Jumapili, 26 Novemba 2017

AFISI KUU CCM ZANZIBAR WATWAA UBINGWA MASHINDANO YA MAJIMBO

Na Is-haka Omar, Zanzibar.
               
WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Kassim Majaliwa ameeleza kuwa mchezo wa soka ni miongoni mwa masoko huria linatoa nafasi kwa vijana nchini kujiajiri wenyewe.

Akihutubia mamia ya wapenzi wa soka katika fainali za mashindano ya majimbo ya Unguja kwa mchezo huo iliyofanyika katijka uwanja wa michezo wa Amaan Zanzibar.

Amesema mchezo huo umekuwa maarufu ulimwenguni na unatoa fursa mbali mbali kwa vijana ambao wana vipaji vya mchezo huo.

Aidha Mhe. Majaliwa amepongeza waandaaji wa mashindano hayo kwa kubuni mashindano la kuwakutanisha vijana katika jukwaa moja kupitia sekta ya michezo bila kujali tofauti zao kisiasa kiuchumi na kijamii.

Waziri Mkuu Majaliwa ambae pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, amesema CCM imekuwa ni mlezi bora wa kulea makundi mbali mbali ya kijamii hususani vijana ambao kitakwimu ni wengi kuliko makundi mengine na kuwataka wawe na maadili mema yatakayosaidia kukuza sekta za utamaduni na uchumi.

Ametoa wito kwa majimbo mbali mbali ya CCM kwa upande wa Tanzania bara  kuiga mfano wa majimbo ya Zanzibar  kwa kuandaa mashindano ya michezo mbali mbali kwa vijana ili kuibua vipaji vitakavyoendelea kuijenga heshima ya  nchi kimichezo katika anga za kimataifa.

“Kupitia mchezo huu nimeona vijana wengi wenye vipaji wanaoweza kucheza katika timu kubwa zilizopo nchini, hivyo endeleeni kujitokeza na kushikamana na michezo ili kujiepusha na vikundi viovu kwani mtapoteza muelekeo wa maisha yenu’’, alisema Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa.

Mapema  Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Dk. Abdulla Juma Mabodi alisema  mchezo huo umeongeza mahusiano mema kwa  majimbo yote yaliyoshiriki  katika mashindano hayo.

Dk. Mabodi alisema CCM kitaendele kuwa karibu na waandaji wa mashindano hayo  katika ligi zijazo kwa lengo la kudumisha amani, utulivu na mahusiano mazuri kwa vijana nchini.

Mashindano hayo yalianza kutimua vumbi toka mwezi Mach 24 mwaka huu yalizinduliwa na Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein yakiwa na timu 18 za Majimbo ya Unguja.

Katika fainali hiyo timu ya Afisi Kuu CCM Zanzibar imefanikiwa kutwaa ubingwa wa mashindano hayo baada ya kuifunga timu ya Jimbo la Kwahani magoli 3 – 1 yaliyofungwa na Kheir Makame mnamo dakika za 25, 32 na Haidham Khamis ksatika dakika ya 65 wakati goli la Kwahani lilifngwa na Yusuf  Juma katika dakika ya 15.

 Kufuatia ushindi wa timu ya Afisi Kuu CCM Zanzibar, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk. Mabodi amewapongeza wachezaji wa timu ya Afisi Kuu kwa kutwaa ubingwa huo na kuipa zawadi ya shilingi Milioni tano.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (kushoto) akikabidhi Gari ndogo aina ya Carry kwa nahodha wa timu ya Afisi Kuu CCM Zanzibar, Vuai Makame Jecha.

 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (kushoto) akimkabidhi ufunguo Gari ndogo aina ya Carry nahodha wa timu ya Afisi kuu CCM Zanzibar Vuai Makame Jecha mara baada ya kutwaa ubingwa wa mashindano ya Majimbo Zanzibar baada ya kuibuka na ushindi wa magoli 3 – 1 dhidi ya timu ya Kwahani.

Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe. Zubeir Ali Maulid akikabidhi zawadi ya mchezaji bora wa mashindano ya majimbo nahodha wa timu ya Afisi Kuu CCM Zanzibar Vuai Makame Jecha.

Viongozi mbali mbali wa Serikali na CCM wakiwa jukwaa kuu la Uwanja wa Amaan Stadium wakifuatilia mchezo huo.

Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk. Abdulla Juma Mabodi akiwa na kombe la ubingwa wa mashindano ya majimbo ya Zanzibar pamoja na wachezaji wa timu ya Afisi Kuu CCM Zanzibar mara baada ya kutwaa ushindi wa mashindano hayo.

Baadhi ya wananchi waliojitokeza katika uwanja wa Amaan kuangalia mechi hiyo wakifuatilia kwa makini timu zao.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni