Ijumaa, 19 Juni 2020

MAKADA WA CCM WANNE LEO WACHUKUA FOMU ZA URAS WA ZNZ

 KATIBU wa Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Organazeni CCM Zanzibar Cassian Galos Nyimbo (kushoto), akimkabidhi fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea Urais wa Zanzibar kupitia CCM, Waziri wa Maji Prof.Makame Mnyaa Mbarawa(kulia), hafla iliyofanyika leo Juni 19,2020 Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Zanzibar.

 KADA wa Chama Cha Mapinduzi Mwatum Mussa Sultan, akionyesha mkoba wenye fomu za kuomba ridhaa ya kugombea Urais wa Zanzibar, mara baada ya kukabidhiwa na KATIBU wa Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Organazeni CCM Zanzibar Cassian Galos Nyimbo, hafla iliyofanyika leo Juni 19,mwaka 2020 Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Zanzibar.

 KADA wa Chama Cha Mapinduzi Mwl.Haji Rashid Pandu(kulia), akionyesha mkoba wenye fomu za kuomba ridhaa ya kugombea Urais wa Zanzibar kupitia CCM, mara baada ya kukabidhiwa na Katibu wa Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Organazeni CCM Zanzibar Cassian Galos Nyimbo, hafla iliyofanyika leo Juni 19,mwaka 2020 Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Zanzibar.

 KATIBU wa Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Organazesheni CCM Zanzibar Cassian Galos Nyimbo(kushoto), akimkabidhi fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea Urais wa Zanzibar kupitia CCM, Kada wa Chama Cha Mapinduzi Dk.Abdul-halim Mohamed Ali(kulia), hafla hiyo imefanyika leo Juni 19, mwaka 2020 Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Zanzibar.


  
MAKADA wengine wanne leo wameendelea wamejitokeza kuchukua fomu za kuomba ridhaa ya kugombea Urais wa Zanzibar,ambao ni Waziri wa Maji Profesa Makame Mnyaa Mbarawa,Kada wa CCM Mwatum Mussa Sultan,Kada wa CCM Mwl.Haji Rashid Pandu na Kada wa CCM Dk.Abdul-halim Mohamed Ali ambao wamefikisha idadi ya makada 13 waliochukua fumu hizo toka zoezi hilo lianze Juni 15,mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa Habari mara baada ya kuchukua fomu hiyo, majira ya saa 4:00 asubuhi

Waziri wa Maji Prof.Makame Mnyaa Mbarawa,hafla hiyo imefanyika Afisi Kuu ya CCM Zanzibar.
Amesema anamshukru Mwenyezi Mungu kwa kumjaalia uwezo na nguvu za kushiriki katika mchakato huo ambao ni muhimu katika hisoria mpya ya maisha yake.

Amesisitiza kwamba jambo muhimu kwa sasa ni kumuomba Mwenyezi Mungu aendelee kufungua milango ya neema katika zoezi hilo liendelee kufanyika kwa ufasini na afikie malengo yake ya kuwa Rais wa Zanzibar.

Aidha amesema atazungumza kwa upana mambo mbali mbali juu ya mbio zake za kuwania Urais wa Zanzibar pindi atakapokamilisha zoezi la kujaza fomu hizo.

Naye Mwatum akizungumza na Waandishi wa habari mara baada ya kuchukua fomu hiyo, alikipongeza Chama Cha Mapinduzi kwa ukomavu wake wa demokrasia ya kuwaruhusu makada wake wa jinsia zote kugombea nafasi mbali mbali za Uongozi kupitia Chama hicho.

Amewataka Wanawake nchini kuendelea kujitokeza kugombea nafasi mbali mbali za uongozi ili kufikia asilimia 50 kwa 50 katika vyombo vya kufanya maamuzi.

Amesema amechukua fomu hiyo ili kuwahamasisha wanawake wengine wajitokeze katika kuwania nafasi mbali mbali za uongozi kama walivyo wanaume.

"Nachukua nafasi hii kumuomba Mwenyezi Mungu anisimamie katika safari yangu hii ya kuomba ridhaa ya kuwa Rais wa Zanzibar", amesema Mwatum.

Pamoja na hayo amesema hatoweza kutoa maelezo mengi kwa waandishi wa habari mpaka atakapokamilisha   zoezi la kujaza fomu hiyo.

Kwa upande wake kada wa CCM Mwl.Haji Rashid Pandu,akizungumza mara baada ya kuchukua fomu hiyo amesema lengo lake ni kutetea maslahi ya wakulima ambao mchango wao ni mkubwa katika maendeleo ya nchi.

Kada huyo ambaye kitaaluma ni mwalimu,amesema lengo lake ni kusimamia kwa vitendo falsafa ya mapinduzi ya kilimo nchini.

Akizungumza kada wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Dk.Abdul-halim Mohamed Ali aliyechukukua fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea Urais wa Zanzibar kupitia CCM,amesema lengo ni kuhakikisha Zanzibar inakuwa na maendeleo endelevu.

Dkt.Abdulhalim, amesema endapo Chama Cha Mapinduzi kitampa ridhaa ya kupeperusha bendera ya CCM kuwania kiti cha Urais, atakuwa mstari wa mbele kutatua changamoto za wananchi bila ubaguzi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni