Jumapili, 21 Oktoba 2018

MATUKIO KATIKA PICHA KAMPENI ZA CCM JIMBO LA JANG'OMBE MGENI RASMI KATIBU MKUU WA UVCCM MWL.RAYMOND.


 MGOMBEA wa  tiketi ya CCM  uchaguzi mdogo wa Jimbo la Jang'ombe Ramadhan Hamza Chande akiwasalimia wanachama wa CCM mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Mkutano wa kampeni uliofanyika Tawi la CCM Kidogo Chekundu.

 MGOMBEA wa CCM Ramadhan Chande pamoja na Katibu Mkuu wa UVCCM Mwl. Raymond wakicheza mziki wa kizazi kipya katika mkutano wa kampeni.

 MSOMA Utenzi katika Mkutano huo

 KATIBU Mkuu wa UVCCM Mwl. Raymond  Mwangwala akihutubia na kumnadi mgombea katika Mkutano uliofanyika Tawi la Kidongo chekundu.

 MGOMBEA wa CCM katika Uchaguzi wa Jang'ombe Ramadhan Hamza Chande akiomba kura za ndio kwa wananchi wa Jang'ombe Shehia ya Kidongo chekundu.

 MWENYEKITI wa UVCCM Mkoa wa Mjini Kamaria Suleiman Nassor akiwatambulisha viongozi mbali mbali na kumuombea kura mgombea wa CCM.

 MWENYEKITI wa UVCCM Jimbo la  Jang'ombe akifungua Mkutano huo wa Kampeni.

 ALIYEKUWA Mgombea mwenza katika mchakato wa kura za maoni CCM ndugu  Othman  Shaaban Kibwana akimuombea kura Mgombea wa Uwakilishi Jimbo la Jang'ombe.

 WAJUMBE wa Baraza la Wawakilishi nafasi za Vijana wakimuombea kura mgombea wa CCM katika mkutano huo.

 MADIWANI wa Wadi za Jang'ombe wakimuombea kura Mwakilishi wa Jang'ombe.

 WAJUMBE wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar nafasi za Vijana wakimuombea kura za ndio mgombea uwakilishi Jang'ombe.

   Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais – Mhe. Mihayo Juma Nhunga akimuombea kura mgombea uwakilishi wa CCM Jimbo la Jang'ombe.

 BAADHI ya Wana-CCM wakimpungia mkono mgombea uwakilishi jimbo la Jang'ombe (hayupo pichani).

 WABUNGE  wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia nafasi za UVCCM wakimuombea kura za ndio mgomea uwakilishi wa CCM, (PICHA NA IS-HAKA OMAR-AKZ).


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni