Jumatatu, 22 Oktoba 2018

MATUKIO KATIKA PICHA MKUTANO WA SITA WA KAMPENI ZA CCM UCHAGUZI WA JANG'OMBE MGENI RASMI MHE.SAMIA SULUHU HASSAN.

 MJUMBE wa Kamati Kuu ya CCM Taifa ambaye pia ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk. Abdulla Juma Mabodi mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Baja kwa ajili ya kumnadi mgombea wa CCM wa Jimbo la Jang'ombe Ndugu Ramadhan Hamza Chande.

 BAADHI ya Viongozi na wanachama wa CCM wakiimba wimbo maalum wa Mashujaa katika Mkutano wa Sita wa kampeni za CCM Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Jang'ombe.

 BAADHI wa wanachama wa CCM wakiimba wimbo maalum wa mashujaa katika mkutano wa kampeni za CCM Jimbo la Jang'ombe uliofanyika katika Uwanja wa Baja Ziwani Zanzibar.

 WAKUU wa Idara za  CCM Zanzibar ambao pia ni Wajumbe wa Kamati Maalum ya NEC Taifa Zanzibar wakifuatilia matukio mbali mbali katika Mkutano wa Kampeni za CCM  Jimbo la Jang'ombe uliofanyika katika Uwanja wa Baja.


VIONGOZI mbali mbali wa CCM wakiwa katika mkutano wa kampeni za Uchaguzi wa Jimbo la Jang'ombe.

 KIKUNDI cha muziki wa Taarab cha Big Star kikitoa burudani katika mkutano huo ambao mgeni rasmi alikuwa ni Mhe. Samia Suluhu Hassan.

 WANA-CCM wakimpungia mikono Mgombea wa CCM Ramadhan Hamza Chande kuashiria kuwa watampigia kura za ndio katika Uchaguzi mdogo unaotarajiwa kufanyika Octoba 27, mwaka 2018.

 VIONGOZI wa CCM wakimtuza fedha msoma utenzi  Ndugu Kassim katika mkutano huo wa Kampemi uliofanyika katika Uwanja wa Baja.

 MJUMBE wa Kamati Kuu ya CCM Taifa ambaye pia ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwahutubia wananchi na Wana-CCM katika mkutano wa kampeni za CCM Jimbo la Jang'ombe.

 MJUMBE wa Kamati Kuu ya CCM Taifa ambaye pia ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe. Samia Suluhu Hassan(kulia) akimkabidi  Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015/2020 pamoja na Katiba ya CCM ya mwaka 1977 toleo la 2017 Mgombea wa Uwakilishi Jimbo la Jang'ombe Ndugu Ramadhan Hamza Chande (kushoto)  ambazo ni nyenzo za kufanyia kazi katika Jimbo la Jang'ombe. 

 Mgombea wa Uwakilishi Jimbo la Jang'ombe Ndugu Ramadhan Hamza Chande kionyesha Ilani ya Uchaguzi ya CCM pamoja na Katiba mara baada ya kukabidhiwa na mgeni rasmi.

Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk. Abdulla Juma Mabodi akizungumza na kumuombea kura mgombea wa CCM Ramadhan Hamza Chande.

 MWENYEKITI wa Mkoa wa Mjini Talib Ali Talib akimuombea kura za ndio mgombea wa CCM.

 KATIBU wa CCM Mkoa wa Mjini Ndugu  Mohamed Nyawenga akizungumza na kuwatambulisha wageni mbali mbali katika mkutano huo wa Kampeni.

 MJUMBE wa Kamati Maalum ya NEC Taifa Zanzibar  Mhandisi  Nassir Ally Juma akimuombea kura Mgombea wa CCM Jimbo la Jang'ombe.

 MJUMBE wa Baraza la Wawakilishi  ambaye pia ni Naibu Waziri  wa Nchi  Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar  Mihayo Juma Nhunga akimuombea kura mgombea wa CCM  Jimbo la Jang'ombe Ramadhan Chande.

 MGOMBEA mwenza wa Ramadhan Chande katika mchakato wa kura za maoni ndani ya CCM Lilian Limo akimuombea kura za ndio mgombea Uwakilishi Jimbo la Jang'ombe Zanzibar.

 MBUNGE Mteule wa Jimbo la Liwale Mkoani Lindi Ndugu Zubeir Mohamed aliyehama katika Chama cha CUF hivi karibuni na kujiunga na CCM akimuombea kura za ndio mgombea uwakilishi wa Jimbo la Jang'ombe.

 MBUNGE wa Jimbo la Jang'ombe Ali  Hassan Omar 'King' akimuombea kura za ndio mgombea  uwakilishi wa Jimbo hilo Ramadhan Hamza Chande, (Picha na Is-haka Omar-AKZ).

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni