Alhamisi, 7 Machi 2019

UWT KUING'OA CUF PEMBA,UWT YAVUNA WANACHAMA 507.





MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake wa CCM Tanzania(UWT) Ndugu Gaudensia Kabaka akisalimiana na wanachama wa CCM katika shule ya sekondari Wara.


MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake wa CCM Tanzania(UWT) Ndugu Gaudensia Kabaka akikagua shule ya Sekondari Wara ambayo ni Utekeleaji wa Ilani ya CCM ya Mwaka 2015/2020.
 MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake wa CCM Tanzania(UWT) Ndugu Gaudensia Kabaka akizungumza na wanachama wa CCM mara baada ya kukagua ujenzi wa shule ya kisasa ya Wara katika Wilaya ya Chake Chake Pemba.



MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake wa CCM Tanzania(UWT) Ndugu Gaudensia Kabaka akichota udongo wa kujengea Tawi la CCM Kangani Wilaya ya Mkoani.



MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake wa CCM Tanzania(UWT) Ndugu Gaudensia Kabaka akijenga Tawi la CCM la Kangani Wilaya ya Mkoani Pemba.


MAKAMU Mwenyekiti wa UWT Taifa Ndugu Thuwaiba Kisasi akijenga Tawi la CCM Kangani.


 KATIBU wa UWT Taifa Mwl.Queen Mlozi akijenga Tawi la CCM Kangani.


 NAIBU Katibu Mkuu wa UWT Tanzania Bara ndugu Jesca Mbogo akijenga Tawi la CCM Kangani.


NAIBU Katibu Mkuu wa UWT Zanzibar Ndugu Tunu akijenga Tawi la CCM Kangani.


MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake wa CCM Tanzania(UWT) Ndugu Gaudensia Kabaka akikabidhi fedha za michango mbali mbali zilizotolewa na Wabunge na Wawakilishi wa Viti Maalum kwa ajili ya ujenzi wa Tawi la CCM Kangani Pemba.





MBUNGE wa Viti Maalum Mhe. Munira Mohamed akikabidhi Fedha kwa ajili ya ujenzi wa Tawi la Kangani Wilaya ya Mkoani Pemba.





 MBUNGE wa Viti Maalum Mhe.Faida Mohamed Bakari akichangia fedha kwa ajili ya ujenzi wa Tawi la CCM Kangani Pemba.


NA IS-HAKA OMAR,PEMBA.



WANAWAKE wa Chama Cha Mapinduzi kisiwani Pemba wametakiwa kufanya Mapinduzi ya kisiasa kwa kuhakikisha CCM inavunja na kusambaratisha ngome ya CUF na hatimaye kushinda majimbo yote ya Uchaguzi ya mwaka 2020.

Wito huo umetolewa na Mwenyekiti wa UWT Taifa Ndugu Gaudensia Kabaka katika mwendelezo wa ziara yake huko Shule ya Sekondari ya Mohamed Juma Pindua Wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba, alisema ni wakati wa wanawake kuonyesha uwezo wao na kutekeleza kwa vitendo falsafa ya 'Wanawake ni jeshi la ukombozi la CCM'.

Amesema hakuna chama cha siasa, wala taasisi yoyote itakayoweza kuzuia ushindi wa CCM mwaka 2020 kisiwani Pemba endapo wanawake wataamua kuungana kwa pamoja ili kufanikisha ushindi wa CCM.

Katika maelezo yake Ndugu Gaudensia amesema Jeshi la UWT la Chama Cha Mapinduzi litakuwa mstari wa mbele kupambana vita ya kisiasa kwa mbinu zote ili kuandika historia mpya katika uwanja wa siasa za ushindani Tanzania kwa kuhakikisha CCM inashinda kwa kiwango kikubwa Zanzibar na Tanzania bara.

“Wanawake tuna nguvu, uwezo, ujasiri, mikakati,nyenzo na mbinu za medali za kisiasa hivyo hatuna sababu ya kuyaachia majimbo ya Pemba yaendelee kubaki kwa wapinzani bali yatarudi mikononi mwa CCM.”,amesema Bi.Gaudensia.

Mwenyekiti huyo wa UWT Taifa Ndugu Gaudensia, amepongeza hatua za kimaendeleo zilizofikiwa katika Sekta ya Elimu Pemba hasa katika suala zima la miundombinu ya Majengo ya Kisasa ya kiwango cha Ghorofa.

Aidha ameyataja mageuzi makubwa katika miundombinu ya Barabara za kisasa mijini na Vijiji kuwa ni ya kiwango bora cha kuridhisha hatua ambayo wananchi wa kisiwa cha Pemba wanastahiki kuithamini Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa mambo mema yaliyotekelezwa.

Pamoja na hayo amewasisitiza hakina Mama Visiwani Pemba bila kujali tofauti zao za kisiasa kushiriki katika kongamano la Kitaifa litakalofanyika Machi 9 mwaka 2019, katika Kiwanja cha Tibirinzi Wilaya ya Chake Chake Pemba.

Ameeleza kuwa Kongamano hilo lililoandaliwa na UWT ni la kupongeza utekelezaji mzuri wa Ilani ya CCM ya mwaka 2015/2020 pamoja na masuala mbali mbali ya kimaendeleo yaliyoasisiwa na Serikali za CCM kwa awamu tofauti za Uongozi.

Pamoja na hayo amewapongeza Wabunge na Wawakilishi wa Viti Maalum Pemba kwa kazi nzuri wanazozifanya katika kuwaletea wananchi maendeleo endelevu.

Naye Katibu Mkuu wa UWT Taifa Mwl.Queen Mlozi amekemea vitendo vya udhalilishaji wa Kijinsia kwa Watoto wa Kike vinavyochangia kukwamisha maendeleo ya wanawake katika kunufaika na fursa za elimu.

Mwl.Queen amewasihi  Wazazi,Walezi pamoja viongozi wa dini na kisiasa kusimamia ajenda za kulinda na kutetea haki za wanawake hasa vijana na watoto ili wanufaike na fursa mbali mbali ndani ya jamii.

Akizungumzia changamoto za dawa za kulevya kwa vijana, Naibu Katibu Mkuu wa UWT Tanzania bara Ndugu Jesca Mbogo amesema baadhi ya vijana kisiwani Pemba wameingia katika changamoto za kutumia dawa za kulevya hali ambayo ni hatari katika ustawi wa maendeleo ya nchi.

Mapema Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Kusini Pemba, ndugu Bimkubwa Khamis Mohamed ameelea kuwa hali ya kisiasa ndani ya mkoa huo imeendelea kuimarika na wanawake wamekuwa wakijitokeza kwa wingi kujiunga na CCM.

Amesema Pemba ya Sasa sio Pemba ya zamani kwani wananchi wengi wameanza kutambua ukweli baada ya kuona kwa vitendo mambo mema yanayotekelezwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inayotokana na Chama Cha Mapinduzi.
Kupitia ziara hiyo jumla ya Wanachama Wapya 507 wamejiunga na UWT na kukabidhiwa kadi za uanachama watu 10 kwa niaba ya Wenzao.


 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni