Jumatano, 29 Novemba 2017

DK.MABODI AWATAKA UVCCM KUCHAGUA VIONGOZI WANAOUZIKA KISIASA

Na Is-haka Omar, Zanzibar.
       
NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Zanzibar Dk. Abdulla Juma Mabodi, amewataka Umoja wa Vijana UVCCM Mkoa wa Kaskazini Unguja, kuwachagua viongozi wa jumuia hiyo ambao ni waadilifu, wabunifu na wachapakazi watakaolinda na kutetea maslahi mapana ya UVCCM. 

Wito  huo  ameitoa leo wakati akifungua Mkutano Mkuu wa uchaguzi wa UVCCM, Mkoa wa Kaskazini Unguja, ambapo alisema viongozi watakaochaguliwa kupitia uchaguzi huo. 

Dk. Mabodi amesema  Vijana wanapaswa kuwa wabunifu kwa kuandaa mazingira rafiki ya kuwavutia vijana kujiunga na CCM kutoka vyama vya upinzani.

Amesema viongozi watakaopatikana kupitia uchaguzi huo ndio watakaounda jeshi la ukombozi wa kisiasa litakalosaidia kupata ushindi katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.

 Naibu huyo aliongeza kuwa wajumbe ambao watachagua viongozi hao wanapaswa kuhakikisha watekeleza sera na Ilani ya CCM.

 Katika maelezo yake Dk. Mabodi alisema UVCMM inapaswa kuzingatia ibara ya tano ya Chama ambapo inaelekeza kuhakikisha CCM inaendelea kushika dola hivyo ni wajibu wao kama vijana kutekeleza.

 "Chama kinatoa kipaumbe cha kupatia nafasi mbalimbali za uongozi kwa vijana ili waweze kusimamia kwa uadilifu sera na miongozo ya chama na serikali kwa maslahi ya wananchi wote,"alisema.

 Amesema  jukumu kubwa ni kuhakikisha vijana wanashawishi wenzao ili kujiunga ndani ya chama hivyo lazima viongozi watakaopatikana wawe wabunifu na wachapakazi wa kuifikisha CCM ushindi wa mwaka 2020.

 "Ikimbukwe kuwa viongozi ambao watakaoshinda ndio wameaminiwa na chama hivyo wajibu wao ni kutengeneza siasa ya mkoa kwa ajili ya ushindi wa mwaka 2020,"amesema. 

 Mbali na hilo,  amesema  ikumbukwe kuwa wakati huu ni wamapambano makali hivyo ni lazima vijana watambue kuwa ni CCM ya mabadiliko na kwamba hakuna kulala hadi kuhakikisha ushindi wa uchaguzi mkuu ujao. 

 Dk.Mabodi amesisitiza jumuia hiyo kuendeleza na kusimamia kwa uadilifu mambo mema yaliyonayo na kufafanua kuwa moja ya malengo makuu ya chama cha siasa chochote ni kushinda uchaguzi mkuu kwa kuendelea kushika dola. 

 "Na hiyo ndio sababu ya msingi ya CCM kuandaa jeshi lake la kisiasa kupitia uchaguzi wa chama ndani ya jumuia hii UVCCM na hivyo ni lazima vijana wawe daraja la kuwaunganisha vijana wenzake na kuwashawishi kujiunga ndani ya CCM kutoka vyama vya upinzani,"amesema.

Kwa upande wake Mwenyekiti ambaye amemaliza muda wake, Bakari Musa Vuai, amewasisitiza wajumbe wa mkutano huo kuchagua viongozi watakaoisaidia ushindi wa uchaguzi ujao. 

Amesema  viongozi watakaopatikana ndani ya jumuia hiyo ya UVCCM wanapaswa kuwa wenye sifa kama kanuni na katiba inavyotaka na kwamba jambo ni kujenga jumuia mpya.

Akizungumza Mjumbe wa Kamati Maalum ya CCM Taifa, Khadija Hassan Aboud alisema  vijana kutumia vizuri fursa za uongozi wanazopewa ndani ya CCM na jumuiya zake ili kujenga heshima ya kundi hilo katika jamii.

Pamoja na hayo amesema  CCM ndio chama pekee kinachopigania haki za wananchi wa makundi yote bila ya ubaguzi hivyo na kwa viongozi watakaochaguliwa wanatakiwa kuendeleza utamaduni huo ili kuimarisha jumuiya hiyo. 

Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa UVCCM Mkoa wa Kaskazini Unguja wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi katika ufunguzi wa mkutano huo.

MJUMBE wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, Mhe Khadija Hassan Aboud akizungumza katika Mkutano Mkuu Maalum wa UVCCM Mkoa wa Magharibi uliofanyika katika ukumbi wa Peace Building huko Welezo Unguja.

MJUMBE wa Mkutano Mkuu wa Uchaguzi UVCCM Mkoa wa Mjini akipiga kura katika uchaguzi huo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni