Jumanne, 3 Aprili 2018

MHE.SAMIA -AANZA ZIARA NA KUTEMBELEA MIRADI YA CCM KATIKA MKOA WA MAGHARIB Z'BAR

  MJUMBE wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Mhe. Samia Suluhu Hassan(katikati), Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Abdulla Juma Mabodi(wa kwanza kushoto) pamoja na viongozi na wananchi wengine wakisikiliza maelezo ya kitaalamu ya Katibu wa Jumuiya ya wakulima wa kizimbani. Ndugu Shafii Kibwana Said(kulia). 
 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk. Abdulla Juma Mabodi akieleza mafanikio yaliyopatikaka  kupitia  utekelezaji wa Ilani ya CCM katika Sekta ya kilimo huko katika bonde la mpunga la Kizimbani.


 BAADHI ya wananchi na Wana CCM wakishiriki katika upandaji wa mpunga katika bonde la Kizimbani katika zira ya Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Mhe. Samia Suluhu Hassan.


 MJUMBE wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi katika hafla ya maandalizi ya kilimo cha mpunga na upandaji wa Mpunga katika bonde la kizimbani Unguja, kilimo kinaendeshwa na Wana CCM wa Jimbo la Bububu na maeneo jirani.
 ENEO lililopandwa mpunga katika bongde la kizimbani  katika ziara ya Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Mhe. Samia Hassan Suluhu iliyofanyika leo katika Mkoa wa Mjini.


 MJUMBE wa Kamati ya uhifadhi mazingira ya fuoni Kibondeni Ndugu Mwaka Masoud akisoma risala baada ya kuwasili mgeni rasmi Mjumbe wa Kamati Kuu CCM Taifa Mhe. Samia Suluhu Hassan katika maeneo ya Fuoni Kibondeni.
  MJUMBE wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Mhe. Samia Suluhu Hassan akielekea katika eneo la ufugaji wa kaa huko Fuoni Kibondeni. 

  MJUMBE wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Mhe. Samia Suluhu Hassan akiweka jiwe la msingi Tawi la Fuoni kibondeni.

MJUMBE wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Samia Suluhu Hassan, ameridhishwa na kasi ya viongozi wa CCM ya kuresha utamaduni wa kurudi kwa wananchi wa chini kusikiliza kero zao na kuzitafutia ufumbuzi  wa kudumu.

Amesema kwa kiasi kikubwa wananchi walikuwa wamepoteza imani kwa CCM kutokana na kuwa viongozi wengi walikuwa wanatabia ya kukaa ofisini n kutowafikia wananchi hao na kusikiliza changamoto zao zinazowakabili.

Kauli hiyo ameitoa wakati akizungumza na wananchi wanaotumia bonde la mpunga la Kizimbani Unguja katika ziara yake ya kutembelea miradi mbali mbali inayotekelezwa na  Wana CCM katika maeneo hayo ya kilimo cha mpunga.

 Mhe. Samia ambaye pia ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  amesema  kuwa  ile dhana ya  CCM mpya na Tanzania mpya imeanza kustawi katika fikra za Wana CCM na kufanyiwa kazi kupitia utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2020/2015.

"CCM mpya imeanza kuonekana ikiwemo kuwafuatilia wananchi wa chini zaidi kwa mfano katika mikakati ya kufuatilia kaya maskini kwenye miradi ya TASAF viongozi wa chama wameanza kuonekana kufuatilia utatuzi wa changamoto za kuondoa hali ya umaskini hivyo CCM iko karibu na wananchi kwa sasa," amesema Makamu wa Rais.

Katika maelezo yake Makamu huyo wa Rais, alisema ni ukweli kuwa chama cha siasa ni watu na kwamba chama hicho chochote cha siasa kinapaswa kuwa karibu na wananchi  kwani wao ndio walioiweka Serikali madarakani.

Amewataka viongozi na watendaji wa CCM kukukumbushana kuwa pindi wanapopewa dhamana za uongozi hawatakiwi kukaa maofisini bali wana majukumu ya msingi ya kuwaletea wananchi maendeleo.

Pia, aliwapongeza wanajumuiya wa wakulima wa kilimo cha mpunga Kizimbani kwa juhudi zao za kuungana kwa jumuiya ambapo itawasaidia kuweza kusaidiwa kwa urahisi kwa pamoja kwenye sekta ya kilimo ikiwemo kupata mbolea kwa haraka.

Makamu wa Rais Samia ameahidi wanajumuiya hiyo kuwasaidia kiasi cha fedha na kuwapatia trekta kupitia CCM ili kuisaidia katika kilimo chao cha mpunga katika mabonde hayo mpunga ya Kizimbani na maeneo mengine.

Naye Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Zanzibar, Dk.Abdulla  Juma  Mabodi  amesema Chama Cha Mapinduzi kinaendelea kutatua  kero za wananchi hatua kwa hatua na kwa sasa kimesaidia kwa kiasi kikubwa wananchi wanaolima zao la mpunga katika bonde la Kizimbani.

Dk. Mabodi ameeleza kuwa lengo la kuwasaidia wakulima hao ni kukabiliana na changamoto za upungufu wa chakula hasa mchele ambao wakulima wengi wamewekeza  nguvu zao katika kilimo cha mpunga.

Mapema Mbunge wa Jimbo la Bububu na anakaimu Jimbo la Mtoni, Ndugu Mwatantakaje Haji Juma amesema kuwa bonde hilo lina wakulima zaidi ya 700 kutoka jimbo hilo na maeneo ya jirani.

Ameeleza kuwa mradi wa kilimo kilimo cha mpunga katika bonde hilo ni moja ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015/2020, ambayo viongozi mbali mbali wa jimbo wamekuwa wakitumia rasilimali fedha kuunga juhudi za wananchi ambao ni wakulima wa zao la mpunga.

 Kwa upande wake Katibu wa Jumuiya ya Wakulima wa kilimo cha Mpunga Kizimbani, Shafii Kibwana Said alimshukuru Makamu huyo wa Rais kwa hatua aliyoifanya kuwafuata wakulima hao walioko chini kwa kuwasikiliza changamoto zao na kuonesha nia ya kuzitatua.

Alisema matokeo ya faida walioanza kunufaika nayo kupitia serikali ya CCM ni pamoja na kupata mbolea kwa gharama nafuu ambapo wanajumuiya hiyo wanalipa asilimia 25 ya mbolea huku serikali ikiwalipia asilimia 75.

Wakati huo huo ametembelea  eneo la uhifadhi wa mazingira huko  Fuoni Kibondeni  na kushiriki  katika uvunaji wa kaa, ambapo awasifu juhudi za Jumuiya ya uhifadhi wa mazingira kwa kupanda mikoko ambayo ni sehemu ya kulinda mazingira ya bahari.

Amesema kila mwananchi ana jukumu la kulinda mazingira yasiharibiwe hivyo kitendo cha Wana CCM na wananchi kwa ujumla kujitolea na kuhifadhi mazingira ni hatua muhimu inayotakiwa kuungwa mkono na Chama pamoja na Serikali.

Akiendelea na ziara hiyo pia  ameweka jiwe la msingi Tawi la Fuoni Kibondeni , na kuwasisitiza wanachama wa Chama cha Mapinduzi kuendeleza utamaduni wa kujitolea katika utekelezaji  miradi ya Chama.

Ameelezea kufurahishwa kwake na hatua zilizofikiwa katika Tawi hilo ambalo chimbuko lake limetokana na Tawi la zamani la ASP, lililozalisha wanachama wazalendo na wenye msimamo imara juu ya Chama chao.

Mapema  Katibu wa CCM Mkoa wa Magharib Bi. Aziza Mapuri amemkabidhi taarifa ya hali ya kisiasa ya Mkoa huo iliyoeleza mipango endelevu ya kuimarisha CCM kisiasa, kiuchumi na kijamii itakayokiwezesha Chama hicho kushinda katika uchaguzi Mkuu ujao.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni