Alhamisi, 24 Oktoba 2019

CCM ZANZIBAR YAPOKEA UJUMBE KUTOKA CHAMA CHA CPC CHINA.


NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar Dk.Abdulla Juma Mabodi, akizungumza na ujumbe wa watu watano kutoka Chama cha Kikoministi cha China (CPC), walipowasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar.

NAIBU Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha (CPC) Mhe.Guo Yezhou,akivishwa sikafu na Vijana Maalumu wa UVCCM baada ya kuwasili Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Zanzibar.



NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM)Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi, leo ameupokea Ujumbe wa Watu  watano kutoka Chama Cha Kikoministi Cha China (CPC).

Ujumbe huo umeongozwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha (CPC) Mhe.Guo Yezhou wamewasili kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar.

Viongozi wengine walioshiriki mapokezi hayo ni Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa,Wajumbe wa Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Zanzibar,Wenyeviti wa CCM wa Mikoa,Makamu Wenyeviti wa Jumuiya  na Watendaji wa ngazi mbali mbali za Chama.  

Mara baada ya mapokezi hayo ujumbe huyo uliwasili Afisi Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Kisiwandui Zanzibar na kuweka shada la maua katika kaburi  la Rais wa Kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Marehemu Sheikh Abeid Amani Karume.  

Lengo la ziara ya ujumbe huo kutoka Jamhuri ya Watu wa China ni kuimarisha uhusiano wa kihistoria uliodumu kwa miaka mingi baina ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama Cha Kikoministi cha China (CPC).

Aidha,Viongozi hao wa Vyama hivyo vyenye undugu wa muda mrefu watazungumzia masuala mbali mbali sambamba na kubadilishana uzoefu wa Kisiasa, Kiuchumi,Kijamii. 

 Ziara hiyo ya CPC itakuwa ya siku mbili visiwani Zanzibar.

Maoni 1 :

  1. Mimi maoni yangu naomba tuhakikishe viongozi wa ccm wanazidi kuwa mfano na pia kusimamisha watu walio mfano katika jamii kipindi cha uchaguzi wa serikali za mitaa

    JibuFuta