Jumapili, 6 Oktoba 2019

MAMA SALMA KIKWETE-KIKUNDI CHA UTALII 255 COMMUNITY.


MKE wa Rais Mstaafu wa awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Salma Rashid Kikwete,akiwahutubia waalikwa mbali mbali katika Hafla ya Uzinduzi wa Utalii 255 Community uliofanyika katika ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Shaaban Robert Ilala, Dar es Saalam.

MWENYEKITI wa Kikundi cha Utalii 255 Community Mhe.Angelina Adam Malembeka, akizungumza katika hafla ya Uzinduzi wa Jumuiya ya masuala ya kuhamasisha na kutangaza Vivutio vya Utalii wa ndani, iliyofanyika katika Ukumbi wa Shaaban Robart, Dar es Saalam

 BAADHI ya Wageni mbali mbali walioudhuria hafla ya Uzinduzi wa kikundi cha Utalii 255 Community wakisikiliza nasaha mbali mbali zinazotolewa katika uzinduzi huo.


MKE wa Rais Mstaafu Mama Salma Rashid Kikwete amewasihi Wanawake Nchini kufuata nyayo za  Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Kaskazini Unguja Mhe.Angelina Malembeka katika kubuni miradi mbali mbali yenye maslahi kwa jamii.

Wito huo aliutoa katika uzinduzi wa Kikundi cha Utalii 255 Community huko katika ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Shaaban Robert, Ikala Dar es saalam, ambapo kikundi hicho  kinachojihusisha na masuala ya sekta ya Utalii pamoja na shughuli za jamii katika uzalishaji zikiwemo ujasiriamali. 

Amesema Sekta ya Utalii ni fursa ya kuikomboa Nchi kiuchumi hivyo juhudi zilizofikiwa na Mhe.Angelina zinatakiwa kuthamini na kupongezwa ili zisaidie vizazi vya sasa na vijavyo.

Katika maelezo yeke Mama Salma Kikwete,amekitaka kikundi hicho kufanya kazi zake kwa bidii kubwa kwa lengo la kwenda na mahitaji ya kutangaza vivuti vya Utalii.

Kupitia hafla hiyo ya uzinduzi Mama Salma Kikwete, amewasisitiza Wanawake na Vijana kujitokeza kuwania fursa za Uongozi katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika hivi karibuni.

Pamoja na hayo amewashauri viongozi mbali mbali hasa Wabunge kufungua milango ya Kutangaza Utalii katika maeneo wanayotoka ili kikundi hicho kiwafikie na kuhamasisha jamii juu ya fursa hizo.

Akizungumza Mwenyekiti wa Kikundi cha Utalii 255 COMMNITY  Angelina Malembeka, 
amesema  kikundi cha utalii 255 kilianzishwa mwaka 2017 kimesajiliwa Mambo ya Ndani na cheti cha Utambuzi kutoka Manispaa ya Ilala mwaka 2019.

Amesema lengo la kuanzishwa kwa kikundi hicho ni kuwawezesha vijana wa makundi mbali mbali kunuika na fursa zinazopatikana katika kikundi hicho juu ya masuala ya Utalii sambamba na Ujasiriamali.

Aidha, ameeleza kuwa kikundi hicho kinafanya kazi zake kwa upande wa Zanzibar na Tanzania bara na muundo wa Wanachama wake wanatoka sehemu hizo kwa lengo la kuwaunganisha katika kuzifikia fursa za kukuza uchumi wa nchi.

Akizitaja baadhi ya kazi zinazotekelezwa na kikundi hicho kuwa ni kuelimisha juu ya ajira Binafsi ikiwemo ujasiriamali wa aina mbalimbali ufugaji,kilimo,uchoraji sanaa na kutangaza sekta ya Utalii wa ndani kwa jamii. 

Kwa upande wake Katibu wa Utalii 255 COMMUNITY Eveln Mwakatuma, amesema wanatarajia  kutembelea maeneo mbali mbali nchini, kwa sasa wameandaa safari ya Utalii kwa watoto yatima 100 ambao watakwenda kutembelea mbuga za wanyama watoto 50 kutoka Tanzania Tanzania Bara na 50 Zanzibar lengo la safari hiyo kujionea vivutio vya Utalii Tanzania.

Katika hafla hiyo Viongozi,Wanachama na waalikwa  mbali mbali walikabidhiwa Tuzo za heshima juu ya mchango wao katika kufanikisha shughuli mbali mbali za kijamii,kiuchumi na kimaendeleo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni