Jumamosi, 24 Juni 2017

DKT. MABODI AWATAKA WASOMI KUBUNI MIKAKATI ITAKAYOPUNGUZA TATIZO LA AJIRA NCHINI.

  
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Dkt. Abdulla  Juma Saadalla akizungumza na vikundi sita vya vijana wa CCM wa Vyuo vikuu na taasisi za  Elimu ya Juu  Zanzibar,  hapo  Afisi Kuu CCM Kisiwandui.


 Baadhi ya vijana wa CCM wa Vyuo vikuu na taasisi za  Elimu ya Juu  Zanzibar wakifuatilia kwa umakini nasaha zinazotolewa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Dkt. Abdulla Juma Saadalla.


Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar  Dkt. Abdulla Juma Saadalla “ Mabodi”  amewataka wasomi na wataalamu wa CCM waliopo katika taasisi za elimu ya juu kutumia taaluma zao kubuni mikakati endelevu itakayosaidia kupunguza tatizo la ajira na kuimarisha uchumi wa nchi.

Rai hiyo ameitoa wakati akizungumza na vikundi  sita  vya vijana na wasomi wa vyuo vikuu na taasisi za elimu ya juu wa Chama hicho nchini huko Afisi kuu CCM Kisiwandui Zanzibar,  Dkt. Mabodi amesema maendeleo ya taifa lolote duniani yanatokana  na fikra za maendeleo  zinazobuniwa na wasomi.

Amewambia wasomi hao wa kada mbali mbali za Vyuo Vikuu kuwa ni lazima wakae pamoja na kupanga mikakati itakayoisaidia CCM na serikali zake kupiga hatua za kimaendeleo katika nyanja mbali mbali za kiuchumi, kisiasa na kijamii.

Ameeleza kuwa Chama Cha Mapinduzi kupitia sera zake kinaendelea kutoa vipaumbele katika sekta za elimu hasa vyuo vikuu kuhakikisha vinazalisha  wasomi wenye uwezo wa  kitaaluma  utakaoisaidia  nchi kujitawala yenyewe  kwa kila sekta ili kuenzi kwa vitendo fikra za  waasisi wa Mapinduzi Matukufu ya mwaka 1964.

Aidha  Dkt. Mabodi amesema  vijana hao ambao ni wataalamu watumie  nyenzo za kitaaluma zikiwemo fursa ya ujasiriamali kwa kujiajiri wenyewe badala ya kusubiri ajira kutoka katika katika chanzo kimoja cha nafasi za ajira kutoka serikalini.

  

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni