Jumapili, 21 Oktoba 2018

MWL.RAYMOND AITIKISA JANG'OMBE , AWASIHI VIJANA KUMPIGIA KURA ZA NDIO RAMADHAN CHANDE.


 KATIBU Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi  Mwl. Raymond Mwangwala akiwahutubia wananchi na kumwombea kura za ndio Mgombea wa CCM Ramadhan Chande  kupitia Mkutano wa kampeni za uchaguzi mdogo wa Jimbo la Jang'ombe Zanzibar, uliofanyika katika Uwanja wa Tawi la CCM Kidogo chekundu.


NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR.

KATIBU Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi  Mwl. Raymond Mwangwala amewasihi wananchi wa jimbo la Jang’ombe hasa vijana kumchagua kwa kura za ndio mgombea wa tiketi ya CCM Ramadhan Hamza Chande.

Wito huo ameutoa leo alipokuwa akimnadi  na mgombea wa CCM Jimbo la Jang’ombe huko katika Mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika katika Tawi la Kidongo Chekundu Unguja.

Amemtaja mgombea huyo wa CCM kuwa ni mgombea pekee mwenye sifa na vigezo vya kuleta mabadiliko chanya ya maendeleo katika Jimbo hilo.
Mwl. Raymond amesema viongozi mbali mbali wa CCM katika Jimbo la Jang’ombe wametekelea kwa ufanisi miradi ya maendeleo na kupunguza kwa kiasi kikubwa changamoto sugu za jimbo.

Pia ameongeza kuwa  Serikali ya awamu ya saba inayoongozwa na  Rais wa Zanzibar  na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein ametekeleza kwa ufanisi Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015/2016  hatua ambazo zinastahiki kuungwa mkono na wananchi wote hasa wa Jimbo hilo.

Katibu Mkuu huyo wa UVCCM Raymond, amebainisha kwamba mafanikio hayo yatakuwa endelevu endapo wanachama na wananchi wa Jang’ombe watamchagua mgombea anayetokana na Chama Cha Mapinduzi chenye sera imara na historia ya kuwatumikia wananchi wa rika zote hasa vijana.

Katika maelezo yake Katibu Mkuu huyo alisema kupitia Bajeti ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 2018/2019  zimetengwa jumla ya shilingi bilioni tatu kwa ajili ya kusaidia kundi la Vijana hatua ambayo inatakiwa kuthaminiwa na kundi hilo.

Amesema mbali na fedha hizo pia Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inayotokana na CCM inajenga viwanja vya kisasa vya michezo kwa kila Wilaya Zanzibar kwa lengo la kuwawezesha vijana wajiajiri kupitia sekta ya michezo mbali mbali.

Aidha amesisitiza kuwa CCM ina matarajio makubwa ya kushinda kwa asilimia kubwa katika uchaguzi huo kutokana na Wananchi hasa kuiamini na kuiunga mkono tasisi hiyo kwani ushahidi wa tathimini hizo umeonekana wazi katika Chaguzi  za Majimbo mbali mbali ya Tanzania bara ambayo chama hicho kimeshinda kwa kishindo.

“Mgombea wetu anauzika ana mvuto na pia ana sifa ya utendaji na uchapakazi uliotuka hivyo nakuombeni wananchi wa Jimbo la Jang’ombe hasa Vijana Wenzangu Octoba 27, mwaka huu tumchague ndugu Ramadhan Hamza kwa kura nyingi  za ndio”, alisema Mwl. Raymond.

Ameongeza kuwa Vyama vya upiunzani kwa sasa havina sera na vimepoteza dira ya kisiasa kwa kutawaliwa na migogoro na visasi vya wenyewe kwa wenyewe hali inayovikosesha sifa ya kuongoza nafasi yoyote katika jamii.

Akizungumza Mgombea wa Uwakilishi tiketi ya CCM  Ramadhan Hamza Chande, amewaomba  kura za ndio wanachama na wananchi wote wa Jimbo hilo.

Amesema  kupitia Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi atakuwa mstari wa mbele kushirikiana na makundi yote hasa vijana  kutekeleza mikakati ya maendeleo.

Akizungumza Mjumbe wa Kamati Maalum ya NEC Taifa Zanzibar kupitia kundi la Vijana Ndugu Abdulghafari Idissa amesema CCM ndio Chama chenye dhamira ya kweli ya kuwaletea wananchi wote maendeleo.

Naye Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi Salha Mohamed Mwinjuma amewaomba Vijana na wanawake siku ya kupiga kura wajitokeze kwa wingi kumchagua mgombea wa CCM kwani ana uwezo mkubwa wa kubuni mbinu mbadala za kuwaletea maendeleo.

Uchaguzi huo unafanyika kutokana na aliyekuwa Mwakilishi wa Jimbo la Jang’ombe Ndugu  Abdallah Diwani kuvuliwa uanachama baada ya kukiuka maadili ya Chama Cha Mapinduzi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni