Jumatano, 18 Aprili 2018

CCM Z'BAR YAWAFARIJI WANANCHI WALIOATHIRIWA NA MVUA MIKOA YA MAGHARIBI NA KUSINI UNGUJA

 KATIBU wa NEC, Idara ya Organazesheni CCM Zanzibar Ndugu Bakari Hamad Khamis(kulia wa pili) akizungumza na mmiliki wa nyumnba iliyopata madhara ya kubomoka kwa shimo la choo  Bi. Sania Zahor Omar(alikaa chini)  uko Magogoni kwa mabata, katika ziara ya CCM ya kuwatembelea wananchi walioathiriwa na mvua.

  ENEO la  shimo la choo  cha Bi. Sania Zahor Omar mkaazi wa Magogoni kwa Mabata  kilichoanguka kutokana na mvua zinazonyesha visiwani Zanzibar.

 

 VIONGOZI mbali mbali wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Magharibi wakiongozwa na KATIBU wa NEC, Idara ya Organazesheni CCM Zanzibar Ndugu Bakari Hamad Khamis,katika ziara ya Chama ya kuwatembelea wananchi walioathiriwa na mvua katika Wadi ya Pangawe mtaa wa Pangawe bondeni. 
 VIONGOZI mbali mbali wa CCM wakikagua maeneo yaliyoathiriwa na maji ya mvua kutokana na baadhi ya wananchi kuziba mitaro ya kupitisha maji.


VIONGOZI wa Chama cha Mapinduzi pamoja na Diwani wa wadi ya Pangawe ndugu Makame Pandu Mgana wakiangalia mitaro ya maji iliyozibwa na nyumba za makaazi ya wananchi katijka eneo hilo. 

 BAADHI ya nyumba iliyoathiriwa na maji ya mvua zinazoendelea kunyesha uko Fuoni Chunga.

 MUONEKANO wa eneo lililojaa maji ya mvua katika mtaa wa Fuoni Chunga(Janga mizini)

 MUONEKANO wa eneo lililojaa maji ya mvua katika mtaa wa Fuoni Chunga(Janga mizini)

 NYUMBA zilizoathiriwa na maji Fuoni Chunga 

 NYUMBA iliyoangukiwa na mti huko Dimani Tasaf ambayo mmiliki wake ni Ndugu Muhidin Khamis Muhidin.

 NYUMBA iliyoanguka ukuta kutokana na mvua zinazonyesha uko Mtoni kidatu juu ambayo mmiliki wake ni Makame Sheha Juma.

 KATIBU wa NEC, Idara ya Organazesheni CCM Zanzibar Ndugu Bakari Hamad Khamis(kushoto)akisalimiana na Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania-Zanzibar Abdallah Haj Haidar alipowasili katika Mkoa wa kusini kwa ajili ya ziara ya kuwatembelea wahanga wa madhara yaliyosababishwa na mvua.
 KATIBU wa NEC, Idara ya Organazesheni CCM Zanzibar Ndugu Bakari Hamad Khamis, akizungumza na Wana CCM na viongozi wa SMZ wa Mkoa Kusini Unguja katika ziara yake ya kukagua maeneo yaliyoathiriwa na mvua.



 MWENYEKITI wa CCM Mkoa wa kusini Unguja Ndugu Ramadhan Abdalla Ali  akizungumza katika kikao cha dharura kabla ya kuanza ziara ndani ya Mkoa huo.

 MKUU wa Mkoa Kusini Ungua Hassan Hatib Hassan ambaye pia ni mjumbe wa Kamati ya siasa ya CCM Mkoa akitoa tathimini ya athari ya mvua ndani ya Mkoa huo.

 VIONGOZI mbali mbali wakiwemo WANEC na wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Mkoa huo wakifuatilia kwa makini kikao hicho.

 MAAFISA kutoka Afisi Kuu ya CCM Zanzibar walioshirikim ziara hiyo wakifuatilia kwa makini masuala mbali mbali yanayofanyika katika kikao hicho.

 NYUMBA iliyoezuliwa na upepo inayomilikiwa na Seif Salum katika kijiji cha Paje Mkoa wa Kusini Unguja.



 MITI mbali mbali iliyong'olewa na upepo ulioambatana na mvua katika shehia ya Michamvi Mkoa wa Kusini Unguja.


 KITUO cha Afya cha Michamvi kilichoezuliwa na upepo.


NA IS-HAKA OMAR,ZANZIBAR.


CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) imeitaka serikali kuwachukulia hatua za kisheria baadhi ya wananchi wanaojenga kwa makusudi katika mabonde na miundombinu ya maji.

Pia imetaka baadhi ya viongozi wa wadi na shehia ambao ni madiwani na masheha, wanaoshindwa kudhibiti ujenzi holela na vitendo vya uharibifu wa mazingira katika maeneo yao, wawajibishwe kwa mujibu wa sheria.

Ushauri huo umetolewa na Katibu wa NEC, Idara ya Organazesheni CCM Zanzibar  Bakari  Hamad Khamis, alipotembelea maeneo yaliyoathiriwa na mvua za masika katika Mikoa ya Magharibi na Kusini Unguja.

Amesema wakati umefika wa Serikali kuondosha muhali na kuwachukulia hatua kali za kisheria wananchi wanaoharibu miundombinu kwa makusudi na kusababisha maji ya mvua kwenda sehemu zisizostahiki na hatimaye kusababisha mafuriko.

Amebainisha kuwa maeneo mengi yaliyopata majanga hayo yameonekana kuathiriwa na shughuli za kibinadamu zikiwemo uchimbaji wa mchanga, ujenzi holela  na ukataji wa miti ovyo.

Amesema kila mwaka serikali imekuwa ikitoa tahadhari na kuwataka wananchi waliojenga mabondeni wahamie maeneo salama lakini wamekuwa wakikaidi maelekezo hayo.

Amezitaka manispaa hadi Serikali kuu kuratibu maeneo yote yenye historia ya kupata mafuriko kila mwaka pamoja na kutafuta ufumbuzi wa kudumu juu ya changamoto hiyo.

Kupitia ziara hiyo amesema CCM imetoa pole wananchi wote waliopata maafa hayo na kuwataka kuwa wawe wavumilivu katika kipindi hiki kigumu na kitaisimamia Serikali kupitia mfuko wa maafa itoe msaada wa haraka kwa wahanga wa mafuriko hayo.

"CCM ipo bega kwa bega na wananchi wote waliopata maafa haya na tutajitahidi kushirikiana na serikali kuhakikisha hatua za dharura hasa misaada ya kibinadamu inawafikia walengwa.

Lakini pia wananchi nakuombeni sana tujenge utamaduni wa kujilinda na kuchukua tahadhari juu ya matukio kama haya, kwani kuna baadhi ya sehemu nimesikitika kuona nyinyi wenyewe ndio chanzo cha kusababisha mafuriko kutokana na uharibifu wa mazingira na miundombinu mingine", amesema Bakari.

Ameuagiza uongozi wa CCM na UVCCM Mkoa Magharibi kwenda kumsaidia shughuli za ujenzi wa nyumba Mwenyekiti wa CCM Tawi la Buyu Ndugu Matias Theodori ambaye nyumba yake imeporomoka kutokana na mvua hizo.

Akitoa katika ziara hiyo Katibu wa CCM Mkoa wa Magharibi Aziza Mapuri, amesema mvua zinazoendelea kunyesha katika Mkoa huo zinasababisha madhara makubwa kwa wananchi na mali zao na Chama kipo karibu na wananchi wote waliopata maafa hayo.

 Naye Diwani wa wadi ya Pangawe Makame Pandu Mgana ambaye wadi yake ni miongoni mwa sehemu zilizoathiriwa na mvua hizo, amesema kwa kushirikiana na uongozi wa jimbo wanafanya juhudi za kuifanyia matengezo mitaro iliyozibwa kwa shughuli za ujenzi na baadhi ya wananchi.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa Kusini Hassan Hatib Hassan, amesema jumla ya nyumba 106 katika maeneo mbali mbali ya Mkoa huo zimeharibiwa na mvua iliyonyesha April 16, mwaka 2018.

Amesema mbali na nyumba hizo kuna miti ya matunda na ya kawaida, migomba pamoja na mazao ya kilimo yameharibiwa na mvua hizo zilizochanganyika na upepo.

Ameeleza kuwa katika juhudi za kuwafariji wananchi waliopata maafa hayo, uongozi wa Mkoa unaendelea na juhudi ya kuratibu maeneo yote yaliyopata majanga ili mamlaka inayohusika na masuala ya maafa iweze kuchukua hatua za haraka.

Akizungumza katika shehia ya Michamvi Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kusini Unguja, Ramadhan Abdallah Ali amesema Chama Cha Mapinduzi katika Mkoa huo kitaendelea kushirikiana na wananchi wote waliopata maafa hayo mpaka watakaporudi katika hali za kawaida za kuendelea na harakati za kimaendeleo.


Maeneo yaliyotembelewa ni Magogoni kwa mabata, Pangawe, Fuoni jangamizi, Fuoni chunga, Dimani Tasaf, Mtoni kidatu juu,Buyu pamoja na shehia ya michamvi na Paje.




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni