Jumatano, 23 Oktoba 2019

WANAWAKE UWT JIMBO LA DIMANI WAPIGWA MSASA.


 KATIBU wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi Tanzania (UWT) Zuwena Suleiman Mohamed,akizungumza katika ziara hiyo na Viongozi na Wanachama wa UWT Jimbo la Dimani.

 MKUFUNZI wa masuala ya uwezeshaji  kutoka Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Vijana, Wazee, Wanawake na Watoto Zanzibar Zanzibar  Safia Mwinyi, akitoa mada ya uwezeshaji kwa akina Mama wa UWT Jimbo la Dimani.

 WAJUMBE wa Kamati ya Utekelezaji wa UWT Mkoa wa Magharibi kichama wakiwa katika Ofisi ya UWT Jimbo la Dimani Unguja kwa ajili ya ziara maalumu.

 WANAWAKE wa UWT Jimbo la Dimani wakisikiliza nasaha za Uongozi wa UWT Mkoa wa Magharibi waliofanya ziara katika Ofisi ya jimbo hilo.

 MJUMBE wa Kamati ya Utekelezaji ya UWT Mkoa wa Maghabi kichama Ndugu Mwaka Abrahman, akiwasalimia akina mama wa UWT  jimbo la Dimani.

 Mwakilishi wa Viti Maalum Mhe.Zainab Abdalla Salum akitoa akizungumza katika ziara hiyo.


KATIBU wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi Tanzania (UWT) Zuwena Suleiman Mohamed,amewataka kulipa ada zao kwa wakati uliopangwa na umoja huo.

kauli hiyo ameitoa katika ziara ya UWT ya Mkoa huo huko katika Jimbo la Dimani iliyofanyika katika Tawi la CCM Kombeni Unguja, alisema sifa ya uanachama hai inatimia kutokana na ulipaji wa ada wa mwanachama.

Katika maelezo yake Katibu Zuwena, amewasisitiza viongozi hao kufanya vikao kwa mujibu wa Katiba ya UWT ya mwaka 1978 toleo la mwaka 2017.

Akizungumza Mjumbe wa Kamati ya utekelezaji wa Mkoa huo Maulid Mohamed Othman, amewambia wanawake hao waendelee kuhamasisha vijana na wanachama wengine wajitokeze kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura pindi muda wa zoezi hilo utakapofika.

Amesema ushindi wa CCM utatokana na uwepo wa takwimu nzuri za wanachama wenye sifa ya kupiga hivyo kila mwanachama ana wajibu wa kuwa balozi wa kuhamasisha watu wengine wenye sifa za kuiunga mkono CCM.

Akizungumza Mwakilishi wa Viti Maalumu Mkoa wa Magharib kichama Mhe.Mwanaid Kassim Mussa, ametoa wito kwa wanachama hao kuwa wanatakiwa kuwa wamoja ili kuzikabili changamoto za kisiasa na kuhakikisha Chama na Jumuiya zake zinaimarika.


Akitoa mada ya mikopo, mkufunzi kutoka Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Vijana, Wazee, Wanawake na Watoto Zanzibar  Safia Mwinyi, amewataka Wanawake wa UWT kuchangamkia fursa mbali mbali zinazopatikana katika idara ya Uwezeshaji zikiwemo mkopo wenye masharti nafuu na usikuwa na riba.

Amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar  chini ya Uongozi wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,wameimarisha  idara ya uwezeshaji ambayo kwa sasa inatoa mafunzo mbali mbali ya ujasiriamali na kutoa mikopo ya kuwainua wanawake kiuchumi.

Katika ziara hiyo Wawakilishi wa Viti Maalumu wa Mkoa huo ambao ni Mhe. Hamida Abdalla Issa, Mhe.Zainab Abdalla Salum na Mhe.Mwanaidi Kassim Mussa wametoa vitendea kazi kwa Wadi mbili za UWT zilizopo katika jimbo hilo, ambavyo ni Katiba za UWT pamoja na Viti vya Ofisi.
                                                             

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni