Jumatatu, 12 Juni 2017

NAIBU KATIBU MKUU WA UMOJA WA WAZAZI CCM Z'BAR BI.NAJMA GIGA ATEKELEZA AHADI ZAKE KWA WILAYA SITA.

  Katibu Msaidizi wa Idara ya Organazesheni Umoja wa Wazazi Tanzania  anayefanyia kazi zake Zanzibar, Nd. Simba Haji Mcha akisoma taarifa fupi ya kukabidhi Komputa kwa Wilaya Sita za Umoja huo.

 Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Wazazi Zanzibar ,  Nd. Mustafa Rashid Kumwala akitoa nasaha kwa  Makatibu wa Wilaya Sita za Umoja huo kabla ya kuwakabidhi komputa hizo.
 Baadhi ya Komputa zilizotolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Wazazi Zanzibar, Bi. Najma Giga kwa Wilaya Sita za Umoja huo.

 Kushoto ni Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Wazazi Zanzibar , Mustafa Rashid akimkabidhi  Kopmputa  Katibu wa Wazazi Wilaya ya Kati Unguja  Bi. Husna Rashid.

Katibu wa Wazazi Wilaya ya Wete Pemba akikabidhiwa Komputa kwa niaba ya Katibu wa  Wazazi Wilaya  ya Chake Chake  na Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Wazazi Zanzibar , Mustafa Rashid.

 Kushoto ni Katibu wa Wazazi Wilaya ya Wete Pemba akikabidhiwa Komouta na Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Wazazi Zanzibar , Mustafa Rashid.
   Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Wazazi Zanzibar , Mustafa Rashid akikabidhi  Kopmputa kwa  Katibu wa Wazazi Wilaya ya Amani, Bi. Mwanaisha Ame.
 Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Wazazi Zanzibar , Mustafa Rashid akikabidhi  Kopmputa kwa  Katibu wa Wazazi Wilaya ya  Mfenesini,  Bi.  Mosi  Omar.
   Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Wazazi Zanzibar , Mustafa Rashid akikabidhi  Kopmputa kwa  Katibu wa Wazazi Wilaya ya  Kaskazini “B” Unguja ,  Bi.  Salma Shaibu .


Baadhi ya Maafisa wa Afisi Kuu ya Wazazi Zanzibar  wakishuhudia zoezi hilo.
 Viongozi na Watendaji mbali mbali wa Wilaya, Mikoa  pamoja na Maafisa  wa Afisi Kuu ya Umoja wa Wazazi Zanzibar  wakiwa katika  picha ya pamoja mara baada ya hafla fupi ya kukabidhiwa  Komputa. (PICHA  NA AFISI KUU CCM ZANZIBAR) .

VIONGOZI  wa  Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Jumuiya  zake   wameshauriwa kutekeleza kwa wakati ahadi wanazotoa ndani ya chama na jumuiya zake ili kurahisha masuala ya kiutendaji katika taasisi hizo.

Ushauri huo umetolewa kwa nyakati tofauti na baadhi ya Makatibu wa Wilaya Sita za Umoja huo Zanzibar mara baada ya kukabidhiwa Komputa zilizotolelewa na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Wazazi CCM Zanzibar, Bi. Najma Giga ikiwa ni miongoni mwa utekelezaji wa ahadi alizowahi kutoa katika ziara zake alizofanya katika wilaya mbali mbali za Umoja huo Zanzibar.

Mmoja kati ya Makatibu hao ambaye ni  Katibu wa  Wazazi  Wilaya ya  Amani, Bi.Mwanaisha  Ame Mohamed amesema upatikanaji wa vifaa hivyo utaongeza ufanisi wa kiutendaji ndani ya umoja huo.

Aidha  Katibu huyo amewashauri  viongozi wa Chama Cha Chama na Jumuiya  zingine hasa  Wabunge, Wawakilishi na Madiwani  kufuata nyayo za kiongozi huyo   katika juhudi za kuharakisha maendeleo ya CCM kisiasa na kiuchumi.

Naye  Katibu wa Wazazi Wilaya ya  Wete Pemba, Bi. Mariam Ali Said  amemshukru Naibu Katibu Mkuu wa Wazazi Zanzibar kwa kutekeleza ahadi zake kwa vitendo na kuongeza kuwa vifaa hivyo vitamaliza changamoto za uchapaji wa nyaraka za kiofisi masafa ya mbali.

Akizungumza Kaimu  Naibu Katibu Mkuu  Wazazi Zanzibar, Nd. Mustafa Rashid Kumwalu  kwa niaba ya Naibu Katibu Mkuu wa umoja huo Bi. Najma Gina mara  baada ya kukabidhi  Komputa  hizo ametoa wito kwa watendaji wa umoja huo kutumia komputa hizo kwa matumizi yaliyokusudiwa  ili shughuli za kiutendaji ndani ya umoja huo zifanyike kwa wakati na kwa ufanisi.

Nd. Rashid  alieleza kuwa  lengo la umoja huo ni kuhakikisha watendaji wake wanapata vitendea kazi vya kisasa vitakavyosaidia  kutekeleza kwa wakati shughuli za kiutendaji  kwa lengo la kwenda sambamba na matakwa  ya Katiba ya CCM iliyofanyiwa mabadiliko miezi kadhaa iliyopita.

Aidha amefafanua kwamba Komputa zilizokabidhiwa leo ni 6 ambapo awali alikabidhi tatu hivyo zimekuwa ni tisa na bado kumi kwa mujibu wa idadi ya komputa zilizoahidiwa na Naibu katibu Mkuu wa Umoja huo.

Komputa hizo zina thamani zaidi ya shilingi milioni Saba zimekabidhiwa kwa  Wilaya  6  za  Umoja  wa  Wazazi  CCM Wilaya ya Amani, Wilaya ya Mfenesini, Wilaya ya Kati, Wilaya ya Kaskazini “B”, Wilaya ya Wete na Wilaya ya Chake Chake Pemba.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni