Jumamosi, 29 Desemba 2018

UVCCM YAANZA KUJINOA KUELEKEA KILELE CHA MIAKA 55 YA MAPINDUZI.

 NAIBU Katibu Mkuu wa UVCCM Zanzibar Ndugu Mussa Haji Mussa (wa pili kushoto) Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Kusini Unguja Ndugu Latifa Khamis Juakali(wa kwanza kushoto), Mkuu wa Wilaya ya Kusini Unguja Mhe. Idrissa Kitwana( wa pili kulia) pamoja na Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Mjini Ndugu Kamaria Suleiman Nassor wakionyesha uwezo wao katika fani ya mazoezi ya viungo vya mwili.
(PICHA NA IS-HAKA OMAR-AFISI KUU YA CCM ZANZIBAR)

UMOJA wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi(UVCCM) leo imefanya matembezi ya kuenzi miaka 55 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, yaliyoanzia Amaani na kuishia Viwanja vya Maisara Unguja.

Matembezi hayo yaliyoongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kusini Unguja Mhe. Idrissa Kitwana yameudhuriwa na Viongozi mbali mbali wa Chama na Serikali.

Maelfu ya Vijana wa UVCCM wameshiriki katika matembezi hayo huku wakionyesha uhodari na ukakamavu wao uliopambwa na nyimbo mbali mbali za kizalendo hasa zile zenye maudhui ya kuwaenzi Waasisi wa Mapinduzi Matukufu ya January 12,1964.

Kwa mujibu wa Taarifa kutoka Afisi Kuu ya UVCCM Zanzibar zimeeleza kuwa matembezi hayo ni sehemu ya mazoezi ya kuweka sawa viungo vya mwili ikiwa ni maandalizi ya Matembezi Makubwa yanayotarajiwa kufanyika hivi karibuni Kisiwani Pemba.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni