumi wa Zanzibar taasisi hizo zimechangia kutangaza  fursa za nchi  katika anga za kimataifa hasa utaliii na zao la karafuu na kusaidia ukuaji wa pato la taifa unaotokana na upatikanaji wa fedha za kigeni.

Pamoja na hayo alisema lengo la ziara hiyo ni kujitambulisha,kubadilishana mawazo, kujenga mahusiano  kwa vyombo hivyo ambavyo ni wadau wakubwa wa CCM katika masuala ya kueneza Itikadi na Habari za Chama kwa wananchi.

Ameahidi kuendelea kufanya kazi na ukaribu na vyombo vya Habari mbali mbali na kuvishauri vielekeze nguvu zake sehemu za kijamii hasa za vijijini kuibua kero zinazowakabili wananchi ili taasisi husika zitafute ufumbuzi wa kudumu.

Naye  Meneja wa Radio ya Zenj Fm, Winifrida Mayao amekipongeza Chama Cha Mapinduzi kwa busara zake za kuendeleza mahusiano ya kiutendaji na Kituo hicho.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Iland Media Group, Hatwab Mbarouk Khamis ameeleza kuwa ziara hiyo imefungua milango ya kiutendaji baina ya Kituo Chake na CCM.

Akizungumza Muhariri Mkuu Mtendaji wa Bomba Fm Radio, Mwinyi Sadala amesema Kituo hicho kimekuwa ni mdau mkubwa wa kuripoti na kuandika habari za kisiasa, kijamii na kiuchumi zinazohamasisha dhana ya Utawala bora, Demokrasia, uhuru wa kutoa na kupokea maoni kwa wananchi.

Hata hivyo Sadala alikishauri Chama hicho kuwakumbusha baadhi ya Wabunge, wawakilishi,Madiwani na viongozi wengine wa Serikali ambao bado hawajatekeleza  ahadi walizotoa katika Uchaguzi Mkuu uliopita, kutumia wakati huu kutekeleza ahadi hizo kwa lengo la kurejesha matumaini ya jamii.

Ziara hiyo imeendelea katika Vyombo vya Habari mbali mbali ikiwemo Zenj Fm, Coconut Fm, Iland TV, Bomba Fm na Tifu TV.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni