Jumamosi, 24 Juni 2017

Wanawake nchini watakiwa kuwa msatri wa mbele




Wanawake Nchini wametakiwa kuwa mstari wa mbele kuisaidia Serikali katika kupiga vita vitendo vya udhalilishaji na watotozinavyoonekana kushamiri Nchini.

Hayo ameyasema Naibu Katibu Mkuu wa UWT Mhe. Salama Abuod Talib katika kikao cha viongozi, watendaji na watumishi wote wa UWT Mkoa na Wilaya kikao kilichofanyika katika Afisi Kuu ya CCM Kiswandui.

 Amesema wanawake wamekuwa mstrai wa mbele kukipa msukumo Chama bila kuchoka na ndio chache ya ushindi ya Chama Cha Mapinduzi. Amewataka wanawake wote kuhamasisha wanawake wenzao kujiunga na UWT kwani ndio chachu na mkombozi Nchini. 

 Salama amempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein kwa kuwaamini wanawake na kuwapa nafasi za uongozi ndani ya Chama na Serikali yake.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni